Msiba tena! Mwanajeshi mwingine wa Tanzania afariki Congo
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Davis Mwamnyange |
MSIBA tena! Hizi ni habari za kusikitisha kusikia, ila ni kwamba shujaa mwingine wa Tanzania amefariki dunia katika harakati za kulinda amani ya waafrika wenzetu.
Habari zilizotolewa na Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) zinasema mwanajeshi anayetambulika kwa jina la Private Hugo Munga, ambaye alijeruhiwa kwenye shambulio lilisababisha Meja Khatibu kufariki dunia, naye amefariki.
Mwanajeshi huyo alikuwa nchini South Africa kwa ajili ya matibabu, lakini kwa bahati mbaya Tanzania imempoteza shujaa huyu.
Mwili wake unatarajiwa kufikishwa hapa nyumbani kesho ukitokea nchini South Africa.
Polisi Dar wapiga marufuku maandamano ya Wapinzani, kisa...!
Kamanda Suleiman Kova |
JESHI la Polisi Jijini Dar es Salaam limeyapiga marufuku maandamano ya umoja wa
vyama vya CUF, NCCR na CHADEMA yaliyopangwa kufanyika kesho Jumamosi.
Maandamano hayo yaliyokuwa yamepangwa
kuanzia Tazara hadi Jangwani kisha Mwenge hadi Jangwani na sehemu mbalimbali .Taarifa iliyotolewa na Kamanda Polisi Kanda Maalum ya Mkoa wa Dar es Salaam, Suleiman Kova kupitia ITV imeeleza kuwa Polisi wamechunguza na kugundua kwamba maandamano hayo yataleta usumbufu kwa watu wengine na kwamba kwa kuwa lengo ni kufika Jangwani basi Viongozi wa vyama hivyo wawaambie wafuasi wao waende Jangwani bila Maandamano.
0 comments:
Post a Comment