WATU 11 wamejeruhiwa vibaya baada ya basi la kampuni ya Taqwa
walilokuwa wakisafiria kutoa Jijini Dar es Salaam kwenda Lubambashi nchini
Congo DRC kugongana uso kwa uso na lori aina ya Center wilayani Mbarali.
Ajali hiyo mbaya ilitokea juzi majira ya saa 2:00 usiku
katika mtelemko wa mlima Mambi katika barabara Kuu ya Mbeya –Iringa wilayani
Mbarali ikihusisha basi la Kampni ya Taqwa lenye namba za usajili T 396 AXZ na
lori aina ya Center lenye namba za usajili T 175 BRA.
Baadhi ya watu walikuwa ndani ya basi hilo walisema kuwa
wakati basi hilo likiwa kwenye mwendo mkali katika mteremko huo, lori aina ya
Center ambalo lilikuwa likipandisha lilijaribu kupita gari lingine lilikuwa
limesimama kando ya barabara, ndipo magari hayo yalipogongana uso kwa uso na
kusababisha basi hilo kupoteza mwelekeo na kupinduka mtaroni.
0 comments:
Post a Comment