Sunday, March 31, 2013

BREKING NEWZZZZZZZZ HIVI SASA

0 comments
wakati wa uokoaji unaendelea kwa kasi mpaka hivi sasa Iadadi za maiti zilizopatikana ni 28 kwa mujibu wa taarifa zilizotufikia tutazidi kuwaletea habari zaidi endelea kuangalia blog yenu 
Endelea Kusoma >>

SHEREHE YA PASAKA LEO

0 comments


 MHASHAMU Askofu  wa kanisa Katoriki jimbo la Morogoro Telesphori Mkude,akihutubia mamia ya waumini wa kanisa hilo katika ibada pasaka ya  kuzaliwa kwa  Yesu kristo   iliyofanyika katika kanisa la Mtakatifu  Patriki Mjini Morogoro,



 Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mke wake Mama Salma Kikwete wakiwa  katika wodi ya Sewa haji ya Taasisi ya Mifupa ya MOI katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam leo Machi 31, 2013 wakimjulia hali na kumpa pole Bw. Selemani Saidi, mmoja wa majeruhi walionusurika katika jengo lililoporomoka katikati ya jiji Ijumaa iliyopita na kusababisha vifo vya watu 28 Kushoto mwenye suti nyeusi ni Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Mhe. Raymond Mushi Kulia ni Daktari C.N. Mcharo wa taasisi ya Mifupa ya Moi.


Baadhi ya watu mbalimbali waliofika katika chumba cha kuhifadhia maiti kwa aajili ya kutambua ndugu zao waliokufa kwa ajali ya kuangukiwa na ghorofa 


Baadhi ya waumini wa kanisa la St Joseph jijini Dar es salaam wakitoka katika ibada ya Pasaka leo 

Muuguzi mkunga Fatuma Uwesu wa Hospitali ya Mwananyamalakulia akimpa chanjo mtoto ambaye aliezaliwa katika mkesha wa pasaka kushoto ni mama wa mtoto huyo Maria Weus leo


 Masita wa Kanisa Katoliki Jimbo la Dodoma wakisikiliza mahubiri ya Askofu Gervas Nyaisonga jana katika kanisa  la Mt Paulo wa Msalaba Dodoma mjini

 Askofu mkuu wa kanisa la Injili la KKKT Dr Alex Malasusa akimbariki mtoto wakati wa ibada ya Pasaka leo


 Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mke wake Mama Salma Kikwete wakiwasili katika wodi ya Taasisi ya Mifupa ya MOI katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam kuwajulia hali vijana Mohamed Ally Dhamji (kushoto), Baqir Virani, ambaio ni kati ya  majeruhi walionusurika katika jengo lililoporomoka katikati ya jiji Ijumaa iliyopita na kusababisha vifo vya watu 28 mpa leo



Baadhi ya waumini wa kikristo wa kanisa la kkkt la Azania wakielekea katika kutoa sadaka wakati wa ibada ya Pasaka leo
Endelea Kusoma >>

Saturday, March 30, 2013

MAZISHI YA MBUNGE WA CHAMBANI

0 comments
 Waziri mkuu mstaafu Edward Lowasa akiweka udongo wa mwisho  kwenye kaburi  aliekuwa mbunge wa chambani salim hemd Khamis aliezikwa chambani mkoani pemba 
 Watu mbalimbali wakibeba jeneza la aliekuwa mbunge wa jimbo la chambani Salim hemed Khamis  m\chambani mkoani pemba
Endelea Kusoma >>

AJALI YA GHOROFA LILILOANGUKA IDADI NI 20 WALIOKUFA

0 comments
Baadhi ya ndugu mbalimbali waliofika katika hospitali ya Taifa  Muhimbili na kutambua miili ya ndugu zao wengi waliofika chumba cha kuhifadhia maiti na kutambua ndugu hao walioangukiawa na ghorofa ajali iliyotikea jana picha  ndugu wakichukua mwili wa ndugu yao leo0 akwenye hospitali hiyo jumla ya maiti zilipatikana ni 20 mpaka saa nane maiti zilizotambuliwa ni 8  ambao  waasia  ni  3 na wengine ni 5  wafanyakazi wa chumba cha maiti pamoja na ndugu wanaofika wanashindwa kuwatambua ndugu zao kutokana na miili yao kuharibika sana wengine  baadhi ya viungo vimekatika huwezi kuviona wakatoa mifano kichwa mikono  na viungo vingine wafanyakazi hao hawakutaka kutaja majina yao  tutaendelea kuwajulisha 

Endelea Kusoma >>

JUMUIYA WAISLAM WATOA DAMU KUWASAIDIA WAGONJWA

0 comments
Jumuia ya Waislam kitengo cha Afya na Ustawi  wa jamii (Jumuiyatul-Akhalaaqul=Islaam (JAI) Taasisi isiyo ya kiserikali leo walijitolea Damu ili kuwasaidia wagonjwa wa jinsia zote  madhehebu zote na imani zote na wagonjwa walio mawodini na majumbani Taasisi hiyo ilitoa damu katika kitengo cha Damu salaama kilichopo Muhimbili

picha imuonyesha mhudumu wa kitengo cha damu salaam Mariam Kabona akimtoa damu Dk Nassir Rajabu Khamisi leo



Endelea Kusoma >>

BREKING NEWZZZZZZZZZZZ

0 comments
Katika ukoaji unaondelea kwenye jengo lililoanguka jana jumla ya maiti nane 8 zimepatikana kwa mujibu ya mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Said Meck Sadick huku juhudi zinaendelea na kuongezea nguvu na vifaa mbalimbali vilivyongezwa tutaendelea kukufahamisheni kadri inapotokea usikose
Endelea Kusoma >>

Friday, March 29, 2013

WAKOAJI WAKIENDELEA KUOKOA

0 comments
Askari wa Jkt wakiwasili kusaidia uokoaji 
 Askari wa Kampuni binafsi wakisaidia kutafuta miili ndani ya kifusi
 Maiti ikitolewa ndani ya kifusi

Mmoja wa mafundi waliokuwa wanaendelea na ujenzi wa Jengo hilo, Said Hassan akiwa ameokolewa
Endelea Kusoma >>

RAIS JAKAYA KIKWETE ATEMBELEA JENGO LILILOANGUKA LEO

0 comments







 : Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa  mtaa wa Indira Ghandi jijini Dar es salaam leo akiwa ameongozana na mkewe Mama Salma Kikwete kujionea mwenyewe jengo lililoporomoka asubuhi saa mbili na nusu leo Machi 29, 2013 ambapo hadi Rais anafika mahali hapo saa saba kamili watu wawili wamethibitishwa kuwa wamekufa na wengine 19 kujeruhiwa, wawili wakiwa mahututi. Juhudi zinaendelea kuokoa watu wanaosadikiwa kunaswa kwenye kifusi cha jengo hilo lililokuwa limefikia ghorofa ya 15, likijengwa ubavuni mwa Msikiti wa Shia Ithnaasheri.



 : Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipata maelezo toka kwa Mkuu wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es salaam Bw. Suleiman Kova na Mkuu wa Mkoa huo Mhe saidi Meck Sadiki katika eneo la  jengo lililoporomoka mtaa wa Indira Ghandi jijini Dar es salaam  asubuhi saa mbili na nusu leo Machi 29, 2013 ambapo hadi Rais anafika mahali hapo saa saba kamili watu wawili wamethibitishwa kuwa wamekufa na wengine 19 kujeruhiwa, wawili wakiwa mahututi. Juhudi zinaendelea kuokoa watu wanaosadikiwa kunaswa kwenye kifusi cha jengo hilo lililokuwa limefikia ghorofa ya 15, likijengwa ubavuni mwa Msikiti wa Shia Ithnaasheri
: Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa  mtaa wa Indira Ghandi jijini Dar es salaam leo akiwa ameongozana na mkewe Mama Salma Kikwete kujionea mwenyewe jengo lililoporomoka asubuhi saa mbili na nusu leo Machi 29, 2013 ambapo hadi Rais anafika mahali hapo saa saba kamili watu wawili wamethibitishwa kuwa wamekufa na wengine 19 kujeruhiwa, wawili wakiwa mahututi. Juhudi zinaendelea kuokoa watu wanaosadikiwa kunaswa kwenye kifusi cha jengo hilo lililokuwa limefikia ghorofa ya 15, likijengwa ubavuni mwa Msikiti wa Shia Ithnaasheri.






 Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakisindikiwa na  Mkuu wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es salaam Bw. Suleiman Kova baada ya kutembelea eneo la  jengo lililoporomoka mtaa wa Indira Ghandi jijini Dar es salaam  asubuhi saa mbili na nusu leo Machi 29, 2013 ambapo hadi Rais anafika mahali hapo saa saba kamili watu wawili wamethibitishwa kuwa wamekufa na wengine 19 kujeruhiwa, wawili wakiwa mahututi. Juhudi zinaendelea kuokoa watu wanaosadikiwa kunaswa kwenye kifusi cha jengo hilo lililokuwa limefikia ghorofa ya 15, likijengwa ubavuni mwa Msikiti wa Shia Ithnaasheri.

PICHA NA IKULU

Endelea Kusoma >>

KUAGA MWILI WA ALIEKUWA MBUNGE WA CHAMBANI SALIM HEMED KHAMIS LEO

0 comments
.
 Rais Jakaya Kikwete, Makamu wake Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Waziri Mstaafu, Edward Lowasa, na viongozi wengine wakishiriki shughuli ya kuaga mwili wa marehemu Salim Hemed Khamis, aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Chambani Visiwani Pemba kupitia CUF, aliyefariki jana mchana katika Hospitali ya Taifa Muhimbili. Shughuli za kuaga mwili wa marehemu zimefanyika kwenye Ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam, leo Machi 29, 2013. Picha na OMR

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na baadhi ya ndugu wa marehemu wakati viongozi wakiondoka kwenye ukumbi wa Karimjee baada ya kushiriki katika shughuli za kuaga mwili wa marehemu, aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Chambani Visiwani Pemba, Salim Hemed Khamis (CUF), aliyefariki jana katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.
 Rais Jakaya Kikwete, Makamu wake Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge) William Lukuvi, na Naibu Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika, Adam Malima, wakizungumza nje ya ukumbi wa Karimjee, baada ya kushiriki shughuli ya kuaga mwili wa marehemu,Salim Hemed Khamis, aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Chambani Visiwani Pemba kupitia Chama cha CUF, aliyefariki jana katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.
Waombolezaji wakibeba jeneza lenye mwili wa marehemu,Salim Hemed Khamis, aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Chambani Visiwani Pemba kupitia Chama cha CUF, aliyefariki jana katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, wakiingiza kwenye gari tayari kuelekea uwanja wa ndege kwa safari ya kuelekea Pemba kwa maziko, yatakayofanyika leo. 

*BREAKING NEEEWZ!!! JENGO LA GHOROFA 14 LAPOROMOKA DAR LAFUKIA WATU KADHAA

 Jengo la Ghorofa 14 lililokuwa likiendelea kujengwa pembeni kabisa mwa Msikiti wa SHIA Mtaa wa INDRA GHAND na Zanaki, limeporomoka na kusambaratika na kusababisha vifo vya watu kadhaa ambao hadi sasa idadi haijaweza kupatikana kutokana na waokoaji kukosa vifaa vya kutosha katika zoezi hilo la uokoaji. Imeelezwa kuwa ghorofa hilo limeporomoka leo asubuhi majira ya saa moja na nusu ambapo ulianza kusikika mlio kama 'Tetemeko la ardhi'. 
Aidha imeelezwa kuwa katika Jengo hilo walikuwepo mafundi ambao walikuwa wakiendelea na ujenzi na chini alikuwepo Mama Lishe, aliyekuwa akiuza chai na eneo hilo pia walikuwapo watoto wadogo ambao haikuweza kufahamika idadi yao waliokuwa wakicheza eneo hilo, ambao wote inasemekana wamefukiwa na kifusi cha ghorofa hilo, huku waokoaji wakifanikiwa kumpata mtoto mmoja tu ambaye hata hivyo imeelezwa hali yake ilikuwa ni mbaya na kuwahishwa hospitali.
 Ni moja ya Kifaa pekee kilichokuwepo eneo hilo Trekta, likifukua kifusi ili kuokoa watu wanaodaiwa kufukiwa na kifusi hicho.
 Baadhi ya watu waliwahi kufika kujaribu kutoa msaada bila mafanikio hapa wakiwa wamekwama baada ya kukosa vifaa vya kutosha.
 Wahindi nao walikuwapo kutoa msaada hapa wakilielekeza Trekta kusogea mahala walipo wao wakihisi kuwa kuna mtu mahala hapo.
 Waokoaji wakijitahidi kutumia mikono kuondoa kifusi hicho ili kuweza kuwaokoa watu waliofukiwa.
 Trekta likiendelea kuondoa kifusi hicho.
 Waokoaji wakiwa hoi......
 Juhudi zinaelekea kulala.........
 Moja kati ya magari yaliyokuwa eneo hilo likiwa limeangukiwa na mabaki ya jengo hilo.
 Trekta likiendelea kuondosha kifusi......../
 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadik, akihojiwa na wanahabari kuhusu tukio hilo.
 Moja ya ghorofa lililo karibu kabisa na jengo hilo lililoanguka nalo likiendelea kujenga nalo pia likiwa na ghorofa 14.....
 Sehemu ya wananchi wakishuhudia tukio hilo.
Vijana wakishusha mitungi ya gesi ili kuwasaidia kukata nondo.... baada ya kuona vimekosekana vifaa vya haraka.
Endelea Kusoma >>
0 comments

MAITI ZAIDI YA 10 NA MAJERUHI 30 TU WACHOMOLEWA HADI SASA KATIKA MABAKI YA JENGO LA GHOROFA 16 LILILOPOROMOKA JIJINI DAR ES SALAAM LEO ASUBUHI HII NA KUWAFUNIKA WATU KIBAO WAKIWAMO MAFUNDI WALIOKUWA WAKIENDELEA KULIJENGA... NI JIRANI NA MSIKITI WA SHIA MAKUTANO YA MOROGORO ROAD NA INDIRA GANDHI... HARAKATI ZA KUCHOMOA MAJERUHI NA MAITI ZAIDI ZINAENDELEA ZIKIONGOZWA NA VIONGOZI KADHAA WA SERIKALI AKIWAMO RC DAR, SAID MECK SADICK

Mashuhuda wakiangalia jengo lililoporomoka asubuhi hii katika makutano ya Morogoro Road na Indira Gandhi jijini Dar es Salaam leo asubuhi Machi 29, 2013.
Maafa makubwa yametokea jijini Dar es Salaam leo baada ya jengo la ghorofa 16 lililokuwa likiendelea kujengwa kuporomoka na kuwafunika watu wanaokadiriwa kuwa zaidi ya 6o

Tukio hilo limetokea mishale ya asubuhi katika mitaa ya Posta, jirani na msikiti wa Shia katika eneo la makutano ya Morogoro Road na Indira Gandhi na hadi sasa, miili ya maiti 12 na pia majeruhi 30 wameshachomolewa.

Aidha, harakati zaidi za uokoaji zingali zikiendelea kufanywa na vikosi vya uokoaji. Katika eneo la tukio hilo, tayari viongozi kadhaa wa serikali na makamanda wa Polisi katika kanda maalum ya Dar es Salaam wamefika kusaidia shughuli za uokoaji, miongoni mwao akiwamo Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadick.

Baadhi ya mashuhuda wamedai kuwa mabaki ya jengo hilo yanaonyesha kuwa mchanga ulikuwa mwingi mno kulinganisha na saruji, hali inayodhaniwa kuwa ni miongoni mwa sababu za kuporomoka kwa mjengo huo uliogharimu mamilioni ya pesa.

Hadi kufikia sasa, hakuna taarifa rasmi za serikali zilizotolewa kuelezea msiba huo
Endelea Kusoma >>
0 comments

BREAKING NEWS; JENGO LA GHOROFA 16 LAANGUKA KATIKATI YA JIJI

 Mtoto Maisamali Karim (6) ambaye ameokolewa kutoka katika madrasa ya Msikiti wa Khoja Shia Ithna Asheri Jamaat iliyoangukiwa na jengo hilo katika mtaa wa Indira Gandhi. (Picha zote na Habari Mseto Blog)
 Changamoto ya uokoaji ni ngumu, lakini vikosi mbalimbali vinaendelea na zoezi hilo, ili kunusuru maisha ya waliofukiwa na kifusi.
 Hizi nia aina ya nondo ambazo kimsingi sio imara kuweza kuhimili ujenzi wa ghorofa ndefu kama hili, kuna haja mamlaka husika likatupia macho kampuni za ujenzi ili kuokoa maisha ya wajenzi na watumiaji wa majengo hayo.
 Askari wakiimarisha ulinzi wakati zoezi la uokoaji likiendelea.
  Jitihada za kuwaokoa watu zikiendelea, huku nondo nyembamba zikionekana na kuacha maswali miongoni mwa mashuhuda wa tukio hilo.
  Jitihada za kuwaokoa watu zikiendelea.
 Jitihada za kuwaokoa watu zikiendelea.
Waokoaji.

 Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk. Emmanuel Nchimbi (kushoto) akipata maelezo kutoka kwa Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam (CP), Suleima Kova kuhusu jengo la ghorofa 16 lililoanguka majira ya saa mbili asubuhi katika makutano ya mtaa wa Indira Ghandi na Barabara ya Morogoro jijini Dar es Salaam. Kulia ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Marietha Minangi. Katika ajali hiyo watu wawili wamekufa papo hapo. (Picha zote na Habari Mseto Blog)
 Waokoaji wakiwa kazini.

 Kamanda wa Polisi Kanda Maalum (CP), Suleima Kova akiwa katika eneo la tukio. Kulia ni Mbunge wa viti maalum (NCCR-Mageuzi James Mbatia.
Endelea Kusoma >>
 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu