Sunday, June 19, 2016

Na Mwandishi wetu Washington 

Makamo wa Kwanza Mstaafu wa Rais wa Zanzibar na Katibu mkuu wa Chama Cha Wananchi (CUF), maalim Seif Sharif Hamad, jana alimaliza ziara yake nchini Marekani iliyochukua muda wa wiki moja.
Makamo wa Kwanza Mstaafu wa Rais wa Zanzibar na Katibu mkuu wa Chama Cha Wananchi (CUF), maalim Seif Sharif Hamad (Picha na http://swahilivilla.blogspot.com/) Maalim Seif alikhitimisha ziara yake hiyo kwa mkutano wa hadhara ambapo alipata nafasi ya kuongea na Watanzania waishio nchini humu.
Katika Mkutano huo, mwanasiasa huyo gwiji nchini Tanzania alisema kuwa lengo la ziara yake ni kuuelezea ulimwengu kukhusu kile kilichotokea Zanzibar kufuatia uchaguzi wa Oktoba 25 na mwelekeo wa demokrasia nchini Tanzania kwa ujumla.
Aliielezea ziara yake hiyo nchini Marekani kuwa imezaa matrunda. “Sina budi kumshukuru Mwenyezi Mungu kuwa tumeeleweka na ziara yetu imezaa matunda” alisema Maalim Seif.
Sehemu ya hadhira wakimsikiliza kwa makini Maalim Seif
Kukhusiana na zoezi la uchaguzi wa mwaka jana Visiwani Zanzibar, Maalim Seif alisema kuwa, uchaguzi huo ulihudhuriwa na waangalizi wa Kimataifa na wa ndani kutoka pande zote za Muungano, Bara na Zanzibar, na wachunguzi wote hao walithibitisha kuwa uchaguzi ulikuwa huru na wa haki. “Waangalizi wote, wote kabisa, walikiri kuwa uchaguzi ulikuwa huru na wa haki”, alisisitiza kiongozi huyo na kuongeza kuwa “Ulikuwa uchaguzi bora kabisa kuliko chaguzi zote zilizotangulia Zanzibar”
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu