Saturday, September 24, 2016




WAZIRI Mkuu wa zamani wa Tanzania na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Taifa ya CHADEMA, Edward Lowassa amewatembelea wananchi wa mji wa Bukoba walioathirika na tetemeko la ardhi na kuwasihi Watanzania kuwasaidia wananchi hao kama ilivyo desturi yetu.
Akizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Meja Jenerali (mstaafu) Salum Kijuu Septemba 10, 2016 alipofika Ofisini kwake kumpa pole kufuatia tetemeko hilo lililotokea Septemba 10, 2016 na kuua watu 17. Lowassa alisema, amefika mkoani humo ili kutoa mkono wa pole kufuatia maafa hayo na kumpapole Mkuu wa mkoa huo kwa niaba yawananchi wa mkoa wa Kagera.
Nawasihi watanzania wenzangu tuendelee kujitolea kuwasaidia wahanga kama ilivyo desturi ya umoja wa kitaifa tulionao”. Ameandika Lowassa katika ukurasa wake wa Tweeter.
Baada ya kuona hali ilivyo sasa kwa baadhi ya wakazi wa mkoa huo kupoteza ndugu zao, nyumba na mali zao kuharibika, Lowassa ametumia ukurasa wake wa Twitter kufikisha ujumbe kwa jamii ya watanzania sehemu yoyote walipo duniani kote.
Ujumbe wa kwanza Lowassa aliandika “Poleni ndugu zangu Wa Kagera na mlioathirika na tetemeko, Tupeane nguvu ili tuvuke katika kipindi hiki kigumu pamoja”


 Lowassa akizungumza na wakazi wa Hamugembe, baada ya kutembelea eneo hio lililoathirika sana na tetemeko hilo


Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu