Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme TEMESA Dkt. Mussa Mgwatu (kulia) akitoa maelekezo kwa Mkuu wa Karakana ya Magari chuo cha Ufundi Arusha, Bw. Joseph Kotini wakati alipotembelea chuo hapo. |
Mkuu wa Karakana ya Magari Chuo cha Ufundi Arusha Bw. Joseph Kotini (kushoto) akitoa maelezo kwa Mtendaji Mkuu wa TEMESA Dkt. Mussa Mgwatu juu ya mtambo unaotumika kufanya ukaguzi na matengenezo makubwa ya magari chuoni hapo.
Picha
zote na Theresia Mwami TEMESA Arusha.
Arusha Bi. Rebecca Temba.
Na Theresia Mwami TEMESA Arusha.
Mtendaji
Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme TEMESA Dkt Mussa Mgwatu ameahidi kuziimarisha
karakana zilizopo chini ya TEMESA ili kuimarisha utendaji kazi.
Mikakati
hiyo imetolewa leo na Mtendaji huyo alipokutana na watumishi TEMESA wa mkoani
Arusha alipotembela kituo hicho kuangalia utendaji kazi wa kituo hicho.
“Naahidi
kushirikiana nanyi katika kuijenga TEMESA Mpya na naomba ushirikiano wenu na
muwe wafuatiliaji wa mambo kwani kazi zetu zinahitaji sana ufuatiliaji wa kina”
Alisema Dkt Mgwatu.
Ameongeza
kuwa amepanga mikakati namna ya kuyatambua madeni ya TEMESA pamoja na utunzaji
wa taarifa zake, kufanikisha utendaji kazi wa baadhi ya karakana,kuwezesha
urahisi wa mawasiliano kati ya TEMESA
makao makuu na vituo mikoani.
Amesisitiza
kuwa watumishi wanapaswa kufanya kazi kwa bidii ili kuondoa dhana potofu
iliyojengwa juu ya TEMESA kwa wateja wake kuwa wanafanya kazi kwa mazoea,
wajiimarishe katika utendaji kazi kwa kasi, ubora, weledi uadilifu,
ufuatiliaji, na uwajibikaji.
Katika
hatua nyingine Dkt. Mgwatu ametembelea Chuo cha Ufundi Arusha ili kujionea
shughuli mbalimbali za mafunzo yanayotolewa chuoni hapo na amefurahishwa na
vifaa vya kisasa vya kutengenezea magari vinavyotumika katika karakana ya chuo
hicho kwa ajili ya mafunzo kwa vitendo kwa wanafunzi wake.
Kwa
upande wake Mkuu wa Chuo hicho Dkt. Richard Masika alionesha nia ya
kushirikiana kwa ukaribu na TEMESA ili kuweza kuboresha mafunzo ili kupata huduma
zinazotolewa katika karakana za TEMESA.
Dkt.
Mgwatu yuko katika ziara ya kikazi kutembelea vituo vya TEMESA Kanda ya
Kaskazini ili kujionea changamoto na hali halisi ya utendaji kazi wa vituo
hivyo.
MWISHO
0 comments:
Post a Comment