Monday, July 22, 2013

Hatimaye ratiba Ligi Kuu yatoka, Simba, Yanga kuanza na wageni zenyewe kuumana Okt. 20

http://blog.pesatimes.com/wp-content/uploads/2013/06/kochaaa.jpg
Yanga itaendelea kubebana kama hivi katika ligi ya msimu huu itakayoanza Agosti 24?
Na Boniface Wambura
LIGI Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara msimu wa 2013/2014 inatarajiwa kuanza  kutimua vumbi rasmi Agosti 24 mwaka huu kwa timu zote 14 kuwa viwanjani katika miji saba tofauti, ambapo mabingwa watetezi Yanga wataanza kibarua dhidi ya Ashanti United, jijini Dar..

Hata hivyo, kabla ya ligi hiyo kuanza kutakuwa na mechi ya kufungua msimu (Ngao ya Jamii- Community Shield) kati ya bingwa mtetezi Yanga na Makamu bingwa Azam itakayochezwa Agosti 17 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mbali na pambano la Yanga na Ashanti litakalopigwa kwenye uwanja wa Taifa, siku hiyo ya ufunguzi wa ligi hiyo, Mtibwa Sugar na Azam zitaonyeshana kazi kwenye Uwanja wa Manungu, Morogoro huku JKT Oljoro na Coastal Union zitapepetana mjini Arusha kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid.

Simba wenyewe wataanzia ugenini mjini Tabora kuumana na 'wageni' Rhino Rangers, kwenye uwanja wa Ally Hassani Mwinyi, wakati  Mgambo Shooting itaialika JKT Ruvu katika Uwanja wa Mkwakwani, mjini Tanga huku wageni wengine wa ligi hiyo Mbeya City watakuwa nyumbani mjini Mbeya kuikaribisha Kagera Sugar katika uwanja wa Soikoine na Ruvu Shooting na Tanzania Prisons zitaumana Mabatini, Mlandizi.

Pambano la watani wa jadi nchini lenyewe kwa raundi ya kwanza litachezwa Oktoba 20 ambapo Simba watakuwa wenyeji kabla ya kurudiana mwakani April 27, katika moja ya mechi za kufungia msimu Yanga wakiwa ndiyo wenyeji wa pambano hilo.

Mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo utamalizika Novemba 3 mwaka huu wakati wa pili utamalizika Aprili 27 mwakani
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu