Sunday, August 2, 2015

SHULE YA MSINGI KIBULUGWA MBAGALA YANUFAIKA NA MADAWATI 100 TOKA KCB TANZANIA

1
Meneja Biashara wa Benki ya KCB Tanzania, Tawi la Mlimani City Jijini Dar es Salaam, Benjamin Mgonja akiangalia daftari la Mwanafunzi wa darasa la sita katika shule ya msingi Kibulugwa ya Mbagala jijini Dar es Salaam John Mwaipopo(watano toka kushoto)wakati wa hafla fupi ya makabidhino ya  msaada wa madawati 100  kwa shule hiyo.Benki hiyo inaendelea na kampeni yake ya kutoa  msaada wa madawati 1000 kwa shule kumi za jijini Dar es Salaam.
2
Wanafunzi wa darasa la sita wa shule ya msingi Kibulugwa ya Mbagala jijini Dar es Salaam,kutoka kushoto Mwajuma Abdallah,Khalima Khalfan na Mwanaid Mwakipesile wakimsikiliza kwa makini Ofisa Uhusiano na wateja wa benki ya KCB Tanzania,Victoria Kisima akiwafafanua jambo liloandikwa katika daftari wakati wa hafla fupi ya makabidhino ya  msaada wa madawati 100  kwa shule hiyo.Benki hiyo inaendelea na kampeni yake ya kutoa  msaada wa madawati 1000 kwa shule kumi za jijini Dar es Salaam.
3
Baadhi ya wanafunzi wa shule msingi Kibulugwa ya Mbagala jijini Dar es Salaam wakiwa wamekaa kwenye madawati 100 waliyopewa msaada na benki ya KCB Tanzania wakati wa hafla fupi ya makabidhino ya  msaada wa madawati hayo  kwa shule hiyo.Benki hiyo inaendelea na kampeni yake ya kutoa  msaada wa madawati 1000 kwa shule kumi za jijini Dar es Salaam.
4
Baadhi ya wanafunzi wa  shule ya msingi Kibulugwa ya Mbagala jijini Dar es Salaam wakibeba madawati kuyapeleka madarasani baada ya kukabidhiwa rasmi msaada  wa madawati 100 na benki ya KCB Tanzania ikiwa ni sehemu ya mradi wa madawati 1000 kwa shule za msingi 10 za msingi jijini Dar es Salaam
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu