MWANDISHI wa habari marehemu Adolph
Simon Kivamwo,aliyefariki dunia wiki iliyopita akiwa na umri wa miaka
48, amezikwa Septemba 25, 2016 kwenye makaburi ya Kinondoni jijini Dar
es Salaam. Mamia ya wanahabari, Wafanyabiashara mashuhuri, viongozi wa
kisiasa, wananchi wakiongozwa na mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul
Makonda, walifurika kwenye mazishi hayo yaliyotanguliwa na ibada ya
kuaga mwili wa marahemu iliyofanyika viwanja vya wazi, Leaders Club,
jijini Dar es Salaam. Marehemu alifariki dunia baada ya kuugua kwa muda
mrefu maradhi ya Saratani ya Utumbo na ameacha mkecna watoto wanne.
Miongoni mwa watu mashuhuri waliohudhuria mazishi hayo ni pamoja na
Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Dkt. Reginald Mengi, Mbunge wa Kigoma mjini,
Zitto Kabwe, Mbunge wa Chalinze, Riziwani Kikwete, Mbunge wa Ubungo,
Saed Kubenea, na Mbunge wa Afrika Mashariki, Shy-Rose Bhanji. Pia
wahariri kutoka vyombo mbalimbali vya habari hapa nchini walishiriki
mazishi hayo
Home »Unlabelled »
Monday, September 26, 2016
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment