Na
Jacquiline Mrisho – MAELEZO, Dodoma
Wizara
ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi imejipanga kuhamishia Bodi ya Pamba katika Mkoa wa
Mwanza kabla ya Novemba 10 mwaka huu ili kuhakikisha wakulima wa pamba waliopo
katika mkoa huo wanapata huduma zilizo bora kwa ukaribu na haraka.
Hayo
yamesemwa leo mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhe. William Ole Nasha alipokuwa akijibu swali la
Mbunge wa Bukombe Mhe. Doto Biteko lililohoji juu ya hatua ya Serikali kwa
wakulima walioathirika na pembejeo zilizotolewa ambazo hazikuwa na ubora pamoja
na kuhamishia Bodi ya Pamba katika mkoa huo.
”ili
kuwafikia kirahisi wakulima wa pamba waliopo mkoani Mwanza, Wizara imeamua
kuhamishia Bodi hiyo katika mkoa huo na kwa taarifa zilizopo Bodi hiyo inatakiwa
kuhama haraka iwezekanavyo kabla ya Novemba 10 mwaka huu”, alisema Mhe.Ole
Nasha.
Kwa
upande wa matatizo ya pembejeo, Mhe. Ole Nasha amesema kuwa Serikali tayari ina
taarifa kuhusu tatizo lililowapata wakulima wa pamba katika maeneo mbalimbali
kwa kusambaziwa viuatilifu pamoja na mbegu ambazo hazikuwa na ubora unaotakiwa
hivyo kuathiri wakulima nchini.
“Serikali
iliiagiza Tropical Pesticides Research Institute (TPRI) kufanya uchunguzi wa
malalamiko ya wakulima ambao ulibaini kuwa viuatilifu hivyo vilikuwa na
utendaji hafifu hivyo Serikali itaanza kuzalisha mbegu bora za pamba za UK08
ili kuhakikisha tatizo hili halijirudii tena”, alisema Mhe. Ole Nasha.
Naibu
Waziri huyo amefafanua kuwa kufuatia changamoto hizo za uotaji wa mbegu,
Serikali iliamua kufanya majaribio ya utoaji wa mbegu ambazo zilikuwa
zikisambazwa hapo awali bila kujua ufanisi katika uotaji wake.
Amethibitisha
kuwa, matokeo ya jaribio hilo yamewezesha kutoa maelekezo kuhusu aina za mbegu
za pamba zenye sifa za msingi ambazo zitasambazwa kwa wakulima katika msimu wa
kilimo wa mwaka 2016/2017.
MWISHO.
0 comments:
Post a Comment