Saturday, October 22, 2016

WAZIRI KAIRUKI AMALIZA ZIARA YA SIKU 2

  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angellah Kairuki, akipokewa na Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Felix Lyaniva, alipowasili Ofisi za mkuu huyo jana kwa ajili ya kuhitimisha ziara yake ya siku mbili kuwatembelea, kuwasikiliza na kuzungumza na wanufaika hao wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (Tasaf ) wa Manispaa za Kinondoni na Temeke jijini Dar es Salaam. 
Baadhi ya wanufaika wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (Tasaf ) na wakazi wa maeneo ya Sandali, wakiwa katika mkutano na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angellah Kairuki, kwenye Mtaa wa Mamboleo, Manispaa ya Temeke, jijini Dar es Salaam jana. (Picha zote na Kassim Mbarouk-www.bayana.blogspot.com)
Diwani wa Kata ya Sandali, Temeke jijini, Abel Tarimo, akitoa maelezo kuhusu masuala mbalimbali kwenye mtaa wake huo, kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angellah Kairuki, alipokuwa na mkutano na wanufaika wa Tasaf pamoja na wakazi wa maeneo hayo jana.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
MZUKA BLOG © Copyright 2014. All Rights Reserved.

Powered by MATERU FROM IBS.
imagem-logoRudi Juu