Sunday, September 22, 2013

Happiness Watimanywa ndiye Redd's Miss Tanzania 2013


MISS Tanzania 2013, Happiness Watimanywa akipunga mkono mara baada ya kuvikwa taji la Redd’s Miss Tanzania 2013 usiku wa Septemba 21, Ndani ya Ukumbi wa Mlimani City na kuwashinda warembo wenzake 29.
Na Father Kidevu Blog
HATIMAYE kitendawili cha nani atanyakua taji la Redd’s Miss Tanzania 2013 kimeteguliwa usiku huu na mrembo Happiness Watimanywa kutoka Mkoa wa Dodoma na Kanda ya Kati kufanikiwa kutawazwa Mshindi wa taji hilo na kuwashinda warembo wengine 29 waiokuwa wakiwania taji hilo.
Nyota ya Happiness ilionekana dhahiri kung’aa vyema katika fainali hizo mwaka huu tangu pale alipofanikiwa kutwaa taji la Miss Tanzania Photogenic 2013 na kuwa mrembo wa kwanza kuingia nusu fainali.
Wakati Happiness akinyakua Taji hilo pamoja na zawadi ya Gari na kitita cha shilingi Milioni 8 nafasi ya pili ilikwenda kwa mrembo Latifa Mohamed kutoka Kitongoji cha Kigamboni na Kanda ya Temeke na nafasi ya Tatu ikienda kwa Miss Tanzania Sports Woman, Clara Bayo.
Pamoja nao warembo wengine walio ingia hatua hiyo ya tano bora ni Lucy Tomeka na Elizabeth Prety.
Hii ndio tano bora ya Redd's Miss Tanzania 2013. Je nani hapa ataondoka na taji, gari na kitita cha Milio ni 8? Warembo hao kutoka kushoto ni Happiness Watimanywa (Miss Photogenic), Elizabeth Pretty, Clara Bayo (Miss Sports Women), Lucy Tomeka na Latifa Mohamed.

Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu