NA K-VIS MEDIA/MASHIRIKA YA HABARI
WAMAREKANI
wameamua tajiri mkubwa Donald Trump kutoka chama cha Republican kuwa Rais wa 45
wa nchi hiyo, baada ya matokeo ya kura kuonyesha, ameshinda uchaguzi huo kwa
kupata alama 276 dhidi ya alama 218 za mpinzani wake toka chama cha Democrat,
mwanamama Hillary.
Kinyume
na matarajio ya wengi kuwa Trump ambaye wakati wa kampeni alikuwa akikabiliwa
na shutuma kadhaa za kibaguzi na uzalilishaji, alipewa nafasi ndogo ya
kumshinda mpinzani wake, Bibi. Hillary Clinton wa chama cha Democrat.
Donald John
Trump alizaliwa mwaka 1946, huko Queens, jijini New York, akiwa ni mototo wa
nne wa familia ya Bw.Frederick C, na Mary MacLeod Trump.
Baba
yake Bw.Frederick Trump, alikuwa mjenzi na muendelezaji wa majumba ya
kibiashara, (kupangisha), akiwa amejikita zaiidi katika masuala ya ujenzi wa
nyumba za watu wa kipato cha kati (Middle income apartments) huko Queens,
Staten Island na sehemu Fulani huko Brooklyn, New York.
Donald
Trump, alikuwa ni kijana mwenye nguvu na akili nyingi, na wazazi wake
walimpeleka shule ya kijeshi huko New York akiwa na umri wa miaka 13,
wakitegemea nidhamu ya shule za kijeshi zitawezesha matumizi bora ya nguvu
alizokuwa nazo.
Trump
alifanya vizuri shuleni katika Nyanja za kushirikiana na wenzake lakini pia
kimasomo na kimfanya kuwa “nyota” na kio ngozi wa wanafunzi wakati akihitimu
mwaka 1964.
Wakati
wa mapumziko ya majira ya kiangazi, Trump alifanya kazi za baba yake za ujenzi,
na alijiunga na chuo kikuu cha Fordham, na baadaye kuhamia shule ya masuala ya
fedha ya Wharton, chuo kikuu cha Pennsylvania
na kuhitimu mwaka 1968 akiwa na shahada ya uchumi.
Trump alijiunga moja kwa moja na shughuli za biashara ya
baba yake, (Trump Organisation) mnamo mwaka 1971 na kufanya makazi yake pale
Manhattan na akawa maarufu miongoni mwa watu maarufu.
Trump akaanza kupata tenda kubwa kubwa za ujenzi wa majengo
pale Manhattan na hivyo kujiingizia mabilioni ya dola na kazi yake ilizidi
kukua siku hadi siku na kumuongezea umaarufu. Donald Trump si mwanasiasa, yeye
anachojua sana ni biashara, amekuwa mwanzilishi, Mwenyekiti, Rais, na Afisa
Mtendaji Mkuu wa Trump Organization kuanzia mwaka 1975 hadi sasa.
Pia ni Mwenyekiti wa Mahoteli na Makasino ya Trump, Donald J. Trump
amemuoa Melania na ana watoto watano, Donald Jr. Ivanka, Tiffany na Barron.
Akizungumza baada ya kutangazwa matokeo, Mgombea mwenza, Pence ndiye alikuwa wa kwanza kujitokeza kwenye jukwaa akiwa na familia yake. "Wamarekani wameongea, wamemchagua mshindi, rais mpya wa Marekani, Donald Trump." alisema Pence.
Akizungumza kwenye hafla hiyo fupi kwenye kambi yake mbele ya wafuasi lukuki mjini New York, Donald Trump akifuatana na mkewe na familia yake, alisema "Asanteni, asanteni sana, samahani kwa kusubiri sana, maana kulikuwa na mkorogo, asanteni sana, nimepokea simu kutoka kwa mama Clinton, anatupongeza na mimi ninampongeza yeye na familia yake." Alisema.
Ni taimu kwetu kuwa wamoja kama wamarekani, Nitakuwa rais wa Wamarekani wote ni hii ndiyo muhimu kwangu.
Akizungumza baada ya kutangazwa matokeo, Mgombea mwenza, Pence ndiye alikuwa wa kwanza kujitokeza kwenye jukwaa akiwa na familia yake. "Wamarekani wameongea, wamemchagua mshindi, rais mpya wa Marekani, Donald Trump." alisema Pence.
Akizungumza kwenye hafla hiyo fupi kwenye kambi yake mbele ya wafuasi lukuki mjini New York, Donald Trump akifuatana na mkewe na familia yake, alisema "Asanteni, asanteni sana, samahani kwa kusubiri sana, maana kulikuwa na mkorogo, asanteni sana, nimepokea simu kutoka kwa mama Clinton, anatupongeza na mimi ninampongeza yeye na familia yake." Alisema.
Ni taimu kwetu kuwa wamoja kama wamarekani, Nitakuwa rais wa Wamarekani wote ni hii ndiyo muhimu kwangu.
0 comments:
Post a Comment