Saturday, April 30, 2016

Bingwa wa Kombe la Mama Shija kuzawadiwa medali 15 za dhahabu

Na Mwandishi Wetu

TIMU ya soka ya Wamang'ati FC ya Mbagala inaingia uwanjani leo kupambana na Uswahilini kwenye fainali ya mashindano ya kuwania ubingwa wa Kombe la Mama Shija zitakazofanyika uwanja wa Shule ya Msingi Kingugi, Mbagala Kiburugwa.

Muandaaji wa mashindano hayo, Fatuma Shija alisema jana Dar es Salaam kuwa maandalizi ya fainali hizo yamekamilika ikiwepo kuandaa zawadi za washindi ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Fatuma Mjema.

Alisema bingwa wa mashindano hayo ataondoka na zawadi ya Kikombe, Medali 15 za dhahabu, jezi seti mbili, mpira mmoja na mshindi wa pili atapata zawadi ya jezi seti mbili, mpira mmoja na medali 15 za fedha huku mshindi wa tatu atapata jezi seti moja na mpira mmoja.

Mama Shija alisema lengo la mashindano hayo ni kuwaweka pamoja vijana kutumia muda wao mwingi kujihusisha na michezo na kuibua vipaji vingi vya vijana watakaunda timu ya soka ya wilaya mpya ya Kigamboni.

Alisema baada ya kumalizika kwa mashindano hayo yatafuata mengine baaada ya miezo minne ikiwa ni mfululizo wa michezo kwa vijana.

Kabla ya fainali hizo kutakuwa na fainali nyingine za mchezo wa bao kati ya mabingwa wa mchezo huo kutoka Kilungule, Kiburugwa na wenyeji Kinguge.

mwisho
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu