Na
Raymond Mushumbusi WHUSM
Serikali
imeazimia kujenga na kuendeleza shule za michezo zilizopo katika mikoa yote
nchini kwa kipindi hiki cha Serikali awamu ya tano.
Azimio
hilo limetolewa leo Jijini Dar es Salaam na Naibu Waziri wa Habari Utamaduni
Sanaa na Michezo Mhe. Annastazia James Wambura wakati akizungumza na timu ya
mpira ya miguu ya wasichana ya Fc Vito Malaika katika hafla ya kukabidhi
Bendera ya Taifa kwa timu hiyo kwenda kushiriki mashindano ya mpira wa miguu ya
Helsinki Cup yatakayofanyika nchini Finland Julai 8 mwaka huu.
“Azima
ya Serikali ya Awamu ya Tano ni kuendeleza michezo nchini kwa kuibua vipaji vya
michezo na kuviendeleza kuanzia wakiwa shule” Alisema Mhe. Annastazia.
Mhe
Annastazia Wambura ameongeza kuwa Serikali ya Tanzania inashirikia na Serikali
ya Finland katika kuendeleza michezo shuleni na zaidi ya shule 462 nchini
zitafaidika na miradi ya michezo ya vijana inayofadhiliwa na Serikali ya
Finland.
Kwa
upande wake Balozi wa Finland nchini Tanzania Pekka Hukka amesema kuwa
wamedhamiria kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kuendeleza michezo
nchini hasa kwa vijana ili kujenga timu nzuri za baadae, na kwa sasa wanapeleka
timu za vijana kwenda kushiriki mashindano mbalimbali ya kimataifa ikwemo Helsinki
Cup linalofanyika nchini finland Julai 8 mwaka huu.
Naye
Meneja wa Timu ya wasichana ya mpira wa miguu ya Fc Vito Malaika Bakari
selemani ameipongeza Serikali kwa juhudi zake za kuendeleza michezo hasa kwa
vijana kwa kushirikiana na Taasisi mbalimbali na ili kuendeleza michezo na
kukuza vipaji kwa vijana Serikali na wadau wa michezo wametakiwa kuwekeza kwa
vijana ili kujenga timu zenye kuleta ushindani katika mashindano ya kitaifa na
kimataifa.
Naibu Waziri wa Habari Utamaduni
Sanaa na Michezo Mhe Annastazia James Wambura (wa pili kulia) akikabidhi Bendera
ya Taifa kwa nahodha timu ya mpira wa miguu Fc Vito Malaika Alia Fikiri (kushoto)
kwenda kushiriki mashindano ya Helsinki Cup nchini Finland Julai 8 mwaka huu
0 comments:
Post a Comment