Friday, January 30, 2015

ROBO FAINALI AFCON 2015 NI VITA TUPU!

*Wakongo kumaliza ubishi kesho, Ghana, Guinea balaa

http://news.bbcimg.co.uk/media/images/74471000/jpg/_74471882_161377467.jpg
Taji linalosubiri mbebaji wake
http://static.allsports.com.gh/img/incoming/origs3434059/431253271-w1280-h960/DR-Congo-National-team.jpg
DR Congo
http://www.redpepper.co.ug/wp-content/uploads/2015/01/eq.jpg
Wenyeji Guinea ya Ikweta
FAINALI za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON- 2015) yamefikia patamu wakati kesho timu nane zilizofanikiwa kupenya kutoka kwenye makundi zitaanza kutupa karata zao katika mechi za Robo Fainali kuwania kucheza Nusu Fainali baadaye wiki ijayo.
Guinea ambayo ililinagana kila kitu na Mali katika nafasi ya pili ya Kundi D lililoongozwa na Ivory Coast jana ilipenya kwa kupitia turufu ya kura na kurejesha matukio matatu kama hayo kuwahi kushuhudiwa kwenye michuano mikubwa duniani ya Kombe la Dunia 1954 na 1990 pamoja na Kombe la Mataifa mwaka 1988.
Guinea na Mali zilishindwa kutambiana katika mechi yao ya mwisho kwa kutoka sare ya 1-1 ikiwa ni sare zao za tatu baada ya awali kufanya kama hivyo mbele ya Ivory Coast na Cameroon iliyooaga mashindano kwa kichapo cha bao 1-0 kutoka kwa vinara wa kundi hiyo Tembo wa Ivory.
Ndipo Shirikisho la Soka Afrika (CAF) likaamua kuzipambanisha timu hizo katika kapu la sadakarawe na Mali kuangusha kuwapisha wenzao kuendelea ambapo sasa Guinea wamepangwa kuumana na Ghana katika mechi ya tatu ya Robo fainali itakayochezwa siku ya Jumapili jioni.
Mechi zitakazochezwa kesho kwa mujibu wa ratiba ni Congo Brazzaville dhidi ya wapinzani wao wa jadi DR Congo pambano litakalochezwa saa 1 jioni kwenye uwnaja wa Bara kabla ya wenyeji Guinea ya Ikweta kupepetana na Tunisia katika mechi isiyotabirika kutokana na timu hizo kumaliza katika uwiano sawa kwenye makundi yao.
Wakongo wameshakutana mara tano katika michezo mbalimbali ya karibuni tangu mwaka 2000 na timu hizo zimeshindw akutambiana kwa kila mmoja kushinda mara mbili na kutoka sare moja.
Kupenya kwa Guinea kwa kutupia turufu ya sadakarawe inakumbusha michuano ya fainali za Kombe la Dunia za mwaka 1954 wakati Ugiriki ilipowazidi kete Uholanzi
Katika fainali hizo Ugiriki na Hispania zililingana katika kundi lao na turufu ikawabeba Ugiriki kwenda kwenye fainali na tuykio hilo lilijirudia tena kwenye fainali za mwaka 1990 Ireland iliibwaga Uholanzi katika zoezi kama hilo.
Katika fainali za Afrika za mwaka 1988 Algeria ilipenya mbele ya Ivory Coast baada ya kulingana kila kitu.
Mbali na michezo hiyo ya kesho, Jumapili kutakuwa michezo miwili kubwa linalosubiriwa kwa hamu kubwa ni Ivory Coast dhidi ya Algeria litakalochezwa usiku wa saa 4:30 huku Tembo wakiwa na wasiwasi na hali ya kiafya ya nahodha wao, Yaya Toure.
Timu zitakazofuzu hatua hiyo zitakutana kwenye nusu fainali zitakazochezwa katikati ya wiki kabla ya kufahamika timu mbili zitakazocheza Fainali itakayopigwa Februari 8 na kupatikana kwa bingwa mpya wa michuano hiyo baada ya wlaiokuwa watetezi Nigeria kukwama kwenye kwenye fainali hizo za Guinea ya Ikweta.

VUMBI LA LIGI KUU ENGLAND WIKIENDI HII LIPO HIVI

KIVUMBI cha Ligi Kuu England kinatarajiwa kuendelea tena wikiendi hii baada ya wiki iliyopita kusimama kupisha Raundi ya nne ya Kombe la FA na mechi za Nusu Fainali ya Kombe la Ligi (Capital One).
Chelsea ambao wamefanikiwa kufuzu Fainali za Kombe la Ligi kwa kuvaana na Tottenham Hotspur Machi Mosi kwenye uwanja wa Wembley, itashuka dimbani kesho kuvaana na Mabingwa Watetezi, Manchester City.
Kwa mujibu wa ratiba ya mechi hizo za wikiendi hii Kesho kutakuwa na mechi nane zitakazokutanisha timu 16 kabla ya Jumapili kushuhudiwa mechi mbili tu ambazo zitazikutanisha timu nne.
Mechi za kesho zipo hivi:
Hull City15:45 Newcastle United
Crystal Palace  18:00  Everton
Liverpool  18:00 West Ham United
Manchester Utd 18:00 Leicester City
Stoke City    18:00 Queens Park Rangers
Sunderland  18:00  Burnley      
West Bromwich 18:00 Tottenham Hotspur   

Chelsea  20:30 Manchester City
Jumapili:

Arsenal     16 : 30     Aston Villa     
Southampton   19:00 Swansea City

Uwanja wa Real Madrid kubadilishwa jina

http://www.larbes.com/photos/2010/1023-1110/large/image045.jpg
Uwanja wa Santiago
KLABU ya Real Madrid inajipanga kubadili jina la Uwanja wake wa Santiago Bernabeu ikiwa ni sehemu ya makubaliano ya udhamini na Kampuni ya Kimataifa ya Uwekezaji ya Petroli-IPIC yenye maskani yake Umoja wa Falme za Kiarabu. Wawili walikubali kushirikiana katika mkataba unaoaminika kuwa na thamani ya euro milioni 500 itakazovuna Madrid katika kipindi cha miaka 20 ijayo kuanzia Octoba mwaka huu. Mkataba huo unajumuisha haki ya kubadili jina la uwanja ambao umekuwa nyumbano kwa timu hiyo toka mwaka 1947. Uwanja huo pia ndio uliochezewa mchezo wa fainali ya Kombe la Dunia mwaka 1982. Sasa inaaminika uwanja huo utakuwa ukiitwa The Abu Dhabi Santiago Bernabeu. Rais wa klabu hiyo Florentino Perez amesizitiza kuwa urithi wa uwanja huo utaheshimiwa kwa kuendelea kubaki na neno Santiago Bernabeu. Perez amesema dhumuni kubwa la udhamini huo ni pamoja na kuukarabati upya uwanja huo na kuuongeza mpaka kufikia uwezo wa kubeba mashabiki 91,000 kutoka 81,000 wa hivi sasa
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu