Wednesday, July 13, 2016

TASWA QUEENS WAONDOKA NA MAKOMBE MAADHIMISHO YA SIKU YA WAANDISHI



 Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Nchini Kenya, SJAK, Mbais Criss, akimkabidhi zawadi ya Kombe la mchezaji bora  Nahodha wa timu ya TASWA QUEENS, Lightness Sirikwa Mayeye, baada ya kutangazwa mchezaji bora aliyejituma katika mchezo wao dhidi ya timu ya SJAK ya Kenya.

Timu hizo zilizoshiriki katika Bonanza maalumu la Maadhimisho ya Siku ya Waandishi wa Habari Duniani, lililofanyika kwenye Uwanja wa Luna Park Jijini Nairobi Kenya Leo Julai 9, 2016,  zilitoka sare ya 0-0 katika muda wa kawaida na kupigiana penati ambapo Taswa Queens waliibuka kidedea kwa mikwaju ya penati 4-3. Picha na Mafoto Blog
Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Nchini Kenya, SJAK, Mbais Criss, akimkabidhi Kombe la ushindi Kipa wa timu ya TASWA QUEENS, Somoe Ng'itu, baada ya timu hiyo kuifunga timu ya SJAK ya Kenya kwa mikwaju ya penati 4-3 baada ya timu hizo kutoka sare ya 0-0 katika muda wa kawaida. 

Timu hizo zilishiriki kwa pamoja katika Bonanza maalumu la Maadhimisho ya Siku ya Waandishi wa Habari Duniani, lililofanyika kwenye Uwanja wa Luna Park Jijini Nairobi Kenya Leo Julai 9, 2016.
Kiungo wa timu ya Taswa Queens,  Ester Zelamula (kulia) akimtoka mchezaji wa Sjak ya Kenya, Mercy Njue, wakati wa mchezo wa kirafiki katika Maadhimisho ya Siku ya Waandishi wa Habari Duniani, uliochezwa kwenye Uwanja wa Luna Park Jijini Nairobi Kenya Leo Julai 9, 2016. Katikati ni Lightness Sirikwa wa Taswa Queens akijiandaa kutoa msaada.
 Kiungo wa timu ya Taswa Queens,  Ester Zelamula (kulia) akimtoka mchezaji wa Sjak ya Kenya, Mercy Njue, (katikati) Kushoto ni Lightness Sirikwa wa Taswa Queens akijiandaa kutoa msaada.
 Zelamula akiambaa na mpira baada ya mtoka Mercy Njue..
 Winga wa Taswa Queens, Angela Msangi (kulia) akipiga shuti huku beki wa Sjak ya Kenya, Rebecca Magoma, akijaribu kumdhibiti bila mafanikio.
 Lightness (kulia) akichuana kuwania mpira na Mercy.....
 Kipa wa Tswa Queens, Somoe Ng'itu akituliza mpira wakati wa mechi hiyo
 Lightness akiambaa na mpira.....
 Mtanange wa Taswa Fc dhidi ya Sjak ya Kenya ukiendelea. Katika mchezo huo Sjak waliibuka na ushindi.
 Mshike mshike langoni mwa Sjak....
 Julius Kihampa (kulia) akijaribu kumtoka beki wa Sjak.......
 Khadija Kalili wa Taswa Queens (katikati) akimdhibiti Eveline wa Sjak....
 Angela Msangi akipiga shuti..........
 Angela Msangi akichuana kuwania mpira na beki wa Sjak Rebecca Magoma
 Ester Zeamula akifunga penati......
 Kipa wa Taswa Queens Somoe Ng'itu akiokoa penati ya Eveline....
 Kipa wa Taswa akibebwa juu kwa furaha baada ya kuokoa penati moja iliyowawezesha kuibuka kidedea.
 Picha ya pamoja kabla ya kuanza mechi hizo..
 Mazoezi ya kupiga danadana kabla ya mchezo wao...
 Katibu wa Chama cha Waandoshi wa Habari za Michezo Tanzania (Taswa) Amir Mhando akizungumza na wachezaji wa Taswa kabla ya kuanza kwa michezo hiyo.
 Picha ya pamoja
 Picha ya pamoja...
 Lightenss mazoezini.....
 Winga wa Sjak, Consolata Makokha (kushoto) akiambaa na mpira....
 Taswa Queens wakinyoosa misuri kabla ya mechi
 Muda wa mapumziko 
 Kikosi cha Taswa Queens
 Muda wa mapumziko
 Picha ya pamoja na viongozi...
 Picha ya pamoja na wapinzani wao
 Wachezaji wakisalimiana kabla ya kuanza kwa mtanange huo.
 Kikosi cha Taswa Fc
 Wachezaji wakisalimiana
 Taswa Queens wakishangilia baada ya kukabidhiwa kikombe chao
 Wakipozi kwa picha na Kombe lao baada ya kukabidhiwa.
Afisa kutoka Kampuni ya Bia TUSKER, Samuel Nzau, akimkabidhi Kikombe cha ushindi, Naohidha wa Sjak ya Kenya, Alex Boke baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 5-1 dhidi ya Wazee wa Taswa. Katikati ni Katibu Mkuu wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) Amir Mhando.
KAWAIDA:-
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu