Thursday, September 19, 2013

Baby Madaha alamba 'bingo' Kenya

baby Madaha
Bosi Mpya wa Madaha, Joe Kariuki
MSHIRIKI wa zamani wa BSS, Baby Madaha amelamba 'bingo' baada ya kuingia mkataba wa miaka miwili wa kufanya kazi na kampuni na Candy n Candy Records ya nchini Kenya wenye thamani ya Sh. Mil 20 za Kenya ambazo ni sawa na Sh. Mil 50 za kitanzania.
Mbali na donge hilo, pia kampuni hiyo inayoongozwa na Mkurugenzi wake, Joe Kariuki imepa msanii huyo anayetamba kwenye fani ya muziki na filamu nchini, gari aina ya Audi TT.
Akizungumza na MICHARAZO, Baby alisema mkataba huo aliingia hivi karibuni na kampuni hiyo na tayari ameshafyatua kazi mpya kupitia kampuni hiyo iitwao 'Summer Holiday' ambao anatarajia kuizindua rasmi Oktoba 6 jijini Dar es Salaam.
Baby alisema uzinduzi huo utakaoambatana na 'party' ya kusherehekea mafanikio yake kisanii itafanyika kwenye ukumbi wa Dar Live na kusindikizwa na burudani za wasanii mbalimbali.
"Nimeingia mkataba wa miaka miwili wa kufanya kazi nchini Kenya kupitia kampuni ya Candy n Candy ambayo mbali na fedha pia wamenipa usafiri na tayari nimeshatoa kazi chini yao  iitwayo Summer Holiday iliyoanza kutamba kwenye vituo vya Channel O na MTV," alisema.
Msanii huyo aliyeibuliwa na shindano la BSS 2007, alisema anajisikia fahari kuwa msanii wa kwanza wa kike nchini kupata mkataba mnono kama huo nchini Kenya na imani yake ni mwanzo wa safari yake kuelekea kwenye kilele cha mafanikio kimuziki.

Barafu, Mzee Majuto waja na Daladala pamoja na Monalisa

Kava la filamu mpya ya msanii Barafu
Barafu
BAADA ya kuwatumikia wenzake kwa muda mrefu, hatimaye msanii mahiri wa filamu, Seleman Abdallah 'Barafu' ameibuka na kazi yake binafsi iitwayo 'Daladala' inayozungumzia mikasa, vituko na kero zote zilizopo ndani ya usafiri huo wa umma.
Ndani ya filamu hiyo, mkali huyo ameigiza na wasanii wakongwe nchini kama Amri Athuman 'King Majuto', Yvonne Cherly 'Monalisa' na wengine.
Akizungumza na MICHARAZO Barafu anayefahamika pia kama 'Mzee wa Land Rover', alisema hiyo ni kazi ya kwanza kwake kuuitoa kupitia kampuni yake iitwayo 'Mtafuna Films Production' na ni 'serious comedy'.
Barafu alisema, anatarajiwa kuitoa hadharani filamu hiyo wiki mbili zijazo, na kuwataka mashabiki kujiandaa kupata burudani na 'kuvunjika mbavu' kwa namna walivyoiigiza filamu hiyo na hasa vimbwanga vya Mzee Majuto.
"Kwa wale ambao wavijua vituko vya Mzee Majuto wajiandae kuumia zaidi kwa namna mzee huyo, mimi na Monalisa tulivyofanya mambo makubwa katika filamu hii ya 'Daladala'," alisema.
Barafu alisema baada ya kutoka kwa 'Daladala' ataanza maandalizi ya kazi zake nyingine kupitia kampuni yake mbali na zile za kushirikishwa na wenzake ambazo alidai hawezi kuziacha.

Chelsea hoi darajani, Barca 'yaua', Arsena yatakata

All smiles: Messi celebrates his opener with defener Dani Alves
Messi akishangilia moja ya mabao yake usiku wa kuamkia leo
Sulley Muntari
Sulley Muntari akishangilia bao la ushindi la Ac Milan alilofunga lala salama
Matchwinner: Marco Streller (second right) steals in at the near post to head Basle's decisive second goal
Basel wakijipatia bao la pili lililoizamisha Chelsea 'darajani' huku Mourhino akipewa ujumbe kupitia mabango kwamba Mata atatakiwa awe uwanjani na siyo kwenye benchi.
 Rumblings of discontent: A Chelsea fan shows his displeasure at Juan Mata's lack of first-team action
WAKATI Jose Mourinho na vijana wake wa Chelsea wakianguka 'darajani' kwa kulala mabao 2-1 mbele ya Basel ya Uswisi, Lionel Messi ameendelea kuboresha rekodi yake ya mabao baada ya kufunga 'hat trick' wakati Barcelona ikiizamisha Ajaz kwa mabao 4-0.
Chelsea ilikumbana na kipigo hicho na kuifanya icheze mechi nne bila kupata ushindi, japo walianza kutangulia katika mechi hiyo iliyochezwa Stanford Bridge kupata bao kupitia Oscar kabla ya Basel kusawazisha mabao yote katika kipindi cha pili.
Mabao ya washindi hao ambao wamekuwa wakizisumbua timu kubwa kila mara katika michuano hiyo, yalifungwa na Salah dakika ya 71 na Streller dakika ya 82.
Katika mechi nyingine Barcelona ikiwa uwanja wake wa nyumbani iliisasambua Ajax ya Uholanzi kwa kuishindilia mabao 4-0, huku 'mchawi mweupe' Messi akitumbukiza mara tatu na kuondoka na mpira wake nyumbani.
Bao jingine la mabingwa hao wa Hispania lilifungwa na Gerard Pique, ilihali Arsenal wakiwa ugenini nchini Ufaransa walitakata baada ya kupata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Olympique Marseille nao Ac Milan ikiwa nyumbani ilifunga Celtic mabao 2-0.
Mecchi nyingine matokeo yake ni Schalke 04 kuilaza Steau Bucharest mabao 3-0, Napoli kuitafuna Borussia Dotmund ya Ujerumani mabao 2-1 nchini Italia, kadhaalika Atletico Madrid wakitakata nyumbani kwa kuilaza Zenit kwa mabao 3-1na Porto ya Ureno kushinda ugenini mbele ya wenyeji wa Austria Wien.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu