Warembo 14
wajitokeza Miss Tabata 2016
Na Mwandishi
Wetu
WAREMBO 14
wamejitokeza kushiriki katika shindano la kumsaka malkia wa Tabata mwaka huu ‘Miss
Tabata 2016’.
Mratibu wa
shindano hilo Joseph Kapinga alisema jana kuwa warembo hao wanaendelea na mazoezi
kila siku kwenye Ukumbi wa Da West Park, ulioko Tabata jijini Dar es Salaam.
Aliwataja warembo
hao kuwa ni pamoja na Latifa Dibwe (18), Salma Abeid (18), Fatma Mapunda (19),
Dinnah David (22) na Joyce Kweka (24).
Wengine ni
Neema Makwaia (22), Jesca Daniel (22), Sabrina Kipunga (22) Happiness Mnyeke
(20), Grace Matiko (20), Olanda Filima (19),Neema Zablon (21),Joyce Nyimbo (24)
na Noela Kyombya (24).
Naye Mkurugenzi
wa shindano hilo ambaye pia ni mkuu wa kambi, Godfrey Kalinga alisema kuwa
warembo hao wanafundishwa na Neema Mchaki ambaye alikuwa ni mkufunzi wa
shindano la Miss Ilala na Miss Tanzania 2014.
Kalinga aliwaomba
warembo wengine wenye sifa kujitokeza kushiriki kwenye shindano hilo ambalo
huvutia wadau wengi wa sanaa ya urembo nchini.
“Bado
tunapokea warembo, tunataka kufanya shindano la kihistoria mwaka huu na
tumepanga kuwapeleka washiriki kwenye mbuga za wanyama ili kupromoti utalii wa
ndani,” alisema Kalinga.
Aliongeza
kuwa washiriki watano watakaoshika nafasi za juu katika shindano hili wataiwakilisha
Miss Tabata kwenye shindano la Kanda ya Ilala ‘Miss Ilala’ na baadaye Miss
Tanzania.
Miss Tabata
inaandaliwa na Keen Arts ambayo ni kampuni tanzu ya Bob Entertainment wakati Ambasia
Mallya ndiye mrembo anayeshikilia taji la Miss Tabata.
Alizitaja
kampuni zilizothibitisha kudhamini Miss Tabata kuwa ni CXC Africa, Fredito
Entertainment, Saluti5 na Bob Entertainment.
0 comments:
Post a Comment