Monday, June 30, 2014

0 comments

Endelea Kusoma >>
0 comments
LEO NI SIKU YA TATU TOKA KUFUNGULIWA KWA MAONYESHO YA 38 YA SABASABA YALIYOANZA JUMAMOSI HUKU WATU MBALIMBALI WAKIWA KATIKA  FOLENI YA KUINGIA KATIKA UWANJA HUO NA KUJIONEA MAMBO MBALIMBALIYALIYOPO KWENYE VIWANJA YALIYOPO KATIKA BARABARA YA KILWA LEO

Endelea Kusoma >>
0 comments
​​
WAZIRI MKUU: MAANDALIZI YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA YANAENDELEA

WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amesema maandalizi ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa ambao unatarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu yanaendelea japo kwa kiasi kikubwa hatma yake inategemea kukamilika kwa mchakato wa Katiba mpya.

Ametoa kauli hiyo leo mchana (Jumatatu, Juni 30, 2014) wakati akizungumza na Mameya wa Majiji, Manispaa na Wenyeviti wa Halmashauri za Miji na Wilaya Tanzania katika kikao cha siku moja kilichofanyika kwenye ukumbi wa Regal Naivera jijini Tanga.

Waziri Mkuu yuko Tanga kwa ajili ya sherehe za Serikali za Mitaa ambayo kilele chake kitafanyika kesho Julai mosi kwenye uwanja wa Tangamano jijini hapa. Ameamua kukutana na viongozi hao ikiwa ni utekelezaji wa ahadi ya kukutana nao aliyoitoa Mei 14, 2014 wakati akifungua Mkutano Mkuu wa ALAT.

"Uchaguzi wa Serikali za Mitaa bado ni kitendawili kwa sababu kwa kiasi kikubwa inategemea sana kukamilika kwa Mchakato wa Bunge la Katiba," alisema na kuongeza:

"Kama Wizara tunaendelea na maandalizi tukiamini uchaguzi upo, kama hiyo fursa isipotokea bado tutakuwa tumekamilisha maandalizi kwa upande wetu.Tunaendelea kuandaa kanuni kwa kushirikisha wadau wote," alisema.

Waziri Mkuu alitumia fursa hiyo kusisitiza suala la ukusanyaji mapato na udhibiti wa matumizi ya fedha za Serikali. Kuhusu mapato, Waziri Mkuu alisema katika mwaka wa fedha wa unaoisha sasa, hali ya ukusanyaji mapato haikuwa nzuri.

Kufuatia hali hiyo, Waziri Mkuu alisema amewaandikia barua Wakuu wa Mikoa akiwataka waweke utaratibu wa kutoa taarifa kila baada ya miezi mitatu juu ya makusanyo ya kila Halmashauri zilizo kwenye mikoa yao.

"Katika taarifa hizi itabidi kila Halmashauri ieleze ilipanga kukusanya kiasi gani, je imefikia lengo na kama sivyo ni kwa nini. Nia yetu ni kutrack down makusanyo na kuona yamekwama wapi na yamekwamishwa na nini," alisema.

Kuhusu udhibiti wa matumizi, Waziri Mkuu aliwataka Mameya na Wenyeviti hao kuendelea kuwabana wahusika ili kudhibiti matumizi yasiyofaa. "Lazima muendelee kuwabana na kuwasimamia wakurugenzi na wataalaam wa kwenye Halmashauri zenu. Fanyeni kazi kwa ufanisi, msiwachekee wale wanaoharibu," aliongeza.

"Ili muweze kuwabana vizuri, ni lazima mdai kupatiwa taarifa za fedha kutoka kwa Mkaguzi wa Ndani (Internal Auditor)... kuna baadhi ya watendaji wanadai kuwa hizi taarifa ni siri wakati siyo siri," alisema.

Aliwaeleza washiriki wa kikao hicho kwamba taarifa hizo ni muhimu kwao kuzipata na zitawasaidia kuonyesha mapungufu yoyote kama yapo.

Aliwataka kila mmoja wao kwa nafasi zao za Meya na Mwenyekiti wahakikishe wanalenga kupandisha pato la wananchi wanaowaongoza.

(mwisho)

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMATATU, JUNI 30, 2014











Endelea Kusoma >>

HAPPY BIRTHDAY MWANDISHI MKUU WA MBEYA YETU BLOG

0 comments
Mwandishi mkuu wa Mbeya yetu Blog, Joseph Mwaisango
******

TONE MULTIMEDIA GROUP Ambao ni wamiliki wa Mtandao huu wa Mbeya yetu Blog , Tunapenda Kuungana na wadau wetu wote Kumpongeza Bwana Joseph Mwaisango ambaye ndiye Mwandishi Mkuu wa Blog hii ya Mbeya yetu  na Mmoja wa wakurugenzi wa Tone Multimedia Company Limited (TMCL)  ambao pia ni wamiliki wa Blogs za Mikoa TanzaniaTone Radio-Tz , This Day MagazineStay In Tanzania(Tanzania Tours) , Tone Tube Tz  , Matukio na Wanavyuo na Watanzania waishio nje ya Nchi kwa kutimiza miaka yake kadhaa siku ya Leo.

Tunapenda kumpa Hongera sana kwa kazi nzito ambazo anazifanya ili kuwaletea wadau habari zilizo sahihi na za uhakika zaidi kutoka pande zote za Mkoa wa Mbeya, Pia tunamuombea kwa Mungu ampe siku nyingi zaidi , Afya Njema na aendelee kuchapa kazi zaidi na zaidi bila kusahau kuongeza Ubunifu zaidi.

Pia katika Hili tunapenda kuwashukuru wadau Mbali mbali wa Habari wakiwemo Bloggers wote wa Tanzania, Magazeti, Radio na TV kwa kuendelea kuonesha ushirikiano mkubwa ili kazi ziendelee kwa ufanisi mkubwa

Mwisho tunapenda kumshukuru kila mmoja wetu ambaye ni mdau mkubwa wa Blog ya Mbeya yetu,  wote tupo pamoja katika kusherekea siku hii ya leo.

Asanteni
Endelea Kusoma >>
0 comments


Na: Hassan Hamad, OMKR
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad ameonya kuwa vitendo vya hujuma dhidi ya raia na wageni, vinaweza kuathiri kwa kiasi kikubwa uchumi wa Zanzibar.
Amesema Zanzibar ambayo imekuwa ikitegemea zaidi sekta ya Utalii kuendeleza uchumi wake na kukuza pato la taifa, imekuwa ikiguswa na matukio hayo ya hujuma, na kwamba yanaathiri uchumi, ustawi wa jamii na sifa ya ukarimu kwa Zanzibar.
Mhe. Maalim Seif ametoa kauli hiyo katika mahojiano maalum na kituo cha televisheni cha ITV, Mikocheni Dar es Salaam.
Amesema katika kukabiliana na vitendo hivyo, serikali inakusudia kutekeleza mpango wake wa kuweka kamera za CCTV katika maeneo muhimu ya utalii likiwemo eneo la Mji Mkongwe, ili kuweza kuwabaini kwa urahisi wahusika wanafanya vitendo hivyo.
Kuhusu zao la karafuu kwa maendeleo ya uchumi wa Zanzibar, Maalim Seif amesema serikali imefanikiwa kudhibiti magendo ya karafuu baada ya kuongeza bei ya zao hilo na kuwashinda wanunuzi wengine wa Afrika Mashariki ambako karafuu hizo zilikua zikipelekwa.
Aidha amesema katika kuhakikisha kuwa ubora wa karafuu za Zanzibar unalindwa na kudhibiti wauzaji wengine, Serikali kupitia Wizara ya Biashara, Viwanda na Masoko, itaweka nembo maalum “brand”, kuweza kuzitofautisha karafuu za Zanzibar na maeneo mengine.
Akizungumzia dawa za kulevya, Maalim Seif ambaye ofisi yake ndiyo inayohusika na udhibiti wa dawa hizo, amesema bado kuna kazi kubwa ya kudhibiti uingizaji na matumizi ya dawa hizo kutokana na jiografia ya visiwa vya Zanzibar.
Amefahamisha kuwa vita hiyo pia ni ngumu kutokana na uwezo mkubwa wa wafanyabiashara wa dawa hizo ambao wanaweza kuwarubuni watendaji kwa pesa nyingi na kuacha kutekeleza wajibu wao.
Amesema katika kupiga vita dawa hizo, ni lazima kuwepo na mashirikiano pamoja na uadilifu miongoni mwa watendaji, hasa wale wanaofanya kazi katika viwanja vya ndege, bandarini na vyombo vya ulinzi.
Maalim Seif ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi CUF, amesema Serikali ya Umoja wa Kitaifa GNU itaendelea kuwepo hata baada ya uchuguzi mkuu wa mwaka 2015, kwa vile suala hilo ni la kikatiba na limewekewa misingi maalum.
Kuhusu mchakato wa katiba mpya, Maalim Seif amesema bado serikali ina jukumu la kuhakikisha kuwa katiba mpya inapatikana, ili kuendeza ustawi wa Taifa na kukidhi mahitaji ya wananchi.
Amesema tayari serikali imeshatumia fedha nyingi za wananchi, na kwamba kushindwa kukamilisha mchakato huo kwa wakati, itakuwa ni hasara kwa serikali na taifa kwa ujumla.
Hivyo amesema hakuna budi kwa serikali kutafuta njia mbadala za mazungumzo, kuhakikisha kuwa mchakato huo unaendelea na unafanikiwa kwa maslahi ya Taifa.
HABARI HII HAINA PICHA. AHSANTENI WADAU.
  
 

Endelea Kusoma >>

Sunday, June 29, 2014

0 comments

BRAZIL `WACHIZIKA` NA USHINDI WA PENATI DHIDI YA CHILE, SASA NGOMA ROBO FAINALI!

 
wakishangilia ushindi wao wa penati 3-2 dhidi ya Chile na kufanikiwa kufuzu hatua ya robo fainali.   WENYEJI Brazil wamekuwa wa kwanza kufuzu hatua ya robo fainali ya kombe la dunia baada ya jana usiku kuifunga Chile kwa mikwaju 3-2 ya penati kufuatia sare ya bao 1-1 katika dakika 90 za kawaida na dakika 30 za nyongeza. Kutokana na matokeo hayo, baadhi ya wachambuzi wa soka wameanza kuwa na wasiwasi na mwendo wa Brazil na kushindwa kutambua watafika hatua gani. Lakini sapoti kubwa wanayopata kutoka kwa mashabiki wao inaweza kuwa motisha kubwa kwao na wakajikaza hatua inayofuata. Jibu...
Endelea Kusoma >>
0 comments
To see with pictures click > View Online
Buy now and save!  Get warehouse shelves from Tshs 70,000, store shelves from Tshs 60,000, checkout counters, merchandise, signage and trucks at huge discounts.
For more information on prices, contact us today at  +255 682 613 537 | dollarama.tz.morogoro@gmail.com.
Huge Discounts at the Dollarama Warehouse Liquidation Sale
"Zoom it"

www.ZoomTanzania.com/ Supermarkets-And-Grocery- Stores

ZoomTanzania Mail Shots

105,000+ Premier Subscribers Across Tanzania

ZoomTanzania.com is the most visited English language website in Tanzania.

Contact Us:
+255 786 264 687
Endelea Kusoma >>

KANISA LA YESU KRISTO LA WATAKATIFU WA SIKU YA MWISH

0 comments


Kiongozi wa shule ya jumapili wa Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa siku za mwisho,Dr, Emanuel Kandusi akiwapatia maelezo mbalimbali kwa watu waliotembelea kanisa hilo wakati wa siku ya wazi kwa ajili ya watu mbalimbali kuangalia shughuli zinazofanywa na kanisa hilo
Baadhi ya watu waliotembelea kanisa hili wakipata maelekezo mbalimbali
Mwakilishi wa Darasa la Mkono msaidizi wa akina mama Happy Ayubu akitoa maelezo kwa watu waliotembelea kanisa hilo
Baadhi ya watu waliotembelea kanisa hili wakipata maelekezo mbalimbali
Mhumini waKanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa siku za mwisho Framers Ngosha akijibu maswali ya watu waliojitokeza katika siku hiyo


Kiongozi wa shule ya jumapili wa Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa siku za mwisho,Dr, Emanuel Kandusi 'kulia' akionesha vitabu vinavyotumika kwa ajili ya mafunzo kushoto ni Rais wa tawi la Mbezi Beach, Malabi Kyubi
Rais wa tawi la Mbezi Beach, Malabi Kyubi akitoa maelezo
Baadhi ya watu mbalimbali waliotembelea katika kanisa hilo lililopo Mbezi Beach
Baadhi ya watoto wa waumini wa Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za mwisho wakicheza na kuimba wakati wa siku ya wazi kwa watu kutembelea na kuona mambo mbalimbali iliyofanyika katika kanisa lao la Mbezi Beach jijini Dar es salaam

Baadhi ya watoto wa waumini wa Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za mwisho wakicheza na kuimba wakati wa siku ya wazi kwa watu kutembelea na kuona mambo mbalimbali iliyofanyika katika kanisa lao la Mbezi Beach jijini Dar es salaam
watu waliotembelea wakipata mahelezo mbalimbali
Baadhi ya watu waliotembelea katisa hilo
Endelea Kusoma >>

Saturday, June 28, 2014

MATUKIO YA LEO

0 comments
mbunge wa jimbo la kawe kupitia chadema Halima Mdee akichangia sheria ya sheria ya mswada wa fedha leo mjini dodoma katika kikao cha bunge ambacho kimaharishwa kikao hicho cha bunge


Katibu mtendaji tume ya Taasisi ya vyuo vikuu vya Afrika Mashariki Profesa Mayunga Nkunya  akiongea na wandishi wa habari kuhusu uhakiki wa ubora wa mifumo ya Elimu ya pamoja katika vyuo vikuu vya  Afrika ya Mashariki  kulia ni   naibu katibu mtendaji Profesa Pantien Ndabaneze leo

Afisa mawasiliano wa kiwanda cha mmsteel Abubakari Mlawa wa pili kulia akiwaeleza baadhi ya wakazi wa jiji la dar es salaam moja ya nyumba ya mfano iliyojengwa kwa kutumia mabati ya kisasa kabisa yanayozalishwa na kampuni hiyo kwenye maonyesho ya sabasaba ambayo yameanza leo

bado maandalizi ya ya sabasaba picha inaonyesha baadhi ya watu wakiawa na mkokoteni wakipeleka bidhaa kwenye mabanda leo

baadhi ya wakazi waliofika kwenye maonyesho ya sabasaba yaliyoanza leo kuwahi kununua bidhaa




Baadhi wa wajumbe waliochaguliwa kuingia Baraza Kuu la Uongozi (CUF) Taifa baada ya kutangazwa rasmi.

Na: Hassan Hamad (OMKR)
Hatimaye Chama Cha Wananchi CUF kimekamilisha mchakato wa kuchagua safu ya uongozi wa kitaifa kwa kuwachagua wajumbe 45 wa Baraza Kuu la Uongozi Taifa, 20 kati yako wakitokea Zanzibar.
Wajumbe hao ni miongoni mwa wajumbe 143 waliogombea Baraza Kuu la Uongozi (CUF) kupitia kanda saba za Tanzania Bara na mbili za Zanzibar ambazo ni Kanda ya Unguja na Kanda ya Pemba.
Kuchaguliwa kwa wajumbe hao kumekamilisha safu ya uongozi wa kitaifa wa Chama hicho ambapo tarehe 25/06/2014 wajumbe wa mkutano mkuu wa CUF Taifa uliofanyika Ubungo Plaza Dar es Salaam, walimchagua tena Prof. Ibrahim Lipumba kuwa Mwenyekiti wa Chama hicho ambapo Maalim Seif Sharif Hamad alichaguliwa tena kuwa Katibu Mkuu wa Chama hicho.
Wajumbe hao pia walimchagua Mhe. Juma Duni Haji kuwa Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho ambaye amechukua nafasi ya Mzee Machano Khamis Ali ambaye hakuomba kugombea tena nafasi hiyo kutokana na sababu mbali mbali ikiwemo ya kiafya.
Akizungumza baada ya uchaguzi huo, Mwenyekiti wa CUF Taifa Prof. Ibrahim Lipumba, aliwashukuru wajumbe wa mkutano mkuu kwa kuonesha nidhamu ya hali ya juu na kufanikisha uchaguzi huo kwa amani na usalama.
Amesema hatua hiyo imedhihirisha ukomavu wa demorasia na uvumilivu ndani ya chama hicho, na kuwataka wajumbe waliochaguliwa kuendeleza kazi ya kukiimarisha na kukijenga chama hicho, ili kiweze kushinda katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.
Akitoa neno la shukrani kwa niaba ya wajumbe wasiochaguliwa kwa upande wa Zanzibar, Mjumbe wa Mkutano huo Bi. Asha Ali Faki amesema wajumbe waliochaguliwa kuingia Baraza Kuu wana kazi kubwa ya kuwaunganisha wanachama, ili kuendeleza umoja na mshikamano uliopo ndani ya chama.
Aidha amewanasihi wajumbe ambao kura zao hazikutosha kuingia katika Baraza hilo kutokata tama, na badala yake waunganishe nguvu zao kuweza kukabiliana na uchaguzi mkuu ujao.
Akiwakilisha wajumbe waliochaguliwa kuingia katika Baraza Kuu la Uongozi CUF upande wa Zanzibar, Mjumbe wa Mkutano huo Bw. Salim Bimani amewashukuru wajumbe wa  mkutano huo kwa kuwachagua, na kuahidi kushirikiana na wanachama pamoja na viongozi wa ngazi zote katika kukiendeleza chama hicho.
Nae mjumbe wa mkutano huo akiwakilisha wasiochaguliwa kuingia Baraza Kuu kwa upande wa Bara Bw. Suleiman Bungala (Bwege), amesema wajumbe wa mkutano huo wamefanya maamuzi sahihi ya kuwachagua viongozi hao kulingana na maeneo wanayotoka.
Amesema viongozi waliochaguliwa wameonesha umahiri mkubwa katika utendaji wao, na kwamba kazi kubwa inayowakabili hivi sasa ni kushirikiana na viongozi wengine pamoja na wanachama kuandaa timu ya ushindi kwa ajili ya uchaguzi wa serikali za mitaa pamoja na uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.
“Viongozi tuliowachagua sasa tushirikiane kwa pamoja kuishinda CCM 2015”, alisema kwa madaha na majigambo.
WALIOCHAGULIWA UNGUJA.
Wajumbe kumi (10) waliochaguliwa kuwakilisha Baraza Kuu CUF kanda ya Unguja ni Salim Bimani, Nassor Ahmed Mazrui, Fatma Abdulhabib Ferej, Zahra Ali Hamad na Shaaban Iddi Ahmed.
Wengine ni Pavu Juma Abdallah, Abdillahi Jihadi Hassan, Hassan Jani Massoud, Mohd Kombo Ali na Hemed Said Nassor.
WALIOCHAGULIWA PEMBA.
Kanda ya Pemba wajumbe 10 waliochaguliwa ni Hamad Massoud Hamad, Abubakar Khamis Bakar, Rukia Kassim, Said Ali Mbarouk na Khalifa Mohd Issa.
Wengine ni Omar Ali Shehe, Riziki Omar Juma, Massoud Abdallah Salim, Hijja Hassan Hijja na Najma Khalfan Juma.
WALIOCHAGULIWA BARA.
Miongoni mwa wajumbe 25 waliochaguliwa kuingia Baraza Kuu la Uongozi (CUF) Taifa kwa upande wa Bara ni pamoja na Chifu Letalosa Yemba (aliyegombea Uenyekiti Taifa), Lobora Petro, Fatma Omar Kalembo, Magdalena Sakaya, Thomas Malima na Kapasha wa Kapasha.
Wengine ni pamoja na Bonifasia Mapunda, Abdul Juma Kambaya, Ashura Mustapha, Karume Jeremia, Julius Nyanja Salim Sarwan na Katani Ahmed Katani.
WALIOACHWA.
Aidha wajumbe wa mkutano huo hawakuwapa ridhaa na kuwaacha baadhi ya wajumbe wa Baraza lililopita wakiwemo Khalifa Suleiman Khalifa, Mohd Habibu Mnyaa, Zakia Omar Juma, Joram Bashange na Khamis Hassan.
Mapema akitoa  maazimio ya mkutano huo, Mwenyekiti wa kamati ya maazimio Hassan Jani Massoud, alisema makubaliano ya marekebisho ya katiba yaliyofanywa kwenye mkutano huo yaingizwe kwenye katiba ya chama hicho ili yaweze kutumika kuanzia tarehe 22/08/2014.
Kupitia maazimio hayo kamati hiyo pia imelitaka Baraza Kuu la Uongozi kusimamia haki ya watu wa kanda ya Kusini kuweza kufanya shughuli zao za kisiasa ikiwa ni pamoja na mikutano ya hadhara ambayo ilizuiwa na serikali.
Endelea Kusoma >>

COUTINHO AWASILI

0 comments

Afisa Haari wa Young Africans Bw Baraka Kizuguto (kushoto) akiwa pamoja na mshambuliaji mpya Andrey Coutinho mara baada ya kuwasili uwanja wa ndege wa JK Nyerer leo
Kiungo mshambuliaji mpya wa timu ya Young Africans SC  Andrey Marcel Ferreira Coutinho amewasili mchana wa leo jijini Dar es salaam akitokea kwao nchini Brazil tayari kabisa kwa kuanza kazi ya kuwatumikia wana Wanajangwani katika msimu wa 2014/2015.
Countinho amewasili mchana kwa shirika la Ndege la Afrika Kusini (South African Airways) akitoka jijini Sao Paul ambapo safari ya kuja Tanzania imemkchukua takribani masaa 20 tokea katika Mji wa Berem ambapo ndipo anapoishi>
Mara baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege  wa JK Nyerere, Coutinho alipokelewa na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji Bw. Mohamed Bhinda ambaye alimuongoza kuwasilimia washabiki na waaandishi wa habari walijitokeza kumlaki.
Akiongea na waandishi wa habari Uwanja wa Ndege Coutinho amesema anajisikia furaha kuwa Tanzania, nchi ambayo watu wake wanapenda mpira na kikubwa amekuja kuisaidia Yanga kufanya vizuri kwenye michuano mbalimbali mbali itayakayowakabili.
Kuhusu changamoto za ugeni katika Bara la Afrika, Coutinho alisema soka kwake ni kazi, ana uzoefu baada ya kucheza pia Barani Asia hivyo hana wasiwasi, na kwa kuwa na walimu aliwazoea anaamini kwa pamoja atafanya vizuri.
Msafara wa kutoka Uwanja wa ndege ulielekea makao makuu ya klabu mitaa ya Twiga/Jangwani ambapo Coutinho aliwasilimia wapenzi, washabiki na wanachama waliojitokeza kumpokea, kisha aliongea na katibu mkuu Bw Beno Njovu kabla ya kwenda kupumzika.
Endelea Kusoma >>

Friday, June 27, 2014

BREEKING NEWZZZZZZ JAMBAZI LAKAMATWA KISIWANI PEMBA ALIUA POLISI NA MGAMBO MKURANGA

0 comments
JESHI LA POLISI KISIWANI PEMBA LIMEFANIKIWA NA LIMEMKAMATA JAMBAZI MOJA ANAYETUHUMIWA KUVAMIA KITUO CHA POLISI WILAYANI MKURANGA MKOANI PWANI NA  WENZAKE NA KUMUUA ASKARI POLISI NA MGAMBO MMOJA NA HATMAYE KUPORA SILAHA NA KUTOKOMEA NAZO JESHI HILO LA POLISI KISIWANI LIMEFANYA KAZI YA ZIADA NA KUMNASA JAMBAZI HILO  HUKU JESI LA POLISI WAKIJITAHIDI KUWASA WENGINE  RADIO 1 STEREO
Endelea Kusoma >>
0 comments
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akutana na kufanya mazungumzo na Rais mpya wa Misri Mhe Abdel Fattah Al-Sisi mjini Malabo, Equatorial Guinea, pembeni ya Mkutano wa kawaida wa Umoja wa Afrika Juni 26, 2014

