Mratibu Mkazi wa Shirika la Umoja
wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro
Rodriguez, aliyeambatana na Mtaalam wa Mahusiano na Mawasiliano wa Umoja
wa Mataifa (UN) Tanzania, Hoyce Temu akiangalia moja ya documentary ya
TV katika banda hilo minayoonyesha wadau mbalimbali wanaotumia mtandao
huu ambao walipata kuhojiwa.
Mmoja wa wadau wa Modewjiblog,
Rehema Pascal akiuzungumzia mtandao wa habari wa Modewjiblog
alipotembelewa ofisini kwake wakati wa kurekodi 'documentary' hiyo.
Pichani juu na chini ni Mratibu
Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la
Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez akiangalia kazi mbalimbali
zinazofanywa kwenye mtandao wa habari wa Modewjiblog
alipotembelea banda hilo katika maonyesho ya 39 ya kimataifa ya
biashara Sabasaba yanaoendelea kurindima katika viwanja vya Mwl. J.K
Nyerere, barabara ya Kilwa, jijini Dar.
Mratibu Mkazi wa Shirika la Umoja
wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro
Rodriguez akiondoka mara baada ya kutembelea banda la Modewjiblog, lililopo katika banda la MeTL Group.
Meneja mwendeshaji wa mtandao wa habari wa Modewjiblog,
Zainul Mzige akitoa maelezo juu ya mtandao huo unavyofanya kazi zake
ambapo aliwataka vijana hao kutembelea mara kwa mara ikiwemo kufaidika
na nafasi za ajira zinazotolewa kwenye mtandao huo zikiwemo habari za
kitaifa na kimataifa, burudani, michezo, utamaduni n.k.
Meneja mwendeshaji wa mtandao wa habari wa Modewjiblog, Zainul Mzige (kulia) na Mwandishi mwandamizi wa mtandao wa habari wa Modewjiblog,
Andrew Chale wakikabidhi zawadi za fulana maalum kwa wadau
waliotembelea katika banda la mtandao huo katika maonyesho ya 39 ya
kimataifa ya biashara Sabasaba yanaoendelea kurindima katika viwanja vya
Mwl. J.K Nyerere, barabara ya Kilwa, jijini Dar.
Mwandishi mwandamizi wa mtandao wa habari wa Modewjiblog, Andrew Chale akikabidhi zawadi ya kofia na fulana kwa Mmiliki wa blog ya Kajunason blog, Cathbert Kajuna (kulia) aliyetembelea banda la mtandao huo.
Wadau wakiendelea kumiminika kwenye banda la Modewjiblog
katika maonyesho ya 39 ya kimataifa ya biashara Sabasaba yanaoendelea
kurindima katika viwanja vya Mwl. J.K Nyerere, barabara ya Kilwa, jijini
Dar.
Mwandishi mwandamizi wa mtandao wa habari wa Modewjiblog, Andrew Chale akikabidhi zawadi ya fulana na kofia kwa Mwandishi wa Michuzi blog, Chalila Kibuda aliyembelea banda hilo.
Mwandishi mwandamizi wa mtandao wa habari wa Modewjiblog, Andrew Chale (kulia) akitoa maelezo ya utofauti wa habari za kwenye magazeti na blog kwa mmoja wa wadau anayesoma habari mbalimbali katika mtandao huo, Peter Chilumba
0 comments:
Post a Comment