Naibu
Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akichungulia pango
lililopo katika msitu wa Mapangopori ya Amboni linalodaiwa kuwa ni njia
kuu ya
watu wanaohofiwa majambazi waliofanya mauaji katika Kitongoji cha
Kibatini,
Kata ya Mzizima, Tarafa ya Chumbageni, jijini Tanga.Watu wanane waliuawa
kwa kuchinjwa na watu hao wasiojulikana mapema wiki hii kwenye kijiji
hicho. Naibu waziri huyo ambaye alifuatana na Mkuu wa Majeshi, Jenerali
Davis Mwamunyange, na Mkuu wa Jeshi la Polisi, IGP, Ernest Mangu, pia
waliwatembelea wafiwa na kuwapa pole ambapo Naibu waziri ameapa Serikali
kuwasaka watu hao na kuwafikisha mbele ya vyombo vya sheria.
Naibu waziri Masauni akitembelea eneo hilo "hatari"
Naibu
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kushoto meza kuu)
akizungumza katika Kikao cha Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama
kilichofanyika katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga. Kulia meza kuu ni Mkuu wa
Mkoa huo, Martine Shigella. Watatu kushoto ni Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi,
Jenerali Davis Mwamunyange na Mkuu wa Jeshi la Polisi, Inspekta Jenerali,
Ernest Mangu (wapili kushoto). Viongozi hao wamekutana mkoani humo kwa ajili ya kuimarisha ulinzi na
usalama mkoani Tanga.
Naibu
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akitoa maelekezo kwa
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Leonard Paulo (kulia), mara baada ya kutoka
ndani ya pango lililopo katika msitu wa Mapangopori ya Amboni linalodaiwa kuwa
ni njia kuu ya watu wanaohofiwa majambazi waliofanya mauaji katika Kitongoji
cha Kibatini, Kata ya Mzizima, Tarafa ya Chumbageni, jijini Tanga. Katikati ni
Mkuu wa Kikosi Maalum kutoka Kikosi cha Kutuliza Ghasia Makao Makuu Dar es
Salaam, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi, William Mwampagale
0 comments:
Post a Comment