Endelea Kusoma >>
0 comments

MTEMVU AKAGUA MADHARA YA  MOTO ULIPOTEKETEZA SOKO LA KEKO USIKU WA KUAMKIA LEO

 Mbunge wa Temeke, Abbas Mtemvu akiingia eneo lililopata madhara kutokana na kuungua moto usiku wa kuamkia leo, katika soko la Keko, katika jimbo hilo jijini Dar es Salaam. Mtemvu amewapa pole walipoteza mali zao kutokana na moto huo ambao chanzo cha ke hakijajulikana.  Hadi inakisiwa imepatikana hasara ya zaidi ya sh. milioni 97.
 Naibu Katibu wa soko la Keko, Hassan Gitigi (kushoto) akimpa maelezo Mbunge wa Temeke Abbas Mtemvu kuhusu madhara yaliyosababishwa na moto huo
 Baadhi ya wafanyabiashara katrika soko hilo akieleza hasara walizopata. Wameeleza kwamba mbali na waliopata hasara ya kuunguliwa bidhaa na mabanda yaop ya biashara, pia wapo waliopata hasara kwa maduka na mabanda yaop ya biashara kuporwa na vibaka wakati wa tukio hilo la moto.
 Mtemvu akizungumza na waliopatwa na madhara kuhtokana na moto huo
Mtemvu akizungumza na baadhi ya viongozi waliofika kutoa pole kwa walipatwa na madhara kwenye soko hilo. Picha zote na Bashir Nkoromo- theNkoromo Blog
Endelea Kusoma >>

Thursday, June 26, 2014

KOCHA MPYA WA YANGA MAXIMO ATUA DAR LEO MUDA WA SAANA NANE MCHANA

0 comments
AKISALIMIANA NA WANACHAMA NA WAPENZI WA KLABU HIYO 

AKISALIMIANA NA WANACHAMA NA WAPENZI WA KLABU HIYO 

AKISALIMIANA NA WANACHAMA NA WAPENZI WA KLABU HIYO

AKIPOKEWA KATIKA KLABU YA YANGA

AKIONGEA NA WANDISHI WA HABARI MARA BAADA YA KUWASILI KATIKA UWANJA WA MWALIM NYERERE LEO

MAXIMO AKITEREMKA KATIKA KLABU YA YANGA
MAXIMO AKITEREMKA KATIKA KLABU YA YANGA

MAXIMO AKIONGEA NA WANDISHI WA HABARI MARA BAADA YA KUFIKA LEO KATIKA UWANJA WA NDEGE WA MWALIM NYERERE LEO

MAXIMO AKIONGEA NA WANDISHI WA HABARI MARA BAADA YA KUFIKA LEO KATIKA UWANJA WA NDEGE WA MWALIM NYERERE LEO

MAXIMO AKISALIMIANA NA WAANDISHI WA HABARI MARA BAADA YA KUWASILI

KOCHA MAXIMO AKITOKA NJE KATIKA UWANJA WA NDEGE LEO MCHAANA BAADA YA KUWASILI
WAPENZI MASHABIKI WA YANGA WALIOFIKA KWENYE UWANJA WA NDEGE WA MALIMU NYERERE KUMPOKEA KOCHA WAO MAXIMO LEO ALIPOFIKA MUDA SAANA NANE MCHANA

MASHABIKI WA SIMBA WAKISHOBOKEA HUKU WAKITOA MANENO YA DHARAU  WAKIWA NJE YA KLABU YAO WAKATI MSAFARA WA KOCHA MAXIMO UKIPITA KATIKA BARABARA YA MSIMBAZI WAKIELEKEA KATIKA KLABU YA YANGA JANGWANI LEO

KOCHA WA YANGA MAXIMO AKIWASALIMIA WAPENZI NA MASHABIKI WA YANGA MARA BAADA YA KUTEREMKA KWENY KLABU HIYO LEO AKITOKEA BRAZILI

MAXIMO AKIWASILI KATIKA KLABU YA YANGA JANGWANI AKIWA KATIKA GARILEO

WAANDISHI WA HABARI NA MASHABIKI WA YANGA WAKIMUHOJI KOCHA MAXIMO MARA BAADA YA KUWASILI LEO KATIKA UWANJA WA NDEGE

MASHABIKI WA YANGA WAKIWA  WAMEJIPANGA KATIKA UWANJA WA NDEGE WANAMSUBIRI KOCHA MPYA MAXIMO AKITOKA WAMPE MKONO LEO

Endelea Kusoma >>
 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu