Friday, May 13, 2016


TANZANIA KUWA MWENYEJI WA MKUTANO MKUU WA WAKADIRIAJI MAJENZI, AFRIKA UTAKAOFANYIKA MWEZI AGOSTI 2016 JIJINI DAR ES SALAAM
 Rais wa Chama cha Wakadiriaji Majenzi Tanzania (TIQS), Samuel Marwa (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo (hawapo pichani), kuhusu Tanzania kuwa mwenyeji wa mkutano mkuu wa wakadiriaji majenzi, Afrika utakaofanyika Agosti 2016. Kutoka kulia ni Mjumbe wa chama hicho, Neema Shabani na Bahati Mbambe.
 Rais wa Chama cha Wakadiriaji Majenzi Tanzania (TIQS), Samuel Marwa (katikati), akisisitiza jambo katika mkutano huo. Kutoka kushoto ni Mjumbe wa chama hicho, Joseph Mhonda, Katibu wa chama hicho, Bernard Ndakidemi, Mjumbe wa Chama hicho, Bahati Mbambe na Mjumbe, Neema Shaban.
 Mjumbe wa Chama hicho, Bahati Mbambe (kulia), akisisitiza jambo.
 Mjumbe wa Chama hicho, Neema Shabani akisisitiza jambo kwenye mkutano huo.
 Mjumbe wa chama hicho, Joseph Mhonda akitoa ufafanuzi kadhaa baada ya waandishi wa habari kuuliza maswali.
 Wanahabari wakichukua taarifa hiyo.
Mkutano na wanahabari ukiendelea.


Na Dotto Mwaibale

CHAMA Cha WakadiriajiMajengo Tanzania (TIQS) kwa kushirikiana na Chama cha wakadiriaji majenzi Afrika (AAQS), watakuwa wenyeji wa mkutano mkuu wa Wakadiriaji Majenzi wa Afrika utakaofanyika tarehe 18 na 19 Agosti 2016 jijini Dar es Salaam.

Katika hatua nyingine chama hicho  kimemuomba Rais John Magufuli,awape kazi katika miradi ya ujenzi, ili aweze kupunguza upotevu wa fedha unaotokana udanganyifu unaofanywa na baadhi ya watu.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo asubuhi Rais wa TIQS,  Samweli  Marwa alisema kuwa, wamesikia kilio cha Rais kuhusu ufisadi unaotokea katika miradi mbalimbali ya ujenzi hapanchini, na kusababishia hasara kubwa Serikali.

‘’Sisi tuko tayari kutumia taaluma yetu, ilikumsaidia RaisMagufuli, kwani watu wamezidi kudanganya kwa lengo la kujinufaisha wenyewe’’ alisema.

Marwa alisema, Rais akiwatumia wao wataweza kupunguza gharama za ujenzi, pamoja na kujua gharama kabla ya kuingia mikataba mbalimbali.

Alisemakuwa, huduma ya ukadiriaji majengo ni nguzo muhimu katika kuchangia ufanisi na udhibiti wa gharama za ujenzi, ikiwa pamoja na ukamilishaji kwa muda wa miradi na kupata thamani ya fedha.

Marwa  alisemawao kazi yao, wanatathmini kabla ya kujenga  hivyo Rais atakuwa na uhuru wa kukubali mradi au lah, endapoataonagharamaimekuwakubwa.

Wakatihuohuo Chama hicho, kimemuomba Magufuli kuwa mgeni rasmi katika mkutano Mkuu wa Afrika wa wakadiriaji majengo unaotarajia kufanyika Agost 18 na 19 Jijini Dar es Salaam.

Marwa alisema kuwa, kwa kutambua umuhimu wakazi yao katika Taifa hili, wameona ni vema kama Rais angekuwepo katika mkutano huo iliaweze kujua mambo mbalimbali yahusuyo chama hicho.

Alisemakuwa, mada Kuu   katika mkutano huo ni’ kufikiaMalengo endelevu(SDGs)- mchango  wahuduma za ukadiriaji majengo’ yanayokusudia kuondoa umaskini, kupambana na udhalimu, kuleta usawa pamoja na kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi.

(Imeandaliwa na mtandao wa www. habari za jamii.com-simu namba-0712-727062)


Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu