Home
»Unlabelled
» KURESHI UFUNGUO KUANZISHA SOKA YA WATOTO
KURESHI UFUNGUO KUANZISHA SOKA YA WATOTO
|
Mchezaji wa zamani wa timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars), Kureshy
Ufunguo (Kushoto) akioneshwa mipira inayofaa kwa ajili ya kufundishia
watoto kutoka kwa Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya Isere Sports, Abbas
Ally (Picha na Mpiga Picha Wetu.) |
|
Mchezaji
wa zamani wa Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars),Kureshy Ufunguo
(Kulia) akipokea jezi kwa ajili ya kuanzisha shule ya mafunzo ya watoto
wadogo (Picha na Mpiga Picha Wetu). |
|
Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya Isere Sports, Abbas Ally (Kulia)
akimkabidhi vifaa vya kuweka alama uwanjani wakati wa mafunzo mchezaji
wa zamani wa Simba na Taifa Stars, Kureshy Ufunguo aliyeamua kuanzisha
shule ya watoto. |
|
Na Mwandishi Wetu
MCHEZAJI
wa zamani wa Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars), Simba, Kajumulo
na Mirambo ya Tabora, Kureshy Ufunguo ameamua kurudi uwanjani safari hii
kuanzia Soka ya Watoto (Academy) ili kusaka vipaji vya wachezaji wa
kuunda Stars baadaye.
Akizungumza Dar es Salaam jana,
Kureshy ambaye aliwahi kuchezea Stars kwa nyakati tofauti alisema anaona
uchungu kuona timu ya Taifa inafanya vibaya mara kwa mara wakati kuna
watoto wengi wenye vipaji ambavyo vikiliendelezwa vitaibua wachezaji
wazuri.
Alisema amefanya mazungumzo na baadhiu ya maduka ya
kuuza vifaa vya michezo likiwemo Isere Sports na kuchagua vifaa ambavyo
ataanzia katika kufundisha watoto hao.
Kureshy alisema kwa
kuanzia atakuwa anawakusanya watoto katika Klabu aliyoianzisha Kitunda,
Kivule ambapo ataanza kuwafundisha kwa nadharia yaani darasani na
baadaye uwanjani ambako atatumia uwanja wa Shule ya Sekondari, Misitu,
Kivule Dar es Salaam.
Mkurugenzi
wa Masoko wa Isere Sports, Abbas Ally alisema Kampuni yake itasaidia
kutoa vifaa vya kuanzia mazoezi kama vikinga ugoko (shin guard), mipira
na jezi za mazoezi.
Alisema
Kampuni itaendelea kutoa misaada kwa mchezaji huyo kwani ni wachache
wenye ndoto ya kufufua soka ya Tanzania ambayo kwa sasa Stars haifanyi
vizuri katika mashindano mbalimbali ya kimataifa. |
|
Mchezaji wa zamani wa Simba na Taifa Stars, Kureshy Ufunguo (Kulia)
akiangalia kikombe kwa ajili ya zawadi wa timu katika mashindano
mbalimbali (Picha na Mpiga Picha Wetu). |
0 comments:
Post a Comment