Saturday, November 29, 2014

0 comments

MATUKIO KATIKA PICHA AJALI YA CHOPA HUKO KIPUNGUNI DAR

 Helkopta aina ya Chopa iliyoanguka maeneo ya Kipunguni B Ukonga jijini Dar es Salaam, leo asubuhi na kuua watu wanne waliokuwemo akiwa ni rubani pamoja na askari watatu.
 Miili ya watu waliokuwemo kwenye helkopta hiyo ikiwa imekandamizwa na mabaki ya chopa hiyo.
 Sehemu ya mashuhuda wa maeneo hayo wakishuhudia ajali hiyo.
Helkopta inayosemekana inamilikiwa na TANAPA imeanguka na kuteketea kwa moto katika eneo la Kipunguni B Ukonga jijini Dar es Salaam leo asubuhi. 
Kwa mujibu wa mashuhuda, wamesema waliona helkopta hiyo ikipoteza uelekeo na badaye kuanguka chini hali iliyosababisha kishindo kikubwa baada ya kulipuka moto. 
Inasemekana ndani ya helkopta hiyo kulikuwa na watu wanne ambao wote wameripotiwa kufariki dunia.
Aidha imeelezwa kuwa katika ajali hiyo kulikuwamo na Askari 3 na rubani

*HELKOPTA YAANGUKA KIPUNGUNI DAR NA KUWAKA MOTO, YAUA

 Habari zilizotufikia hivi punde zinasema kuwa Helkopta inayosemekana kuwa inamilikiwa na Tanapa imeanguka huko maeneo ya Kipunguni, na kuuwa watu wote wanne waliokuwa wakisafiri na helkopta hiyo.
Mashuhuda wakiwa eneo la tukio.

Helkopta inayosemekana inamilikiwa na TANAPA imeanguka na kuteketea kwa moto katika eneo la Kipunguni B Ukonga jijini Dar es Salaam leo asubuhi. 
Kwa mujibu wa mashuhuda, wamesema waliona helkopta hiyo ikipoteza uelekeo na badaye kuanguka chini hali iliyosababisha kishindo kikubwa baada ya kulipuka moto. 
Inasemekana ndani ya helkopta hiyo kulikuwa na watu wanne ambao wote wameripotiwa kufariki dunia.
Aidha imeelezwa kuwa katika ajali hiyo kulikuwamo na Askari 3 na rubani Blog sufian mafoto
Endelea Kusoma >>
0 comments

MWANAMUZIKI BILEKU MPASI KUTOKA CONGO (DRC) NA MASHUJAA BAND KUFANYA ONESHO LA PAMOJA DISEMBA 12-2014 UKUMBI WA ASCAPE 1 MIKOCHENI JIJINI DAR ES SALAAM KUZITAMBULISHA NYIMBO MBILI MPYA ZA BAND HIYO

Rais wa Band ya Mashujaa, Chalz  Baba  
 Rais wa Band ya Mashujaa, Chalz  Baba (kushoto), akitoa burudani mbele ya wanahabari Dar es Salaam leo, kuhusu onesho hilo litakalofanyika katika ukumbi huo.. Kutoka kulia ni Meneja Mauzo wa Kampuni ya Bia ya Mabibo, Joseph Emanuel na Ofisa Uhusiano wa Band ya Mashujaa, King Dodo la Buche. 
 Ofisa Uhusiano wa Band ya Mashujaa, King Dodo la Buche (katikati) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu onesho hilo. Kulia ni Meneja Mauzo wa Kampuni ya Bia ya Mabibo, Joseph Emanuel na Rais wa Band ya Mashujaa, Chalz Baba
 Meneja Matangazo wa Band ya Mashujaa, Maxmilian Luhanga (katikati), akizungumza katika mkutano huo.  
 Meneja Mauzo wa Kampuni ya Bia ya Mabibo, Joseph Emanuel (katikati), akizungumza katika mkutano huo. Kampuni ya Bia ya Mabibo imedhamini onesho hilo. Kulia ni Ofisa Mauzo wa Kampuni ya Bia ya Mabibo, Salumu Kabanda.
Wanahabari wakichukua taarifa hiyo.



Na Mwandishi Wetu

MWANAMUZIKI mkongwe kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Bileku Mpasi, atafanya onesho maalum katika utambulisho wa nyimbo mbili mpya za bendi ya Mashujaa 

utakaofanyika Desemba 12 mwaka huu kwenye ukumbi wa Ten Lounge zamani Business Park.


Akizungumza Dar es Salaam leo  mratibu wa onesho hilo, King Dodoo la Buche, alisema kuwa Mpasi ambaye alitamba katika tasnia ya muziki wa dansi alipokuwa na gwiji, marehemu, Pepe Kale, atakuja na wasanii wengine ili kutoa burudani ya kiwango cha juu.

Dodoo alitaja nyimbo hizo mbili ambazo zitatambulishwa ni pamoja na Rafiki Sokoni na My Queen.

Aliwataka mashabiki wa muziki wa dansi nchini kujiandaa kushuhudia onyesho hilo linalotarajiwa kuwa la kihistoria hapa nchini.

Rais wa Mashujaa Musica, Chalz Baba, alisema kuwa wamejiandaa kutoa burudani nzuri na kuendeleza heshima yao ya bendi bora kwa mwaka wa pili mfululizo.


" Napenda kuwahakikishia wapenzi wa bendi yetu tutafanya kazi ya ubora wa juu, ni kawaida yetu kufanya kazi nzuri, tuna usongo,"  alisema Chalz.

Katika onesho hilo lililodhaminiwa na Kampuni ya Bia ya Mabibo  kupitikia kinywaji chake cha  Windhoek.

Akizungumza kwa niaba ya kampuni hiyo meneja biashara wa kampuni hiyo Joseph Emmanuel, alisema wameamua kudhamini utambulisho huo ili kuendeleza muziki wa dansi nchini kufikia hadhi ya kimataifa.

Alisema kuwa wapenzi 100 wa kwanza watakaoingia kwenye onesho hilo watapewa bia moja ya Windhoek Draught bure.

Mashujaa pia itatumbuiza nyimbo zake zilizotamba katika albamu zake za Risasi Kidole na Ushamba Mzigo.

Naye Rais wa Mashujaa Chalz Baba amewataka wapenzi wajiandae kupata burudani ya aina yake katika uzinduzi. (Imeandaliwa na mtandao wa www.habari za jamii.com)
Reply, Reply All or Forward | More
Endelea Kusoma >>
0 comments

MKURUGENZI WA BLOG YA UJIJIRAHAA ZIARANI NA WASAIDIZI WA KISHERIA  Khamisi Mussa 
 Safari ilianzia katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam. kuelekea Mwanza .(PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA) Mkurugenzi wa Blog ya UJIJIRAHAA.
 Nikiwa angani katika pozi
Nikiwa nashuka na abiria wenzangu Mjini Mwanza majira ya jioni.

 Nikiwa nimepozi huku abiria wenzangu wakiwa wana panda gari tayari kwakutoka Nje ya Uwanja na kuendelea na Safari ya mimi kuelekea Maeneo ya Bugando nilipo fikia kwa ndugu zangu. kupumzika .
 Nikipata Picha na Abiria wenzangu mara baada ya kuwasili Mwanza.
  Hapa ni Asubuhi  kuelekea Wilaya ya Magu. Safari ya kuanza kutembelea vituo hivyo.

 Mkurugenzi wa Blog ya UJIJIRAHAA, nikielekea Bukoba.
 Picha ya pamoja  ya wasaidizi wa Kisheria Wilayani Karagwe Kagera, wakiwa na wateja wao.
 Vikundi vya Ujasiliamali Wilayani Karagwe, wakifurahiya baada ya kikao chao na wasaidizi wa Kisheria kufanya Kikao cha pamoja , ambao waliokuwa na Matatizo mbalimbali , yakiwemo ya Migogoro ya Ardhi , naMigogoro ya kifamilia.

 Pichani  ni Picha ya jengo la Kanisa  ambalo liliharibiwa katika Vita ya kumpiga Idd Amini wa Uganda alipo ivamia Tanzania mnamo miaka ya 79, katika eneo la Kyaka  Mto Kagera , Wilaya ya Bukoba Mkoa wa Kagera.
 Nilibahatika kukanyaga Ardhi ya Karagwe, Pichani  nyuma yangu  ni Picha ya jengo la Kanisa  ambalo liliharibiwa katika Vita ya kumpiga Idd Amini wa Uganda alipo ivamia Tanzania mnamo miaka ya 79, katika eneo la Kyaka  Mto Kagera , Wilaya ya Bukoba Mkoa wa Kagera.
 Nikionyesha Kibao kilicho andikwa Karagwe, nahapo nilikula Kitu kinachoitwa Ngonja kwa Nsenene, ni aina ya ndizi ambazo hakuna zinapopatikana kwa urahisi ila ni hapo tu, hakika nilifurahi kula Ngonja kwa Nsenene , nikitu ambacho sijawahi kula , kwangu ilikuwa ni mara ya kwanza. hakika ni tamu sana.
 Nikitoka Uwanja wa Ndege wa Bukoba kuja Mwanza .
 Picha tofauti nilizo zipiga nikiwa angani, nikitokea Uwanja wa Ndege wa Bukoba kwenda uwanja wa Ndege wa  Mwanza.


 Picha niliyo ipiga nikiwa Ndani ya Ndege yenye ujumbe , unao kataza kuvuta Sigara ukiwa ndani ya Ndege.
 Najianda kuingia katika Ndege ya Fastjet nikitokea Mwanza kwenda Dar.
 Ni kiingia katika Ndege ya Fastjet nikitokea Mwanza kwenda Dar.
Baadhi ya  Picha nilizo zipiga nikiwa angani.


Nilipo tuwa katika Uwanja wa Ndege  wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaa.
Endelea Kusoma >>

BREKING NEWWZZZ HELKOPTA YAANGUKA NA KUUA WATU 4 JIJINI DAR ESSALAAM

0 comments
WATU 4 WAMEFARIKI DUNIA BAADA YA HELKOPTA INAYOMILIKIWA MALI ASILI  KUANGUKA KATIKA ENEO LA KIPUNGUNI NJE YA JIJI LA DAR ES SALAAM  MAENEO YA UKONGA KWA MUJIBU WA JESHI LA POLISI LIMETHIBITISHA KUTOKEA KWA AJALI HIYO ASBUHI  ENDELEA  KUSOMA BLOG YA MZUKA KUPATA HABARI ZAIDI
Endelea Kusoma >>

Friday, November 28, 2014

0 comments

Francis Dande Francis Godwin me Gadiola Emanuel Geofrey Adroph and 20 more... CC MUHIDIN MICHUZI Ahmad Michuzi Othman Michuzi sek david Nov 27 at 12:52 AM
 Mkurugenzi wa kwaya ya ‘Family Singers’ Daniel Misheto (kulia). Picha zote na Cathbert Kajuna wa Kajunason Blog.
Na Mwandishi Wetu.
WAZIRI MKUU, Mizengo Pinda ametajwa kuwa mgeni rasmi kwenye uzinduzi wa albamu ‘Usilie’ ambayo itapatikana kwenye DVD Desemba 7, mwaka huu.
Akizungumza Dar es Salaam jana kwenye mkutano na waandishi wa habari, Mkurugenzi wa kwaya ya ‘Family Singers’ Daniel Misheto, alisema hafla hiyo itafanyika kwenye Ukumbi wa PTA uliopo Uwanja wa Sabasaba, Dar es Salaam.
Mbali ya uzinduzi huo Misheto alisema pia wasanii mbalimbali wa filamu watanogesha siku hiyo.
 Aliwataja waimbaji wa injili ambao watakuwepo siku hiyo kuwa ni Leah Mudy, AIC (T) Vijana Chang’ombe, Accasia Singers, Papson Mastaki kutoka Kenya na Frank Hume kutoka Boston nchini Marekani watatumbuiza.
Uzinduzi huu umeratibiwa na Misheto Promotion, ambapo kabla ya uzinduzi huo kutafanyika huduma za bila malipo za kiafya na kitabibu kutoka kwa madaktari bingwa wa magonjwa mbalimbali, ambayo yamekuwa yakiikabili jamii.
Misheto ameyataja magonjwa hayo kuwa ni moyo, figo, kisukari na mengineyo ambapo huduma hiyo itatolewa na madaktari bingwa nchini.
“Huduma hii itaanza saa mbili asubuhi na itatolewa bure, ikiwemo ushauri na kwa wale ambao wataweza kutibika watatibiwa, ila ambao watakuwa kesi zao zimekuwa ni kubwa zaidi watapewa ushauri wa bure wa kuendelea na matibabu katika hospitali kubwa na hakutakuwa na kiingilio," alisema Misheto.
-- ----
Endelea Kusoma >>

WATU 11 WAMEFARIKI DUNIANI

0 comments
Watu 11wamefariki dunia papo hapo na wengine  kadhaa wamejewruhiwa baada ya basi dogo la Abiria aina ya toyota coster ambao abiria hao waliokuwa wanasafiria kugongana uso kwa uso na lori la mizigo katika eneo la Mkanyageni jijini Tanga asbuhi leo RADIO ONE STEREO
Endelea Kusoma >>
0 comments

*SHEIKH PONDA AIBUKA KIDEDEA RUFAA YAKE MAHAKAM KUU LEO

Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda (wa pili kushoto) akitoka katika chumba cha Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam baada ya kushinda rufaa ya kupinga hukumu iliyotolewa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ya kuvamia na kujimilikisha kwa nguvu kiwanja cha Markaz Chang’ombe jijini Dar es Salaam.
Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda akiwa chini ya ulinzi wa askari wa Magereza wakati  akitoka Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam.
Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda akitoka katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam baada ya kushinda rufaa ya kupinga hukumu iliyotolewa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ya kuvamia na kujimilikisha kwa nguvu kiwanja cha Markaz Chang’ombe jijini Dar es Salaam.
  Wafuasi wa Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda wakiwa nje ya Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam leo huku wakipaza sauti baada Sheikh Ponda kushinda rufaa ya kupinga hukumu ilitolewa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ya kuvamia na kujimilikisha kwa nguvu kiwanja cha Markaz Chang’ombe jijini Dar es Salaam. Hukumu hiyo ilitolewa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, mbele ya Hakimu Mkazi Victoria Nongwa, Mei 9, 2013. 
 Wafuasi wa Sheikh Ponda.
 Wafuasi wa Sheikh Ponda Issa wakitoka Mahakamani.
  Wafuasi wa Sheikh Ponda Issa wakitoka Mahakamani.
picha zote na DANDE
Endelea Kusoma >>
 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu