Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki
Dkt. John Pombe Magufuli akibadilishana makabrasha ya mkataba na Rais wa Sudan
Kusini Salva Kiir Mayardit mara baada ya kukamilika kwa zoezi la utiaji Saini wa kuiwezesha Jamhuri ya Sudan Kusini kuwa Mwanachama
kamili wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).
Rais wa Sudan
Kusini akitia saini kwenye Mkataba wa Sudani Kusini kujiunga na Jumuia ya
Afrika Mashariki.
|
Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki
Dkt. John Pombe Magufuli akitia saini kwenye mkataba wa
kuiwezesha Jamhuri ya Sudan Kusini kuwa Mwanachama kamili wa Jumuiya ya Afrika
Mashariki (EAC).
Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki
Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir
Mayardit wakipiga makofi mara baada ya kufurahishwa na wimbo wa bendi ya Polisi
iliyokuwa ikitumbuiza Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki
Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na mgeni wake Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir
Mayardit pamoja na viongozi wengine, Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan watatu
kutoka kushoto na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa watatu kutoka kulia.
Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki
Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir
Mayardit kabla ya utiaji saini wa Mkataba wa Sudani Kusini kujiunga na Jumuiya
ya Afrika Mashariki ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Sudan
Kusini Salva Kiir Mayardit akipokea maua kutoka kwa mtoto Sharon Innocencia
Shiyo mara baada ya kuwasili kwenye viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam na
kulakiwa na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. John Pombe Magufuli.
Rais wa Sudan
Kusini Salva Kiir Mayardit akisalimiana na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa mara
baada ya kuwasili katika viwanja vya Ikulu kwa ajili ya Utiaji saini wa Mkataba
wa kujiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Rais Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia wakati Bendi ya Matarumbeita ilipokuwa ikitumbuza Ikulu jijini Dar es Salaam
0 comments:
Post a Comment