Mwenyekiti wa MISATAN, Simon
Berege akizungumza na waandisshi wa habari kuhusu SIku ya Uhuru wa
Vyombo vya Habari. Kushoto ni Afisa Mafunzo wa TMF, Raziah Mawanga na
Mhariri Mtendaji wa Gazeti la Jamhuri na Makamu Mwenyekiti wa Jukwaa la
Wahariri (TEF), Deodatus Balile.(Picha na Modewjiblog)
Siku za Uhuru wa Vyombo vya Habari
ambayo hufanyika Mei 3 ya kila mwaka inataraji kufanyika jijini Mwanza
kwa mwaka huu ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Jaji Mkuu wa Tanzania,
Mohamed Chande Othman na kuhudhuliwa na viongozi wengine nchini na
wengine kutoka nje ya nchini ambapo kwa mwaka huu kaulimbiu ni KUPATA
TAARIFA NI HAKI YAKO YA MSINGI.
Akizungumzia sherehe hizo katika
mkutano na waandishi wa habari, Mwenyekiti wa MISATAN, Simon Berege
amesema sherehe za mwaka huu zinataraji kuwa na wageni zaidi ya 250
akiwepo Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Nnauye,
Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini, Alvaro Rodriguez na Mkuu wa
Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia
Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Zulmira Rodrigues.
Aidha Berege amesema kuwa siku ya
uhuru wa vyombo vya habari kwa mwaka huu itafanyika kwa siku mbili, Mei,
2 kutakuwa na kongamano ambalo litatumika kujadili hali ya uhuru wa
vyombo vya habari nchini na Mei, 3 ndiyo itakuwa siku husika ya
maadhimisho.
“Kikawaida huwa kuna mambo
tunafanya katika siku hiyo, tutawakumbuka waandishi wa habari
waliopoteza maisha kazini, tutawakumbuka waandishi wa habari maveterani
na waandishi wa habari waliopatwa na matatizo wakiwa kazini ... kwa
mwaka huu tutakuwa na mambo ya kipekee tofauti na miaka iliyopita,”
amesema Berege.
Pia ameongeza kuwa watapitia sheria
zinazohusu uhuru wa vyombo vya habari kama Cyber Crime Act 2015 na
Sheria ya Takwimu 2015 pia kuipitia miswada ya huduma ya vyombo vya
habari na uhuru wa kupata taarifa.
Mhariri Mtendaji wa Gazeti la
JAMHURI na Makamu Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri (TEF), Deodatus
Balile akizungumzia hali ya uhuru wa vyombo vya habari na haki ya kupata
taarifa ilivyo nchini. Kulia ni Afisa Mafunzo wa TMF, Raziah Mawanga,
Mwenyekiti wa MISATAN, Simon Berege na Ofisa Miradi katika Kitengo cha
Mawasiliano na Tehama UNESCO, Nancy Kaizelege.
Afisa Mafunzo wa TMF
0 comments:
Post a Comment