Tuesday, July 23, 2013

Shiwata watakiwa kuchangia ujenzi nyumba zao Mkuranga



Na Mwandishi Wetu

MTANDAO wa Wasanii Tanzania (SHIWATA) umewataka wanachama wake kuchangia ujenzi wa nyumba zao katika kijiji cha Mwanzega, Mkuranga ili kukamilisha mradi huo.


Mwenyekiti wa Mtandao wa Wasanii Tanzania (SHIWATA), Caasim Taalib alisema jana Dar es Salaam katika mkutano wa wanachama wanaochangia ujenzi ambapo mpaka sasa nyumba 29 zimekamilika na wanachama 220 wamechangia ujenzi na jumla zilizokusanywa ni mil. 82.5.

Alisema SHIWATA haina fedha za kujenga nyumba za wanachama wake wala haina chanzo cha mapato kama si kwa njia ya kuchangishana na baada ya hapo kuwakabidhi wale waliokamilisha uchangiaji wa ujenzi wa nyumba hizo.

‘Ujenzi wa nyumba za wasanii utafanikiwa kwa kila mwanachama kuchangia nyumba yake kwa kujiaminisha kuwa hakuna utapeli wala biashara katika gharama za ujenzi wa nyumba hizo’alisema Taalib.

SHIWATA ambayo inaundwa na wasanii, wanamichezo, wanahabari na vijana wapatao 7,000 ilikuwa ikabidhi nyumba Agosti mwaka huu kwa mchezaji wa zamani wa Timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’, Jellah Mtagwa na wasanii wengine 14 ambao wamekamilisha michango ya ujenzi  wa nyumba zao katika kijiji chao cha Mwanzega Kimbili, Mkuranga.
Wengine watakaokabidhiwa nyumba zao ni msanii maarufu nchini, Lumole Matovola ‘Big’ wa Bongo movie ambaye ni mwanachama wa SHIWATA wangine ni Mwandishi wa Habari, Josephine Moshi, Farida Ndimbo wa Jeshi la Magereza, Flora Kafwembe wa JKT Mgulani na Nyanza Kisadugwa wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ). 

 Mpaka sasa SHIWATA imejenga nyumba 29 kwa ajili ya wasanii katika eneo la hekari 300 na wanajiandaa kulima shamba la hekari 500 walizonazo ili kujikwamua kimaisha.
              
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu