Wednesday, July 31, 2013

0 comments

SIMBA SC YASAJILI STRIKER LA MAREKANI JIONI HII


IMEWEKWA JULAI 31, 2013 SAA 12:03 JIONI
Mshambuliaji wa zamani wa Pamba FC ya Mwanza, Betram Mombeki (kulia) aliyekuwa Marekani kwa muda mrefu, akisaini Mkataba wa miaka miwili kuichezea SImba SC leo, baada ya kuvutia katika majaribio. Kulia ni Kaimu Makamu Mwenyekiti wa Simba SC, Joseph Itang'are 'Kinesi'.
Endelea Kusoma >>
0 comments

NEYMAR, MESSI WAANZA KAZI PAMOJA BARCA...PACHA JIPYA LA HATARI LA USHAMBULIAJI DUINA NZIMA

MCHEZAJI  mpya wa Barcelona, Neymar ameanza mazoezi na timu yake hiyo mpya baada ya kukamilisha vipimo vya afya.
Wachezaji wote wa Barcelona waliokuwa kwenye Kombe la Mabara walitipoti jana baada ya mapumziko na Neymar alikuwa miongoni mwao pamoja na Xavi, Andres Iniesta, Cesc Fabregas na Lionel Messi.
Ilikuwa mara ya kwanza kukutana na wachezaji wenzake wapya, baada ya kuweka rekodi ya kuwa mchezaji wa pili ghali katika historia ya klabu baada ya Zlatan Ibrahimovic mwaka 2009 kusajiliwa kwa Pauni Milioni 56.
 VIDEO  Mazoezi ya Barcelona na wachezaji kupimwa afya jana
Not bad: Lionel Messi (left) and Neymar (right) trained together for the first time
Si mbaya: Lionel Messi (kushoto) na Neymar (kulia) wakifanya mazoezi pamoja kwa mara ya kwanza
One of the lads: Neymar (left) was put through his paces with his new team-mates in Barcelona
Neymar (kushoto) akiwa na wachezaji wenzake wapya wa Barcelona
Cesc Fabregas
Neymar
Neymar na mchezaji anayetakiwa na Manchester United, Cesc Fabregas (kushoto) wote walikuwa kivutio mazoezini 
At home: Neymar with Brazilian team-mate Daniel Alves during Barcelona training
Nyumbani: Neymar na mchezaji mwenzake wa Brazil, Daniel Alves katika mazoezi ya Barcelona
Welcome: Goalkeeper Victor Valdes meeting new manager Gerardo Martino
Karibu: Kipa Victor Valdes akisalimiana na kocha mpya, Gerardo Martino
Endelea Kusoma >>

RAIS JAKAYA KIKWETE NA MGENI WAKEWaziri Mkuu wa Thailand, Yingluck Shinawatra leo, wameshuhudia utiaji sai

0 comments
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete na Waziri Mkuu wa Thailand, Yingluck Shinawatra leo, Jumanne, Julai 30, 2013 wameshuhudia utiaji saini mikataba minne ya kuimarisha ushirikiano na uhusiano kati ya nchi hizo mbili.

Viongozi hao wawili wameshuhudia utiaji saini huo katika shughuli fupi iliyofanyika Ikulu, Dar es Salaam mchana wa leo ikiwa sehemu ya shughuli za Mheshimiwa Shinawatra katika Tanzania wakati wa ziara yake ya siku tatu nchini.

Mikataba ambayo viongozi hao wameshuhudiwa ikitiwa saini ni pamoja na ule wa kubadilisha wafungwa uliotiwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mheshimiwa Silima Pereira kwa niaba ya Tanzania na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Thailand, Mheshimiwa Surapong Tovichachakul,.

Mikataba mingine ni mkataba wa Kuimarisha na Kulinda Uwekezaji (Promotion and Protection of Investments) na mkabata wa Ushirikiano katika Masuala ya Ufundi iliyotiwa saini na Mheshimiwa Tovichachakul na Waziri wa Fedha wa Tanzania, Mheshimiwa William Mgimwa.

Mkataba wa nne kutiwa saini ni Makubaliano kati ya Wizara ya Nishati na Madini na Chuo cha Madini cha Thailand kwa niaba ya Wizara ya Biashara ya Thailand uliotiwa saini na Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini Bwana Eliakim Maswi na Mkurugenzi Mkuu wa Chuo cha Madini cha Thailand Bi. Prom Sawatwatthanakul.


Mapema leo Waziri Mkuu wa Thailand ambaye aliwasli nchini akitokea Mozambique katika ziara yake ya nchi tatu za Afrika amepokelewa kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) na pia akalakiwa Ikulu, Dar Es Salaam na mwenyeji wake Rais Kikwete.

Viongozi hao wamekutana na kufanya mazungumzo ya faragha na baadaye kufanya mazungumzo rasmi ya Kiserikali kati ya Sserikali hizo mbili.
Kubwa ambalo limekubaliwa katika mazungumzo hayo ni umuhimu wa nchi hizi mbili kuimarisha uhusiano na ushirikiano kati yao kwa manufaa ya wananchi wa Tanzania na Thailand.

Baadaye viongozi hao wawili wamekwenda kwenye Hoteli ya Hyatt Regency-Kilimanjaro mjini Dar Es Salaam ambako Mheshimiwa Shinawatra ametangaza Mpango Mpya wa Ushirikiano kati ya Afrika na Thailand.

Mama huyo ameuambia mkutano huo wa maofisa wa Serikali, wafanyabiashara wa sekta binafsi, wasomi, mabalozi na wanadiplomasia pamoja na wawakilishi wa taasisi zisizokuwa za Kiserikali kuwa Mpango huo una misingi yake katika ushirikiano wa Nchi Zinazoendelea za Kusini (South-South Cooperation).

Chini ya Mpango huo, Thailand itaitisha mkutano wa kwanza wa wakuu wa nchi za Afrika na Thailand mwanzoni mwa mwaka ujao na amemwalika Rais Kikwete kuhudhuria mkutano huo wenye nia ya kujenga mahusiano ya karibu zaidi kati ya Afrika na Thailand.

“Kwa kutilia maanani usawa wa ujuzi wa jitihada za maendeleo nchi za Afrika na Thailand, nchi yangu itaongeza kasi ya mahusiano ya maendeleo na Afrika katika maeneo ambako uhusiano huo unaweza kuongeza faida kwa pande zote mbili, kwa jamii zetu na watu wetu hasa katika sekta za kilimo, afya, elimu na maendeleo ya watu kwa jumla.”


Ameongeza mama huyo: “Wakati huo huo, Thailand inatangaza leo kuanzishwa kwa Mpango wa Wanathailand Kujitolea ambako wataalam wa Thailand watafanya kazi na wenzao wa Afrika katika nchi za Afrika kwenye miradi iliyoko chini ya ushirikiano wa kiufundi.”

Baadaye leo, Waziri Mkuu Shinawatra atahudhuria dhifa ya kitaifa ambayo imeandaliwa kwa heshima yake na Rais Kikwete na itakayofanyika Ikulu, Dar Es Salaam.

Kesho, Waziri Mkuu huyo atakwenda kwenye Mbunga ya Taifa ya Serengeti ambako atakutana na maofisa wa Wizara ya Maliasili na Utalii watakaomwelezea hali halisi, changamoto na umuhimu wa kulinda mbunga za wanyama. Aidha, akiwa Serengeti, mama huyo atashuhudia utiaji saini wa Makubaliano ya Kushirikiana Katika Kulinda Hifadhi na Wanyamapori kati ya Serikali za Tanzania na Thailand, ikiwa ni pamoja na kushirikiana katika kupambana dhidi ya ujangili.

Mama huyo atarejea Dar Es Salaam keshokutwa kumalizia ziara yake na kuondoka kurejea nyumbani.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
30 Julai, 2013

Endelea Kusoma >>
0 comments

MAHAKAMA ya wilaya ya Mbeya imemhukumu kwenda jela miaka 30 mkazi wa Isanga Mkoani hapa baada ya kumtia hatiani kwa kosa la kumlawiti na kumzalisha binti yake wa kumzaa.

Yusufu Amani (39) aliyembaka mwanaye wa kumzaa kisha kumzalisha baada ya kutengana na mkewe Afungwa miaka 30
Hapa akijifunika sipigwe picha baada ya hukumu
Kulia ni mtoto aliyebakwa na baba yake kisha kuzalishwa akiwa na mtoto wake wakitoka mahakamani kulia ni mama mzazi wa binti aliyebakwa na kuzalishwa


MAHAKAMA ya wilaya ya Mbeya imemhukumu kwenda jela miaka 30 mkazi wa Isanga Mkoani hapa baada ya kumtia hatiani kwa kosa la kumlawiti na kumzalisha binti yake wa kumzaa akiwa na miaka 15( jina linahifadhiwa).



Mwendesha mashitaka wa serikali  Archiles Mulisa  aliiambia mahakamani hiyo Mbele ya Hakimu Gilbert Ndeuruo kuwa Mshtakiwa huyo ni Yusufu Amani (39) anayedaiwa kumbaka mwanaye wa kumzaa kisha kumzalisha baada ya kutengana na mkewe.



Alisema kosa hilo ni kinyume cha sheria kifungu cha 154 (1)a na 155 sura ya 16 iliyofanyiwa marekebisho  mwaka 2002, pamoja na kifungu cha 158(a) cha makosa ya kuzini.


akisoma Hukumu hiyo Hakimu Ndeuruo alidai kuwa Mtuhumiwa alianza kujihusisha kimapenzi na mwanaye Mwaka 2008 baada ya kutengana na mkewe ambapo Mtuhumiwa aliachiwa watoto wote.
Aliongeza kuwa wakati huo binti huyo alikuwa na umri wa miaka 12 na alikuwa akisoma shule ya msingi darasa la Tano jambo ambalo wamedumu nalo kwa Miaka mine hadi ilipogundulika kuwa binti alikuwa mjamzito Mei, 2012.
Alisema mbinu aliyokuwa akiitumia ni kumtishia binti asitoe taarifa kwa mtu yoyote na kwamba baada ya kugundulika kuwa na ujauzito alimwambia amsingizie kijana yoyote mtaani kwao.
Hakimu Ndeuruo alisema Mahakama ilimtia hatiani Mtuhumiwa kutokana na ushahidi wa Mhanga wa tukio hilo ambaye ni binti pamoja na ushahidi wa kitaalamu kutoka kwa Mkemia mkuu wa Serikali.
Alisema ushahidi wa Mkemia Mkuu wa Serikali baada ya kupima Vinasaba kutoka Mtuhumiwa, Mhanga na Mtoto aliyezaliwa ulidai kuwa  Mshtakiwa ndiye baba halali wa Mtoto kutokana na Maeneo 15 ya vipimo vya Vinasaba kati ya Baba na Mtoto aliyezaliwa kufungana kwa asilimia 99.9.
Aidha kabla ya kutoa hukumu Hakimu alimpa nafasi mtuhumiwa kujitetea ili apunguziwe adhabu au asiweze kuhukumiwa kabisa lakini hali ikawa tofauti baada ya Mtuhumiwa kujibu kuwa hana la kujitetea vyovyote itakavyokuwa anachotaka ni nakala ya hukumu.
Kutokana na kushindwa kujitetea Hakimu Ndeuruo alimhukumu kwenda jela miaka 30 na kwamba ana haki ya kukata rufaa katika Mahakama kuu endapo hakuridhika na hukumu hiyo.
Awali katika ushahidi wake Mahakamani hapo Mtuhumiwa huyo alidai kuwa hakutenda kosa hilo bali alitengenezewa na Mkewe ambaye aliapa kumkomesha baada ya kukosana na kumpata mume mwingine jambo ambalo lilipingwa vikali na hakimu na kudai kuwa “ mfa maji haachi kutapatapa”

Na Mbeya yetu
Endelea Kusoma >>

WAZIRI MKUU WA THAILAND YINGLUCK SHINAWATRA ATUA BONGO

0 comments




Mpiga Picha wa New Habari House, wachapishaji wa magazeti ya Mtanzania na The Africa, Anthony Siame, akisukumwa na afisa usalama, wakati akiwa kwenye kazi ya ujio wa waziri mkuu wa Thailand, Yingluck Shinawatra kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam leo

Endelea Kusoma >>

Sunday, July 28, 2013

COAST UNION YAITUNGUA SIMBA BAO 1-0 BILA MAJIBU LEO MKWAKWANI TANGA

0 comments
KIKOSI CHA COAST UNION
TIMU ya soka ya Coastal Union ya Tanga imeendelea kuvitisha vigogo vya soka nchini ikiwa ni mwezi mmoja kabla ya kuanza kwa Ligi Kuu Tanzania Bara msimu  wa 2013-2014 baada ya jioni hii kuizima mdomo Simba na kushinwdwa kunguruma  baada ya kunyukwa  bao 1-0 katika mechi ya kirafiki.
Pambano la leo lililochezwa kwenye uwanja wa Mkwakwani Tanga ilishuhudiwa hadi wakati wa mapumziko kukiwa hakuna mbabe yeyote baada ya timu zote kutoshana nguvu ya kutofungana.,
Hata hivyo katika kipindi cha pili Coastal walionyesha ilivyopania msimu ujao kwa kuwakimbiza Simba na kujipatia bao pekee lililowekwa kimiani na mchezaji wao mpya toka Kenya,  Crispian Odula Odwenye aliyefunga katika dakika 54.
Hicho ni kipigo kingine kwa Simba katika mechi zake za karibu za kirafiki za kujipima nguvu na inamfanya kocha wake, King Abdallah Kibadeni kurekebisha mapema kikosi chake kabla ya ligi.
 

Endelea Kusoma >>

BOMOABOMOA IMEWAKUMBA WAKAZI WA BOKO LEO

0 comments
Bomoabomoa imewakumba wakazi wa boko basihaya uboaji wa nyumba zai ya mia moa 100 umeanza toka leo kwa mujibu wa diwani wa kata ya Bunju  anaejulikana kwa jina la Majisafi amesema zoezi la ubomoaji wa nyumba hizo ni kutokana na mpango wa dawasa wa kupitisha bomba kubwa la maji kwa wakazi wa jijini Dasr es salaam amedai kuwa nyumba hizo ambazo baadhi yao wamejenga katka barabara ya bombo na wengine ni pale sehemu ya nyumba zao zimezidi kidogo wananchi hao ambo leo walikuwa na kikao cha wananchi kwa madai ya kutopewa taarifa mapema na uwekaji wa alama za ukutani zimewekwa alama za x na nyingine kuielekeza bomoa

kijiko kikiwa kazini leo kusafisha barabara






zahanati ya boko nayo yavunjwa

vijana nao wajipatia kuni mara baada ya kungolewa kwa miti


mkutano wa wananchi wa boko leo

mkutano wa wakazi leo

wakazi wakichangia kwenye mkutanoleo


BIBI Hamida kilemba mkazi wa boko akionyesha alama aliyowekewa na dasawa kluashiria kubomo sehemu hiyo

moja ya jengo la ghorofa la bwana Allan Lema linatakiwa kubomolewa kupisha ujenzi wa bomba kuu  lwa dawasa

Endelea Kusoma >>
 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu