Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO
Hospitali
ya Rufaa ya Amana Jijini Dar es Salaam imeboresha huduma za afya kwa kuweka
mashine maalumu ya kutibu meno ijulikanayo kama (Ceramic dental machine) lengo
ikiwa ni kuboresha huduma hizo katika hospitali za umma.
Akiongea
katika mahojiano kwa njia ya simu Mganga Mkuu wa Hospitali hiyo Bw.Meshack
Simwela ameeleza kuwa kwa sasa wataweza pia kutoa huduma ya afya kwa viongozi
wa serikali pamoja na wabunge kupitia wodi maalum iliyotengwa kwa ajili yao ili
kupata huduma hiyo wanapokuwa jijini hapa.
"Tunaishukuru
sana Serikali yetu kwa kutuletea mashine hii maalumu kwa ajili ya magonjwa yote
ya meno na tunaishkuru pia kwa kutushauri kutenga wodi maalumu kwa ajili ya
kuwatibia viongozi mbalimbali wakati wakiwa hapa Dar es Salaam,ushauri huo
tumeupokea na tumeufanyia kazi", alisema Simwela.
Aliongeza
kuwa maboresho hayo yatasaidia wananchi kupata huduma bora za afya na kupunguza
gharama za matibabu na kuondoa usumbufu wa kwenda kutafuta huduma hiyo katika
hospitali binafsi.
Bw.
Simwela anabainisha kuwa mashine hiyo ilikuwa ikipatikana katika Hospitali
chache za binafsi na matibabu yake huchukua muda mwingi na gharama kubwa jambo ambalo lilikuwa
likiwaumiza wananchi wenye kipato cha chini, hivyo upatikanaji wa huduma hiyo
imekuwa msaada mkubwa sana.
Vilevile
aliongeza kwa kutolea ufafanuzi suala la huduma ya wodi maalumu itakayokuwa
ikitoa huduma za afya kwa viongozi na wabunge tayari imeshaanza kufanya kazi tangu mwezi
Machi mwaka huu ikiwa na vyumba viwili vya wagonjwa mahututi (ICU)
pamoja na vyumba 24 ambavyo vina sehemu ya kukaa, kulala pamoja na choo.
Aidha,
amefafanua kuwa matibabu katika wodi hiyo yanaweza kulipiwa kwa bima ya afya au
kwa fedha taslimu pia ameongeza kuwa wodi hizo hazijatengwa kwa ajili ya
viongozi pekee bali zinaweza kutumika pia kwa wananchi wa kawaida watakaoweza
kulipia gharama za matibabu zilizopangwa katika wodi hiyo.
Naye
Afisa Habari wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, David Langa amesema kuwa
kufunguliwa kwa wodi hiyo kumesaidia sana waganga kuwepo katika vituo vyao vya
kazi muda wote kwasababu huduma za afya kwenye wodi hiyo ni masaa 24 pia mganga
anapomtibu mgonjwa anapatiwa asilimia 30 ya gharama za matibabu yale papo hapo,fedha
hizo ni nje ya mshahara wa mwisho wa mwezi.
Ametoa
rai kwa Serikali kuongeza mashine hizo maalumu kwa ajili ya magonjwa ya meno na
kuziweka katika Hospitali mbalimbali ili kupunguza mlundikano wa wagonjwa wengi
katika Hospitali moja.
0 comments:
Post a Comment