Mkurugenzi Mkazi Shirika la Umoja
wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya Watu (UNFPA), Natalia Kanem
(kulia) akifanya manunuzi ya bidhaa zinazotengenezwa na wanakijiji wa
Vikuge ambao wamewezeshwa na mpango wa PSSN wa TASAF. (Picha na Modewjiblog)
Washirika wa maendeleo nchini
wametembelea vijiji viwili Vikuge na Mwanabwito vilivyopo Wilayani
Kibaha kwa ajili ya kutazama miradi ya kusaidia kaya masikini ambayo
imeanzishwa kwa msaada wa fedha ambazo zinatolewa na Mfuko wa Maendeleo
ya Jamii (TASAF) ambapo washirika hao wamekuwa wakitoa fedha ili
kusaidia miradi hiyo.
Washirika hao wa maendeleo kutoka UN
Tanzania, Idara ya Maendeleo ya Kimataifa ya Serikali ya Uingereza
(DFID), Irish Aid, USAID na Shirika la Kimataifa la Misaada la Sweden
(SIDA) ambao wamekuwa wakishirikiana na TASAF katika Mpango wa Kusaidia
Kaya Masikini (PSSN).
Wakitoa taarifa mbele ya washirika
wa maendeleo, wanavikundi kutoka Kijiji cha Vikuge wamesema kuwa kupitia
mpango huo wameweza kuboresha maisha yao tofauti na jinsi ilivyokuwa
awali.
Walisema kuwa maisha yao ya awali
yalikuwa magumu lakini kutokana na msaada walioupata kutoka TASAF
wameweza kuanzisha vikundi ambavyo vinawasaidia kuboresha maisha kwa
kufanya biashara za mazao, nguo na chakula.
“Kuna mafanikio tumeyapata darasani
mahudhurio yameongezeka, klini wamama wanakwenda na hata utapiamlo haupo
tena kwa watoto kwa sababu ya TASAF kutusaidia,” alisema mwakilishi wa
wanavikundi kutoka Vikuge.
Mratibu TASAF Kibaha, Goodson
Hare, akitoa neno la ukaribisho kwa ujumbe wa washirika wa maendeleo
nchini waliotembelea vijiji viwili Vikuge na Mwanabwito vilivyopo
Wilayani Kibaha kwa ajili ya kutazama miradi ya kusaidia kaya masikini
ambayo imeanzishwa kwa msaada wa fedha ambazo zinatolewa na Mfuko wa
Maendeleo ya Jamii (TASAF).
Akizungumzia ziara hiyo, Mratibu
Mkazi wa Umoja wa MATAIFA NCHINI, Alvaro Rodriguez alisema wamefanya
ziara hiyo ili kuona ni hatua gani imefikiwa na wanufaikaji na kuona ni
changamoto gani bado zinawakabili.
“Tunaangalia changamoto zilizopo ili
kuona ni jisni gani tunaweza kuwasaidia kama Mpango wa Kusaidia Kaya
masikini ulivyo nab ado kuna wahitaji zaidi licha ya kuwa tumeshasaidia
kaya Milioni1.1 kwa nchi nzima,
0 comments:
Post a Comment