NMB YAFADHILI SEMINA YA MAAFISA MAENDELEO WA VIJANA NCHINI
Benki
ya NMB imefadhili semina kubwa iliyohusisha maafisa maendeleo wa vijana
kutoka nchi nzima.Semina hii ambayo ilikua ni ya siku mbili ilifanyika
katika kumbi za uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam. Mhe. Dkt.Fenella Mukangara ambae ni Waziri wa Habari,Vijana, Utamaduni na Michezo alizindua
rasmi semina hii na kuishukuru Benki ya NMB kwa ufadhili mkubwa ambao
wamejitolea ili kufanikisha semina. Dhumuni la semina ni kujadili maendeleo ya vijana kuanzia ngazi ya halmashauri,kuimarisha utendaji kazi kwa vijana wa mikoa na wilaya.
Katibu Mkuu Wizara ya Habari ,Vijana,Utamaduni na Michezo Bw. Seth Kamuhanda akifafanua jambo wakati wa semina hiyo.Meneja wa NMB Mikopo Midogo Midogo Bw. Mashaga Changarawe akielezea huduma mbali mbali zitolewazo na Benki ya NMB zikiwemo akaunti pamoja na mikopo mbalimbali kwa wajasiriamaliMeneja Mawasiliano wa
NMB, Josephine Kulwa akizungumzia jinsi ambavyo Benki ya NMB kwa
kupitia huduma zake kwa wajasiliamali inavyosaidia kuongeza ajira kwa
vijana nchiniErick Shigongo nae alitoa maada kuhusiana mafanikio na kujitambua katika ajira.
Sehemu ya washiriki wa semina hiyo.
0 comments:
Post a Comment