Thursday, April 21, 2016



WATU wanaosadikiwa kuwa majambazi, wamenusurika kifo baada ya wananchi wenye hasira, kuyaweka “mtu kati” neo la Kariakoo jijini Dar es Salaam mida hii.
Msomaji wa K-VIS Blog amerusha picha zinazoonyesha majambazi mawili yakiwa hoi bin taaban kwenye eneo la tukio baada ya polisi wenye silaha kuwahi kwenye eneo hilo na kuyaokoa yakiwa tayari yanavuja damu.
Kama ilivyo kawaida, mamia kwa maelefu ya watu wanaotafuta mahitaji eneo hilo la Kariakoo waliyazingira majambazi hayo baada ya jaribio lao la kupora fedha kushindwa.
Taarifa kamili itawajia kadrizitakavyotufikia



 

 

Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu