NA
K-VIS BLOG/KHALFAN SAID
RAIS wa pili na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Serikali ya Zanzibar, Mzee Aboud Jumbe Mwinyi, (96), amefariki dunia
leo Agosti 14, 2016.
Mwinyi ambaye alikuwa akiishi Mji Mwema
Kigamboni jijini Dar es Salaam, tangu patokee “mchafuko wa hali ya hewa”
kisiwani Zanzibar, alikuwa akisumbuliwa na maradhi kwa muda mrefu.
Hayati Jumbe alianza kuitawala Zanzibar
mnamo Aprili 11, 1972 mara baada ya kuuawa Rais wa Kwanza wa visiwa hivyo,
Hayati Mzee Abeid Aman Karume Aprili 7, 1972.
Mzee Jumbe alitawala visiwa hivyo tangu
wakati huo hadi Januari 30, 1984 alipojiuzulu kufuatia msimamo wake wa kutaka
mabadiliko katika mfumo wa Muungano wa baina ya Zanzibar na Tanzania bara.
Mzee Mwinyi alizaliwa Juni 14, 1920
Mwenyezimungu ailaze roho yake mahala
pema peponi AMIN
0 comments:
Post a Comment