NA SHAMIMU NYAKI WHUSM
SERIKALI
kupitia Jeshi la polisi limewaasa vijana nchini kushiriki katika michezo
mbalimbali ya kuigiza yenye lengo la kutoa elimu kwa jamii ili iweze kupambana
na kuzuia uhalifu.
Wito
huo umetolewa jana jijini Dar es Salaam na Inspekta Salum Abdalah (pichani juu), kutoka Wizara
ya Mambo ya Ndani ya Nchi alipokuwa akitoa mafunzo kwa vijana kuhusu Umuhimu wa
kutoa elimu kuhusu kuzuia na kupambana na uhalifu nchini kupitia michezo ya
kuigiza.
Inspekta
Salum amesema kuwa miongoni mwa mikakati ya serikali ni kuwajengea vijana uwezo
wa kuwa na tabia njema na kupata kipato cha halali kwa kuwawezesha kupata
mafunzo ya stadi za kazi kwa lengo la kuimarisha na kukuza uchumi, pamoja na
kuwapa uwezo wa kuendeleza vipaji vyao.
“Ili
kuwawezesha vijana kuwa na tabia njema na kuwa na maadili yanayotakiwa hatuna
budi kuanzisha
mbinu za kuwawezesha kuanzisha vikundi vya ujasiriamali, ulinzi shirikishi na
kuwepo kwa mipango thabiti wa kushiriki katika mafunzo, semina na warsha
mbalimbali”. Alisema Inspekta Salum.
Inspekta
Salum ameongeza kuwa wananchi ,wadau pamoja na mamlaka zinazohusika na
maendeleo ya Vijana, Michezo na ujasiriamali kuwahamasisha vijana ili
waweze kujshughulisha na shughuli zinazoleta maendeleo
kwa taifa na kujiepusha katika vitendo vya uhalifu.
Mmoja
wa washiriki wa mafunzo hayo Bw Ismael Mnikite amesema mafunzo hayo
yamemuwezesha kuelewa umuhimu wa ulinzi shirikishi kwa vijana kwakua anaamini ndio
wenye uwezo mkubwa wa kushawishi jamii kujiepusha na vitendo viovu.
“Mafunzo
haya yameniwezesha kuelewa umuhimu wa kuwa mfano kwa jamii kwani nitatumia elimu
hii kupanua uwezo wa kutafuta miradi itakayoniwezesha kupata mikopo kutoka
kwa wawezeshaji ili nisipate tamaa ya kujiingiza katika uhalifu”.Alisema Bw.
Ismael.
Mafunzo
hayo yameandaliwa na Idara ya Maendeleo ya Vijana ili kuwasaidia vijana kuwa
raia wema na kushiriki ipasavyo katika shughuli za ujasiriamali na ulinzi wa
jamii kwa kutumia elimu na vipaji walivyonavyo.
Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Maendeleo ya Vijana Bibi. Venorose
Mtenga akizungumza na vijana kuhusu umuhimu wa kujiajiri kupitia ujasiliamali
katika mafunzo yaliyoandaliwa na Idara ya Maendeleo ya Vijana Julai 12, 2016
Jijini Dar es Salaam.
Hafidhi Omary akichangia mada katika mafunzo kuhusu umuhimu wa
kujiajiri kupitia ujasiliamali na filamu katika mafunzo yaliyoandaliwa na Idara
ya Maendeleo ya Vijana Julai 12, 2016 Jijini Dar es Salaam.
Zuhura Madaba akichangia mada katika mafunzo kuhusu umuhimu wa
kujiajiri kupitia ujasiliamali na filamu katika mafunzo yaliyoandaliwa na Idara
ya Maendeleo ya Vijana Julai 12, 2016 Jijini Dar es Salaam.
0 comments:
Post a Comment