Home
»Unlabelled
» Waziri Nape apokea Milioni Kumi kutoka Skol Contractors Building Limited Kusaidia Waathirika wa Tetemeko Kagera.
Waziri Nape apokea Milioni Kumi kutoka Skol Contractors Building Limited Kusaidia Waathirika wa Tetemeko Kagera.
|
(a) & (b):Mwenyekiti
wa Kampuni ya Skol Building Contractors Limited
Bw.Vincent Massawe (kushoto) akikabidhi Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na
Michezo Mhe.Nape Moses Nnauye(kulia) kiasi cha Shilingi Milioni Kumi taslimu
leo jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kusaidia wakazi wa Mkoa wa Kagera waliyoathirika
na tetemeko la ardhi liliotokea hivi karibuni.
Na Shamimu Nyaki – WHUSM
Dar es Salaam.
Waziri
wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye amepokea kiasi cha Shilingi Milioni Kumi kutoka Kampuni ya Skol Building Contractors Limited.
Akipokea
fedha hizo leo Jijini Dar es Salaam kutoka kwa Mwenyekiti wa Kampuni hiyo Bw. Vincent Peter Masawe Waziri Nnauye amemthibitishia kuwa pesa hizo
zitawasilishwa kwa waathirika wa
tetemeko hilo ili zitatue changamoto zinazowakabili.
“Ninashukuru
sana kwa msaada wenu mmetambua changamoto wanazopata wenzetu,niwaombe
Watanzania wote tuendelee kujitoa kuwasaidia ndugu zetu waliopata maafa
haya”.Alisema Mhe.Nnauye.
Aidha
Mwenyekiti wa kampuni hiyo Bw.Vincent Peter Masawe amesema Kampuni yao imeguswa
na matatizo waliyopata wakazi hao wa
Kagera na ndio maana wameamua kuwasaidia
ili hali zao za maisha zireje kama zamani.
“Tumeamua
kuwasaidia wenzetu na tunaomba wafanyabiashara na Watanzania kwa ujumla popote
walipo waguswe na jambo hili na waunge mkono Serikali katika juhudi zake za
kuwasaidia waathirika wa tetemeko hili”. Aliongeza Bw.Masawe.
Katika
hatua nyingine Mhe. Waziri amewakaribisha wananchi wote katika harambee ya
kuchangia waathirika hao iliyoandaliwa na Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) itakayofanyika
Septemba 21 mwaka huu jioni katika Ukumbi wa Mwalimu Nyerere uliopo Jijini Dar
es Salaam.
|
0 comments:
Post a Comment