BAYERN MUNICH YAICHAPA BARCELONA 2-0 NA KUTWAA KOMBE LA ULI HOENESS
Daniel
van Buyten (katika) akinyanyua juu Kombe la Uli Hoeness, ambalo Bayern
Munich ilitwaa jana usiku baada ya kuichapa Barcelona ya Hispania kwa
mabao 2-0.
Wachezaji wa Bayern wakipozi kwa picha wakiwa na taji la ubingwa wa Kombe la Uli Hoeness ndani ya dimba la Allianz Arena.
Philip Lahm (mwenye beji ya unahodha katikati) akishangilia na wenzake baada ya kufunga bao la uongozi dhidi ya Barcelona.
Kocha wa zamani wa Barcelona, Pep Guardiola anayeinoa Bayern Munich kwa sasa akifuatilia mtanange huo.
Mtokea benchi Lionel Messi wa Barcelona akishindwa kuamini kilichotokea kwa kikosi chake.
Mario Mandzukic (mwenye jezi namba 9) akifunga bao la pili la Bayern katika mechi hiyo.
Lahm kushoto akishangilia bao la uongozi kwa timu ya Bayern Munich.
Thiago (kushoto) na Jerome Boateng (kulia) wa Bayern Munich, wakimdhibiti Lionel Messi.
Frank Ribery wa Bayern Munich akichuana na Marc Bartra wa Barcelona.
Guardiola katika moja ya harakati zake na kikosi chake cha Bayern katika mechi hiyo.
Brass
Band ikitumbuiza kupanga ufunguzi wa pambano la kuwania ubingwa wa
Kombe la Uli Hoeness, ambalo liliisha kwa Bayern kuilaza Barcelona mabao
2-0.
0 comments:
Post a Comment