Saturday, April 23, 2016

Natalia Kanem -TASAF Beneficiaries Kibaha
Mkurugenzi Mkazi Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya Watu (UNFPA), Natalia Kanem (kulia) akifanya manunuzi ya bidhaa zinazotengenezwa na wanakijiji wa Vikuge ambao wamewezeshwa na mpango wa PSSN wa TASAF. (Picha na Modewjiblog)
Washirika wa maendeleo nchini wametembelea vijiji viwili Vikuge na Mwanabwito vilivyopo Wilayani Kibaha kwa ajili ya kutazama miradi ya kusaidia kaya masikini ambayo imeanzishwa kwa msaada wa fedha ambazo zinatolewa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) ambapo washirika hao wamekuwa wakitoa fedha ili kusaidia miradi hiyo.
Washirika hao wa maendeleo kutoka UN Tanzania, Idara ya Maendeleo ya Kimataifa ya Serikali ya Uingereza (DFID), Irish Aid, USAID na Shirika la Kimataifa la Misaada la Sweden (SIDA) ambao wamekuwa wakishirikiana na TASAF katika Mpango wa Kusaidia Kaya Masikini (PSSN).
Wakitoa taarifa mbele ya washirika wa maendeleo, wanavikundi kutoka Kijiji cha Vikuge wamesema kuwa kupitia mpango huo wameweza kuboresha maisha yao tofauti na jinsi ilivyokuwa awali.
Walisema kuwa maisha yao ya awali yalikuwa magumu lakini kutokana na msaada walioupata kutoka TASAF wameweza kuanzisha vikundi ambavyo vinawasaidia kuboresha maisha kwa kufanya biashara za mazao, nguo na chakula.
“Kuna mafanikio tumeyapata darasani mahudhurio yameongezeka, klini wamama wanakwenda na hata utapiamlo haupo tena kwa watoto kwa sababu ya TASAF kutusaidia,” alisema mwakilishi wa wanavikundi kutoka Vikuge.
TASAF Kibaha
Mratibu TASAF Kibaha, Goodson Hare, akitoa neno la ukaribisho kwa ujumbe wa washirika wa maendeleo nchini waliotembelea vijiji viwili Vikuge na Mwanabwito vilivyopo Wilayani Kibaha kwa ajili ya kutazama miradi ya kusaidia kaya masikini ambayo imeanzishwa kwa msaada wa fedha ambazo zinatolewa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF).
Akizungumzia ziara hiyo, Mratibu Mkazi wa Umoja wa MATAIFA NCHINI, Alvaro Rodriguez alisema wamefanya ziara hiyo ili kuona ni hatua gani imefikiwa na wanufaikaji na kuona ni changamoto gani bado zinawakabili.
“Tunaangalia changamoto zilizopo ili kuona ni jisni gani tunaweza kuwasaidia kama Mpango wa Kusaidia Kaya masikini ulivyo nab ado kuna wahitaji zaidi licha ya kuwa tumeshasaidia kaya Milioni1.1 kwa nchi nzima,
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu