Chelsea bado yamng'ang'ania Rooney
Wayne Rooney |
KLABU
ya Chelsea inajiandaa kuongeza dau la kumnasa mshambuliaji wa
Manchester United, Wayne Rooney licha ya United kusisitiza kuwa nyota
wao huyo HAUZWI.
Kwa
mujibu wa duru za kimichezo toka nchini England zinasema kuwa Chelsea
wanajiandaa kuweka mezani Pauni Milioni 40 ili kumnasa mchezaji huyo.
Mchezaji huyo amekuwa hana furaha ndani ya United na imedaiwa kuwa anataka auzwe, lakini uongozi unaweka ngumu.
Chelsea
chini ya kocha wake Jose Mourinho imekuwa ikimmezea mate mshambuliaji
huyo tegemeo wa England na imeendelea kusisitiza kuwa inahitaji saini
yake kwa sasa.
Arsenal
pia ilitajwa kuwa katika mbio za kumnasa mkali huyo wa mabao, ikijitapa
wana uwezo wa kumlipa mshahara wake wa pauni 250,000 kwa wiki.Kuna uwezekano mdogo kwa United kulegeza msimamo wake licha kwamba huenda dau hilo litawavutia baada ya timu yao kuandamwa na majeruhi kabla ya kuanza kwa Ligi.
Mfungaji Bora wa EPL, Robin van Persie aliumia wakati United ikilala Asia kwa mabao 3-2 huku Danny Welbeck akitajwa kuwa majeruhi hali inayomtisha kocha David Moyes
0 comments:
Post a Comment