CHAMA
kikuu cha upinzani nchini Tanzania, CHADEMA, kimemteua rasmi Waziri Mkuu wa
zamani, Mh. Edward Ngoyai Lowassa, kuwa mgombea wake rasmi wa kiti cha Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika
Oktoba 25, 2015.
Mkutano
Mkuu maalum wa chama hicho ulioketi kwenye ukumbi wa mikutano wa Mlimani City
jijini Dar es Salaam leo Agosti 4, 2015, ulimteua Mh. Lowassa kuwa ndiye
atakuwa mgombea wake wa Urais na kwa hali hiyo anakuwa mgombea rasmi wa
vuguvugu la Umoja wa Katiba ya Wananchi UKAWA, unaoundawa na vyama vya upinzani
vya CUF, NCCR-Mageuzi, CHADEMA na NLD.
Hali
kadhalika, aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa CUF, Zanzibar, Juma Duni Haji,
amekihama chama hicho na kujiunga na CHADEMA na baadaye kuchaguliwa kuwa
mgombea mwenza wa Mh. Lowassa. Hii ni kufuatia makubaliano ya UKAWA, ambapo
mgombea mwenza ni sharti atoke CUF, ingawa matwaka ya kikatiba yanaelekeza kuwa
mgombea Mgombea mwenza wa kiti cha Rais, ni lazima atoke chama kimoja na
mgombea mwenza na hivyo Mh. Duni Haji akalazimika kukihama chama chake. Mh.
Lowassa amabye alikihama chama chake cha zamani CCM na kujiunga na UKAWA, hatua
hiyo imebadilisha sura ya siasa za Tanzania, kwa mujibu wa wachambuzi wa
masuala ya kisiasa, ambapo wanasema, uchaguzi wa mwaka huu utakuwa na ushindani
mkubwa, kwa vile vyama vikuu vya uopinzani vimeamua kuungana na kjusimamisha
mgombea mmoja kwa kila eneo, la Ubunge, Udiwani, Uwakilishi na Usheha.
Mh.
Lowassa na Mh. Juma Duni Haji, walichaguliwa kwa kura ya wazi, ambapo wajumbe
wa mkutano huo kupitia kanda zao waliulizwa kama wanawachagua au la na wote waliitikia kukubali kuwachagua.
Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe,
(wasita kushoto), Mgombea urais wa chama hicho, Mh.Edward Lowassa,
(watatu kulia), Mgombea mwenza wa Mh. Lowassa, Juma Duni Haji, (wanne
kushoto) na wanachama wapya wa chama hicho waliojiunga wakitokea CCM
wakishikana mikono kuonyesha mshikamano
Mtoto mkubwa wa Mh. Lowassa, Freddy (katikati), akiwa na marafiki zake, wakifuatilia mkutano huo
Wajumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA
Vijana wa 4U wakishangilia na kuonyesha mabango yanayomsifia Mh. Lowassa
Wageni waalikwa kutoka mataifa ya njeMh. Lowassa, (kushoto), mgombea mwenza Juma Duni Haji na mgombea kiti cha Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad
0 comments:
Post a Comment