Tuesday, September 30, 2014

RAIS JAKAYA KIKWETE AWASILI KUTOKA KATIKA ZIARA NCHINI MAREKANI

0 comments
jk1:Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Saidi Meck Sadik  baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Septemba 30, 2014 akitokea Marekani alikohudhuria Mkutano wa 69 wa Umoja wa Mataifa.
 

jk3: Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na IGP Ernest Mangu, Mnadhimu Mkuu  wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi  Tanzania (JWTZ), Luteni Jenerali Samuel Ndomba na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Saidi Meck Sadik  baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Septemba 30, 2014 akitokea Marekani alikohudhuria Mkutano wa 69 wa Umoja wa Mataifa.




 

jk2:  Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Mnadhimu Mkuu  wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi  Tanzania (JWTZ), Luteni Jenerali Samuel Ndomba mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Septemba 30, 2014 akitokea Marekani alikohudhuria Mkutano wa 69 wa Umoja wa Mataifa.

 

jkk1:Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama   baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Septemba 30, 2014 akitokea Marekani alikohudhuria Mkutano wa 69 wa Umoja wa Mataifa.

PICHA NA IKULU
 

Endelea Kusoma >>
0 comments

26 WAITWA TAIFA STARS KUIVAA BENIN

Wachezaji 26 wameitwa kwenye kikosi cha timu ya Taifa (Taifa Stars) kwa ajili mechi ya Kalenda ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) dhidi ya Benin itakayochezwa Oktoba 12 mwaka huu jijini Dar es Salaam. 
Kocha Mart Nooij ambaye yuko Cairo, Misri kwenye kongamano la makocha la Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF), amesema kikosi cha Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager kitaingia kambini Oktoba 6 mwaka huu jijini Dar es Salaam. 
Wachezaji walioitwa ni makipa Deogratias Munishi (Yanga), Aishi Manula (Azam), na Mwadini Ali (Azam). 
Mabeki ni Said Moradi (Azam), Shomari Kapombe (Azam), Oscar Joshua (Yanga), Nadir Haroub (Yanga), Kelvin Yondani (Yanga), Aggrey Morris (Azam), Miraji Adam (Simba), Charles Edward (Yanga) na Emmanuel Simwanda (African Lyon). 
Viungo ni Erasto Nyoni (Azam), Mwinyi Kazimoto (Al Markhiya, Qatar), Amri Kiemba (Simba), Himid Mao (Azam), Salum Abubakar (Azam), Said Ndemla (Simba) na Haruna Chanongo (Simba). 
Washambuliaji ni Khamis Mcha (Azam), Simon Msuva (Yanga), Thomas Ulimwengu (TP Mazembe, DR Congo), Mbwana Samata (TP Mazembe, DR Congo), Mrisho Ngasa (Yanga), Mwegane Yeya (Mbeya City), na Juma Liuzio (Zesco, Zambia). 
BONIFACE WAMBURA
MKURUGENZI WA MASHINDANO
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA
Endelea Kusoma >>
0 comments

MKUTANO WA SIKU MBILI JUU YA MABADILIKO YA TABIANCHI, UHAKIKA WA CHAKULA NA HAKI ZA ARDHI ULIOANDALIWA NA OXFAM PAMOJA NA FORUM CC WAANZA LEO 
 Jenerali Ulimwenguambaye ndiye mwezeshaji  akiendelea kutoa Mwongozo katika mkutano wa siku mbili juu ya mabadiliko ya Tabianchi, uhakika wa Chakula na haki za Ardhi mkutano ulioandaliwa na Oxfam pamoja na Forum CC

Robert Muthami Program Support Officer kutoka Pan African Climate Justice Alliance (PACJA) akitoa ufafanuzi juu ya baadhi ya mambo yanayohusu mabadiliko ya Tabianchi.
 Meza  ya Majaji wakiwa wanasikiliza kwa makini malalamiko ya walalamikaji kutoka Loliondo juu ya kuchukuliwa ardhi pamoja na Malalamiko kutoka Wilaya ya Kishapu.
Kushoto ni mmoja wa walalamikaji kutoka Loliondo akielezea kwa uchungu jinsi Muwekezaji alivyo wanyang'anya Ardhi yao na mpaka sasa hakuna kitu ambacho kinaendelea na wanahitaji kupata Msaada wa kisheria ili wapate rudishiwa Ardhi yao.
 Kushoto ni Mama kutoka Loliondo akitoa malalamiko yake Mbele ya Mahakama ya wazi Jinsi mwekezaji alivyochukua Ardhi, kusababisha uharibifu na akina mama kuteseka pamoja na wengine kuharibu Mimba zao pia kupoteza watoto ambapo mpaka sasa kuna mtoto hajaonekana.
 Mlalamikaji Mwengine kutoka Loliondo akielezea Mbele ya Mahakama ya wazi  jinsi ya eneo lao lilivyochukulia na mwekezaji, na kutaka agizo la Mh. Waziri Mkuu lifanyiwe kazi la kwamba ardhi ile ni ya wafugaji na wanatakiwa warudishiwe
Mmoja wa walalamikaji kutoka Wilaya ya Kishapu akitoa malalamiko yake mbele ya Mahakama ya wazi juu ya walivyo chukuliwa maeneo kwa ahadi ya kuyaendeleza na kuto fanya hivyo, na kuomba eneo hilo ambalo ni mashamba warudishiwe ili waendelee na kilimo kwa kuwa eneo hilo kuna shida ya njaa.
Mchangiaji kutoka Oxfam Bwana Marc akizungumza juu ya haki za binadamu na moja ya haki hizo ni haki ya kila mwanadamu kuwa na Chakula, na kuongezea kuwa hata Umoja wa Mataifa unafahamu hilo Pia amesisitiza kuwa ni jukumu la kila mtu kujua sheria za umiliki wa Ardhi
Mjumbe wa Bodi kutoka Forum CC akizungumza jambo wakati wa Mkutano huo

 Mmoja wa wachangiaji akizungumza Jambo
Mh. Jaji Richard Mzilay Akitoa Maelezo ya kina juu ya Walalamikaji kutoka Loliondo ambao walikuwa wana malalamiko ya Ardhi na Kishapu ambapo walikuwa wanataka Eneo lao lirudishwe, Ametoa maelekezo ya yale ambayo wanatakiwa wayafuate.

 

Washiriki wa Mkutano huo
 Mama Shujaa wa Chakula 2014 akichangia maada
 Burudani Elimisha ikiendelea
 Wadau wameguswa na kujumuika kucheza
 Picha ya pamoja

Endelea Kusoma >>

Monday, September 29, 2014

BREKING NEWZZZ WATU ZAIDI YA 200 WANUSURIKA KUFA

0 comments
ZAIDI YA WATU WAPATAO 200 WAMENUSURIKA KUFA BAADA YA KUNYWA KINYWAJI AINA YA TOGWA  KINACHODHANIWA KUWA NA SUMU KATIKA KIJIJI CHA CLITAPWASI MKOANI RUVUMA LEO HABARI ZAIDI TUTAWALETEA SOMA BLOG YA MZUKA
Endelea Kusoma >>
0 comments

TAASISI YA VYOMBO VYA HABARI KUSINI MWA AFRIKA(MISA-TAN) YAADHIMISHA SIKU YA KIMATAIFA YA HAKI YA KUPATA TAARIFA NA KUTOA MATOKEO YA UTAFITI WA UPATIKANAJI WA TAARIFA KWENYE OFISI ZA UMMA NCHINI TANZANIA‏

Mkurugenzi  wa Misa-Tanzania-Media Institute of Southern Africa (Taasisi ya vyombo vya habari Kusini mwa Afrika) Bwana Simon Berege (kushoto) akiwakaribisha wageni waalikwa na waandishi wa habari waliofika kweye mkutano wao uliofanyika Jana kwenye ofisi za MISA Tanzania  zilizopo jijini Dar es Salaam kulia ni  Mkurugenzi msaidi wa Misa-Tanzania-Media Institute of Southern Africa (Taasisi ya vyombo vya habari Kusini mwa Afrika) Bwana Andrew.
Misa-Tanzania-Media Institute of Southern Africa (Taasisi ya vyombo vya habari Kusini mwa Afrika) Jana imekutana na waandishi wa habari na wadau tofauti katika kuadhimisha Siku ya haki ya kupata taarifa kimataifa amabayo huadhimishwa kila mwaka Septemba 28.09.2014 katika ofisi zao zilizopo kinondoni Mkwajuni Jijini Dar es salaam.
 Mkurugenzi msaidi wa Misa-Tanzania-Media Institute of Southern Africa (Taasisi ya vyombo vya habari Kusini mwa Afrika) Bwana Andrew Marawiti (kulia) akizungumza jambo mbele ya waandishi wa habari(hawapo pichani) kwenye siku ya kimataifa ya haki za kupata taarifa zinazoadhmishwa septemba 28 kwa kila mwaka.
 Mkurugenzi  wa Misa-Tanzania-Media Institute of Southern Africa (Taasisi ya vyombo vya habari Kusini mwa Afrika) Bwana Simon Berege  (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari pamoja na wagene waalikwa (hawapo pichani) kwenye siku ya kimataifa ya haki za kupata taarifa zinazoadhmishwa septemba 28 kwa kila mwaka. kwenye ofisi za MISA Tanzania  zilizopo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi  wa Misa-Tanzania-Media Institute of Southern Africa (Taasisi ya vyombo vya habari Kusini mwa Afrika) Bwana Simon Berege (kushoto) akikata utepe wakati wa uzinduzi rasmi wa chapicho la ripoti ya matumizi bora ya utoaji wa habari katika sekta za umma hapa nchini.
 Mkurugenzi  wa Misa-Tanzania-Media Institute of Southern Africa (Taasisi ya vyombo vya habari Kusini mwa Afrika) Bwana Simon Berege akiwaonesha waandishi wa habari pamoja na wageni waalikwa kitabu cha ripoti ya haki ya kupata taarifa halali katika sekta za umma.
  Mkurugenzi  wa Misa-Tanzania-Media Institute of Southern Africa (Taasisi ya vyombo vya habari Kusini mwa Afrika) Bwana Simon Berege akitangaza taasisi iliyochukua tuzo ya Kofuli la Dhahabu kwa kubana sana taarifa kwa mwaka 2014.
  Mkurugenzi  wa Misa-Tanzania-Media Institute of Southern Africa (Taasisi ya vyombo vya habari Kusini mwa Afrika) Bwana Simon Berege akionesha tuzo ya Kufuli la Dhahabu kwa kubana sana taarifa kwa mwaka 2014 iliyokwenda kwenye Idara ya Mahakama.
   Mkurugenzi  wa Misa-Tanzania-Media Institute of Southern Africa (Taasisi ya vyombo vya habari Kusini mwa Afrika) Bwana Simon Berege akitangaza taasisi iliyochukua tuzo ya Ufunguo wa Dhahabu kwa mwaka 2014 kwa kutoa taarifa bila kificho kwa mwaka 2014
 Mkurugenzi  wa Misa-Tanzania-Media Institute of Southern Africa (Taasisi ya vyombo vya habari Kusini mwa Afrika) Bwana Simon Berege (kulia) akimkabidhi tuzo ya Ufunguo wa Dhahabu Kaimu Mkurugenzi wa Shighuli za Takiwimu ofisi ya Taifa ya Takimu Bi. Aldegunda Komba(kushoto) kwenye maadhimisho ya siku ya kimataifa ya haki ya kupata taarifa jana jijini Dar es Salaam
 Kaimu Mkurugenzi wa Shighuli za Takiwimu ofisi ya Taifa ya Takimu Bi. Aldegunda Komba akionesha tuzo hiyo kwa waandishi wa habari pamoja na wageni waalikwa waliofika kwenye ofisi za Misa-Tanzania-Media Institute of Southern Africa (Taasisi ya vyombo vya habari Kusini mwa Afrika) zilizopo eneo la Mkwajuni, Kinondoni jijini Dar es Salaam.
 Kaimu Mkurugenzi wa Shighuli za Takiwimu ofisi ya Taifa ya Takimu Bi. Aldegunda Komba akizungumza na vyombo vya habari baada ya taasisi yaokutwaa tuzo ya Ufungu wa Dhahabu.
 Afisa utafiti na maelezo wa Misa-Tanzania-Media Institute of Southern Africa (Taasisi ya vyombo vya habari Kusini mwa Afrika) Bwana Sengiyumva Gasirigwa akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari kwenye siku ya kimataifa ya haki ya kupata taarifa ambayo uadhimishwa septemba 28 kwa kila mwaka.
 Baadhi ya wageni waalikwa pamoja na waandhishi wa habari wakifuatilia shughuli zima iliyokuwa inaendelea kwenye ofisi za Misa-Tanzania-Media Institute of Southern Africa (Taasisi ya vyombo vya habari Kusini mwa Afrika) zilizopo jijini Dar es Salaam.
Siku Ya Kimataifa Ya Haki Ya Kupata Taarifa 
TANZANIA_Most Open and Most Secret Survey(1)
Endelea Kusoma >>

msama promotion atoa msaada

0 comments

 Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotions, Alex Msama akizungumza katika tamasha la Uimbaji na Uchangiaji wa Ujenzi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Segerea jijini Dar es Salaam na kuahidi kutoa sh. milioni 6 kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa kanisa hilo. Msama alikuwa mgeni rasmi katika tamasha hilo akimwakilisha Waziri wa Habari Vijana Utamaduni na Miochezo, Dk. Fenela Mukangala. 
 Mjumbe wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASAT) Alex Msama ambaye pia ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotions akizungumza katika tamasha la Uimbaji na Uchangiaji wa Ujenzi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Segerea jijini Dar es Salaam. Msama alikuwa mgeni rasmi katika tamasha hilo.
 Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotions, Alex Msama akizungumza katika tamasha la Uimbaji na Uchangiaji wa Ujenzi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Segerea jijini Dar es Salaam. Msama alikuwa mgeni rasmi katika tamasha hilo akimwakilisha Waziri wa Habari Vijana Utamaduni na Miochezo, Dk. Fenela Mukangala.
 Mchungaji Emmanuel Masanja 'Masanja Mkandamizaji' aliguswa na kutoa ahadi ya shilingi milioni 1 katika hafla hiyo.
"Mimi na familia yangu tutatoa milioni 1".
 Familia mbalimbali ziliguswa na kutoa ahadi za kuchangia ujenzi wa kanisa hilo.
 Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la KKKT Usharika wa Tabata Matumbi, Mchungaji Christosiler Kalata akimkabidhi Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotions, Alex Msama sehemu ya mchango walioahidi katika tamasha la Uimbaji na Uchangiaji wa Ujenzi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Segerea jijini Dar es Salaam. Usharika huo ulitoa ahadi ya sh. laki 7.
 Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotions, Alex Msama akipokea mchango wa Usharikia wa Kanisa la KKKT Usharika wa Tabata Matumbi kutoka kwa Mchungaji Kiongozi wa Kanisa hilo Christosiler Kalata .
 Familia mbalimbali ziliguswa na kutoa ahadi za kuchangia ujenzi wa Kanisa hilo.
 Watu mbalimbali waliahidi kutoa michango yao kwa ajili ya kufanikisha ujenzi wa Kanisa hilo.
Mwimbaji wa nyimbo za injili, Edson Mwasabwite alichangia kiasi cha sh. laki moja.

Na Mwandishi Wetu 

 

MJUMBE wa Baraza la Sanaa la Taifa (Basata), Alex Msama ametoa kitita cha sh. mil 6 katika harambee ya kuchangia ujenzi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika Segerea.



Msama ambaye alikuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo, alitoa kiasi hicho katika harambee hiyo ya kufanikisha ujenzi huo, iliyofanyika katika Ukumbi wa Diamond Jubelee jijini Dar es Salaam, huku akitoa na ushuhuda wa maisha yake mpaka kufikia hatua aliyofikia sasa.


Akizungumzia ushuhuda huo, Msama aliwataka waumini kuiga mfano wake kwa kujitolea bila ya kugeuka nyuma, kwani ana imani Mungu yupo na anatenda muujiza kama alioutenda kwake.

"Unajua mimi katika maisha yangu hakuna ninayemwamini zaidi ya Bwana Yesu, kwa kuwa bila ya yeye mie nisingekuwa hapa nilipo, kwa taarifa yenu wapendwa mimi nilishakuwa dereva taxi, nilishakuwa kondakta wa daladala, lakini Mungu ni mwema na anatenda muujiza mpaka mimi kuwa hivi," alisema Msama.

Msama ambaye ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotions, aliongeza kuwa hata hivi karibuni katika ajali aliyoipata akienda Dodoma licha ya kupinduka gari mara nne lakini alitoka akiwa hai.

Harambee hiyo iliyoenda sambamba na mnada, ilihudhuriwa na wasanii mbalimbali wa muziki wa Injili kama Masanja Mkandamizaji, Edson Mwasabwite aliyeimba wimbo wa Ni kwa neema tu.

Mbali ya kiasi hicho alichotoa, Msama pia alichangia katika mnada uliofanyika katika tamasha hilo na kununua mtungi wa gesi kwa sh. laki 5.
Endelea Kusoma >>
 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu