Friday, March 4, 2016

KONGAMANO LA MOYO WA MWANAMKE



Katika kuelekea siku ya mwanamke Duniani Kanisa la Living Water Centre Kawe kupitia huduma ya Wamama kanisani hapo ikiongozwa na mmbeba maono Mwalimu Lilian Ndegi wameandaa Kongamano linalojulikana kama “Kongamano la Moyo Wanawake”

 Kongamano hilo huwa linalofanyika mara moja kila mwaka Katika Kanisa la Living Water Centre Kawe chini ya mtumishi wa Mungu Apostle Onesmo Ndegi na Mwalimu Lilian Ndegi,Kongamano hili ni kwa kusudi la kuwajenga Wanawake kuwa na uwezo katika kumtumika Mungu na kujua nafasi yao ya kutumika aliyowapa katika ufalme Mungu.

Theme ya mwaka huu ni Mwanamke Mjenzi Mithali 14:1 Kusudi kuu la Kongamano ni Kuwafanya Wanawake kuwa watendaji katika ufalme wa Mungu na wawajibikaji na watekelezaji wa majukumu katika ngazi ya Familia,Huduma,Jamii na Taifa kwa ujumla.
Waimbaji Women of The Kingdom,Living Waters,More than Enough Band na wengine wengi.

Karibuni sana.



Mawasiliano 0713 580 400 


Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu