Sunday, September 8, 2013

MWANAMUZIKI AZONTOKUTUMBUIZA DAR KESHO





Zantel yamleta mkali wa Azonto Dar es Salaam

  • Kutoa burudani kali viwanja vya Posta kesho

Mwanamuziki mashuhuri kutoka nchini Ghana, Fuse ODG, kesho anatarajiwa kutoa burudani kali kwenye viwanja vya Ustawi wa Jamii hapa jijini Dar es Salaam.

Mwanamuziki huyo ambaye anatamba na wimbo wake wa Azonto, analetwa kwa ushirikiano wa kampuni ya simu za mikononi ya Zantel, pamoja na Times FM.

Burudani hiyo inatarajiwa itaanza kuanzia mida ya saa mbili usiku hadi majogoo kwa kiingilio cha shilingi elfu kumi kwa kununua tiketi kabla na elfu kumi na tano kwa watakao nunua tiketi mlangoni.

Akimzunguzia mkali huyo, Afsa Biashara Mkuu wa Zantel, Sajid Khan, alisema Zantel imemleta msanii huyo ili kuwapa ari wasanii wa ndani wenye lengo la kufikisha kazi zao hatua za kimataifa.

‘Zantel imekuwa msitari wa mbele katika kuwawezesha wasanii wa ndani, hasa vijana, na kwa kumleta Fuse ODG, ambaye ni mmoja wa wasanii wachache kutoka Afrika waliofanikiwa kufikisha mziki wao soko la kimataifa tunaamini vijana watajifunza mengi’ alisema Khan.

Fuse ODG ni mwanamuziki wa Ghana mwenye makazi nchini Uingereza, ambaye wimbo wake wa Azonto ulifanikiwa kuwa namba moja kwenye iTunes World Chart, akiwa ni mwanamuziki wa kwanza kutoka Ghana kufikia mafanikio hayo.

Kwa wimbo wa Azonto pekee, Fuse ODG alifanikiwa kupata watazamaji zaidi ya milioni kumi na moja kwenye You Tube kwa mwaka 2012.

Naye Mkurugenzi wa Times FM, Rehure Nyaulawa, alisema wamemleta msanii huyo ili kuhakikisha watanzania wanapata burudani wanayoipenda ya Azonto hapa hapa nchini.

‘Azonto imejipatia umaarufu mkubwa karibu dunia nzima, lakini pia kwa upande wa radio yetu wimbo huu umepata maombi mengi kuliko wimbo wowote wa kimataifa kiasi cha kuona tuwaletee watanzania burudani wanayoipenda’ alisema Nyaulawa.

Fuse ODG atasindikizwa na wasanii wote wa kundi la BHitz, Mshindi wa Epiq BSS Walter Chillambo, Menina pamoja na wasanii wa Marco Chali Foundation.

Wimbo wake mpya wa Antena ambao amemshirkisha Wyclef Jean unafanya vizuri kwenye chati mbalimbali duniani kwa sasa.








Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu