IKIWA
ni
siku moja tu baada ya kuchaguliwa kwa muhula wa tano kuliongoza
Shirikisho la
Mpira wa Miguu Duniani, FIFA, Rais wa Shirikisho hilo, Sepp Blatter
(79), (pichani), amejiuzulu wadhifa huo, leo Jumanne Juni 2, 2015
Tayari
ametangaza kuitishwa kwa mkutano mkuu haraka iwezekanavyo, ili apatikane mrithi wake.
Kujiuzulu
kwa Blatter, ni sawa Mbuyu kuanguka, yalianza matawi na sasa Mbuyu wenyewe,
kwani wiki iliyopita, viogogo kadhaa wa shirikisho hilo, wametiwa mbaroni kwa
tuhuma za kupokea mlungula.
Akitanagza
uamuzi huo baada ya kuita mkutano na waandishi wa habari, Blatter alisema, “Maslahi
ya Fifa, ndiyo mapenzi yangu, na ndiyo sababu nimeamua kuchukua uamuzi huu,
kinachohesabika hapa kwangu mimi ni taasisi ya FIFA na mpira wa miguu duniani
kote.” Alisema Blatter wakati akitrangaza uamuzi huo mjini Zurich, Uswis
|
0 comments:
Post a Comment