Posted by KHALFAN SAID on 07:07
Naibu
Waziri, akiangalia kiatu kilichotengenezwa kwenye kiwanda cha viatu
Karanga, kilichko gereza kuu la Karanga mjini Moshim, mkao wa
Kilimanjaro, wakati wa ziara yake ya kikazi majuzi, ambapo pia
alitembelea mpaka wa Tanzania na Kenya, wa Tarakea ulioko wilayani Rombo
mkoani Kilimanjaro
Naibu
Waziri, akiangalia kiatu kilichotengenezwa kwenye kiwanda hicho
Naibu
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni ya utengenezaji wa viatu kiwandani hapo.
Naibu
Waziriakiwasili eneola mpakani
Naibu
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni (katikati) akisikiliza maelezo
kutoka kwa Kamishna Mkuu wa Uhamiaji Mkoa wa Kilimajaro alipotembela mpaka wa
Tarakea wilayani Rombo Naibu waziri Masauni amesema kuwa licha ya changamoto
zinazojitokeza katika mipaka yote miwili ni lazima kuendelea kuimarisha ulinzi
kwenye mipaka hiyo na kudhibiti njia zote zisizo rasmi zinazotumiwa na
wahamiaji haramu pamoja na wafanyabiashara za magendo.
Naibu
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masaun akipewa maelezo na Afisa Mipaka
Holili Michel Amo, juu ya jiwe
linaloonyesha mpaka wa Tanzania na Kenya lililopo katika mpaka wa Holili
ambalo limekua likisogezwa na watu wasiojulikana hivyo kuharibu alama za
mipaka. Naibu waziri Masauni amesema kuwa licha ya changamoto zinazojitokeza
katika mipaka yote miwili ni lazima kuendelea kuimarisha ulinzi kwenye mipaka
hiyo na kudhibiti njia zote zisizo rasmi zinazotumiwa na wahamiaji haramu
pamoja na wafanyabiashara za magendo.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad
Masauni akisalimiana na Mkuu wa Gereza
la Karanga, Kamishna Msaaidizi wa Magereza, (ACP), Mkwiche mkoani Kilimanjaro wakati alipofanya ziara
katikaa Kiwanda cha viatu kilichopo katika gereza hilo ili kujionea uzalishaji wa bidhaa za viatu ambavyo Rais
Magufuli alitaka majeshi yote nchini kutumia viatu vinavyotengenezwa na Jeshi
la Magereza
Naibu
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni akipokewa na maafisa wa
Gereza la Karanga Moshi, mkoani Kilimanjaro wakati wa ziara yake kwenye
kiwanda cha kutengeneza viatu kinachomilikiwa na jeshi hilo
NA
MWANDISHI MAALUM, MOSHI
NAIBU
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni avitaka vyombo vya ulinzi na
usalama nchini kuzidi kuimarisha ulinzi katika mipaka ili kushirikiana na
Serikali katika mpango wa kupambana na uhalifu nchini.
Masauni
aliyasema hayo leo wakati alipofanya ziara katika mipaka ya Tarakea na Holili iliyopo mkoani Kilimanjaro ili
kujione changamoto zinazojitokeza katika mipaka hiyo ambapo tarifa zinaonyesha
kwamba kuna njia zisizo rasmi zaidi ya 265 zinazotumiwa kuptisha bidhaa za
magendo na wahamiaji haramu
Katika
ziara hiyo Naibu Waziri Masauni alivitaka vyombo vyote vya ulinzi na Usalama
nchini kuhakikisha vinaashirikiana kila mtu kwa nafasi yake ili kupambana na
uhalifu wa kupitisha bidhaa za magendo zinazopitishwa katika mipaka hiyo na
kuikosehsa serikali mapato.
Masauni
alisema kuwa Serikali ya awamu ya Tano ina dhamira ya kupeleka nchi katika
uchumi wa kati hivyo ni lazima kwa vyombo hivyo kudhibiti biashara zote
zinazopita kimagendo mipakani humo lakini pia kuepuka rushwa ili kupiga hatua
mbele za kimaendeleo.
Pamoja
na kuwapo kwa changamoto ya nguvu kazi na vitendea kazi serikali itahakikisha
inaaandaa maofisa wa kutosha mipakani humo ili kuongeza nguvu kazi wakati wa
operesheni zao na doria wakati wote.
Aidha
Masauni ametoa rai kwa watumishi wa vyombo hivyo kujiepusha na tabia ya
kushirikiana au kuwaficha wafanyabiaashara wanao jihusishaa na biashara ya
maagendo.
Naye
Mkuu wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Kilimaanjaro Kamishna Msaidizi Mwqaandanizi
Wilbrod Muutafungwa almueleza naibu Waziri huyo licha ya changamoto zilizopo
wanaendelea kuimarisha ulinzi katika maeneo yote ya mipaka kwa kufanya doria
mara kwa mara licha ya kwamba wafanyabiashara hao wa bidhaa za magendo kutumia
mbinu mbalimbali kukwepa ushuru lakini Jeshi la Polisi Mkoa wa Kilimanjaro
limeweza kuwatia mbaroni.
Awali
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masaun aliliagiza Jeshi la
Magereza kuzidi kuboresha viatu vinavyotengenezwa na kiwanda chao ili kujipatia
soko kubwa ndani ya nchi na nje.
Hayo
aliyasema jana kwa wakuu wa Gereza la karanga na viongozi wa kiwanda hicho
alipofanya ziara yake ya siku moja katika kiwanda cha viatu kilichopo katika
gereza hilo, mkoani Kilimanjaro
Aidha,
Naibu Waziri huyo alisisistiza Jeshi hilo kutekeleza agizo la Rais John
Magufuli kuhakikisha majeshi yote nchini yanatumia viatu vinavyozalishwa na
Jeshi la Magereza, hivyo ni muhimu kuendelea kuzalisha bidhaa zilizo bora zaidi
Haiingii
akilini maofisa wa majeshi mbalimbali nchini kuagiza viatu nje ya nchi wakati
viwanda vya ndani vinauwezo wa kuzalisha viatu bora zaidi vinavyodumu kwa muda
mrefu kuliko vinavyoagizwa kutoka nje ya nchi, alisema Masauni.
Masauni
alisema kwamba dhamira ya Serikali ya awamu ya tano ya kuipeleka nchi katika
uchumi wa kati hivyo Jeshi la Magerezaa kupitia kiwanda chake na miradi mingine
mingi halina budi kuendelea kuzidisha kuzalisha viatu bora vitakavyo kidhi
kiwango cha uhitaji na soko ili kukuza uchumi wao na Serikali kwa ujumla.
Aidha,
katika ziara yake, Naibu Waziri Masauni amesisitiza kuwa ni muhimu Jeshi hilo
kufanya miradi mingi kwa ustadi mkubwa ili kujipatia psa zitakazosaidia
kujiendesha wao kama jeshi na mashirika mengine yanayounga mkono miradi yao hivyo
kutotegemea ruzuku kutoka serikalini.
Waziri
huyo alilipongeza Jeshi hilo kwa kuzalisha bidhaa zenye ubora kulinganisha na
nyingine zinazoingizwa nchi, hivyo amesisitiza kuzidi kutengeneza viatu bora
zaidi ili kuwa na uwanja mpana wa soko la ndani na nje ya nchi.
0 comments:
Post a Comment