Mwenyekiti wa muda wa Mtandao wa Wamiliki na waendeshaji mitandao ya kijamii nchini (TBN), Bw. Jochim Mushi
Na
Mwandishi wetu
Chama cha Wamiliki/Waendeshaji wa Mitandao ya Jamii nchini
'Tanzania Bloggers Network' – TBN inawaomba wanachama wake wote kutotumia
taarifa ama habari au picha yoyote kutoka katika mkutano wa maadhimisho ya
Uhuru wa Vyombo vya Habari (WPFD) unaofanyika kitaifa mkoani Mwanza.
Kamati Kuu ya Uongozi TBN imefikia hatua hiyo leo Mei 3, 2016 baada
ya kujadiliana na kujiridhisha kuwa kumekuwepo na taasisi za tasnia ya habari
ambazo zimekuwa zikiwatenga wanahabari wa mitandao ya kijamii (bloggers) na
kutotambua umuhimu wao wakati sehemu kubwa ya taarifa mbalimbali nchini
husambazwa na mitandao hiyo nanyingi zimekuwa zikitumiwa na magazeti na
televisheni.
TBN iliyosajiliwa rasmi serikalini Aprili, 2015 na kupewa namba
ya usajili; S. A 20008 inawataka wanachama wake kutotoa ushirikiano wa aina
yoyote kwa taasisi ambazo zinawatenga Bloggers.
Tunasikitika kufikia hatua hii ila hakuna jinsi. TBN itasikitika
na kumshangaa mwanachama wake au Blogger asiye mwanachama kutounga mkono agizo
hili, na kwenda kinyume na agizo hili. Muda umefika ‘Bloggers’ kudai heshima,
kutambulika na kuthaminika kama tasnia ya habari ingine yoyote.
0 comments:
Post a Comment