Sunday, April 26, 2015

Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama ya Tanzania, Rais Jakaya Kikwete, akipungia wananchi wakati akiingia kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam, akitumia gari maalum la kijeshi huku akisindikizwa na Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange. Rais aliongoza watanzania kwenye sherehe za miaka 51 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Katika sherehe hizo ambazo kauli mbiu yake ni "Tudumishe mshikamano wetu, pigia kura ya ndio katiba inayopendekezwa", zilihudhuriwa pia na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Ali Mohammed Shein,  wananchi lukuki, na viongozi mbalimbali ambapo zilipambwa kwa gwaride maridhawa la vikosi maalum vya kijeshi, ikiwemo halaiki. Hali kadhalika ngoma za kitamaduni kutoka bara na visiwani, zikiwemo kwaya nazo zilinogesha sherehe hizo. Kama kawaida ndege vita nazo zilitawala anga la uwanja wa Uhuru.

Vijana wa Halaiki

Vijana wa halaiki wakionyesha ishara ya kudumisha mshikamano wetu


Komandoo wa JWTZ, wakitoka uwanjani baada ya kupita mbele ya Amiri Jeshi Mkuu katika gwaride lililofana

Komandoo wakipita mbele ya jukwaa kuu




Ngoma za kitamaduni

Askari wa kikosi cha anga

Mama Fatma Karume, mjane wa hayati Rais Abeid Aman Karume

Kwaya kutoka Mbeya

Asakari maalum wa wanamaji wa JWTZ (Marine special forces)

Rais Jakaya Kikwete, na Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohammed Shein, pamoja na viongozi wan juu wa serikali wakisimama kwa heshima wakati wimbo wa taifa ukipigwa

Amiri Jeshi Mkuu wa Mjeshi ya Ulinzi na Usalama, Rais Jakaya Kikwete, akikagua gwaride

EBU GONGA: hivi ndivyo inavyoelekea Rais mstaafu wa Awamu ya tatu, Benjamin Mkapa akimwambia Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad. Kulia ni Jaji Mkuu wa Zanzibar, Omar Makungu
NGABWE MLULU BLOG
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu