Na Theresia Mwami - TEMESA
Ujenzi wa kivuko kipya cha Mv Pangani uko katika hatua za mwisho
na kinategemea kumamilika Julai mwaka huu na kuanza kutoa huduma.
Hayo yamesemwa na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme
(TEMESA) Mhandisi. Lekujan Manase alipotembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa
kivuko hicho ambao upo mbioni kukamilika kwa kuanza kutoa huduma kwa wananchi.
“Kivuko hiki kipo katika
hatua za mwisho za ujenzi wake na leo tumekuja hapa kukagua mitambo ya
kuendeshea kivuko (propulsion units) pamoja na injini zilizofungwa katika
kivuko hiki ili kukamilisha ujenzi wake na hatimaye kianze kufanya kazi”
alisema Mhandisi Manase.
Kwa upande wake Mkurugenzi kutoka Idara ya Huduma za Ufundi na
Umeme kutoka Wizara ya Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Dkt. William
Nshama alieleza kuwa ameridhishwa na kasi ya ujenzi wa kivuko hicho unaofanywa
kwa kiwango cha kimataifa na kuwa kivuko cha Mv Pangani kinatarajiwa kutoa
huduma kati ya Pangani na Bweni Mkoani Tanga baada ya ujenzi wake kukamilika.
Kwa mujibu wa kampuni ya Songoro Marine Transport LTD kivuko hicho
kina uwezo wa kubeba magari sita na abiria 100 kwa pamoja, na ni sawa na uzito
wa tani 50.
Kivuko kipya cha
Mv Pangani katika hatua za kukamilika kwa ujenzi wake, unaofanyika katika eneo
la Bandari ya Dar es salaam.
Picha zote na Theresia
Mwami,TEMESA
0 comments:
Post a Comment