MAJOGOO WA JIJI WAWADONOA MASHETANI WEKUNDU 1-0
Wachezaji
wa Liverpool wakishangilia bao la Daniel Sturridge lililoipa ushindi wa
1-0 dhidi ya Manchester United kwenye Uwanja wa Anfield. Huo ni ushindi
wa tatu mfululizo kwa Liverpool tangu kuanza kwa msimu, matokeo
iliyowahi kupata miaka 19 iliyopita. (Picha kwa Hisani ya Gazeti la
Daily Mail la Uingereza)
Sturridge
akishangilia bao pekee la Liverpool, alilofunga leo. Ushindi huo
umekuja wakati ambao mshambuliaji huyu anaadhimisha miaka 24 ya kuzaliwa
kwake leo Septemba 1.
Sturridge
akidondoka baada ya kupiga kichwa kufunga bao hilo akiunganisha pasi ya
kichwa ya Daniel Agger aliyeunganisha kona ya Steven Gerrard.
Sturridge akikumbatiana na kocha wa Liverpool Brendan Rodgers baada ya kuifungia timu yake bao la ushindi.
Mashabiki
wa Liverpool wakiwa wamekaa jukwaani kuunda picha na kuandika namba 100
ambayo ini idadi ya miaka ambayo nguli wa zamani aliyezaliwa Septemba
2, Bill Shankly ilikuwa aitimize, ingawa alifariki kabla.
Steven Gerrard wa Liverpool, akitunishiana msuli na Robin van Persie wa Man United wakati wa mechi hiyo.
Martin
Skrtel (37), ambaye aliingia kujaza pengo la majeryhi Kolo Toure,
akiruka juu kuwania kupiga mpira wa kichwa kuondoa hatari langoni mwa
Liverpool.
Steven Gerrard akipiga adhabu ndogo.
Kocha
wa timu ya taifa ya England, Roy Hodgson (wa pili kulia) akifuatilia
mtanange huo wa kukata na shoka kwenye dimba la Anfield.
Mshambuliaji Luis Suarez wa Liverpool, akiangalia mechi hiyo akiwa jukwaani.
Kocha wa Liverpool, Rodgers (kulia) na wa Manchester United David Moyes wakitoa maelekeo kwa wachezaji wa vikosi vyao.
0 comments:
Post a Comment