JOSEPH MUNGAI AFARIKI DUNIA
NA
K-VIS MEDIA
WAZIRI wa zamani Bw. Joseph Mungai, (pichani), amefariki dunia
jioni hii ya Novemba 8, 2016.
Hospitali ya taifa Muhimbili, (MNH), imethibitisha
kupokea mwili wa marehemu kupitia kitengo chake cha wagonjwa wa dharura ambapo
hospitali hiyo ilithibitisha kifo chake.
“Tumepokea mwili wa marehemuJoseph Mungai kupitia
idara yetu ya magonjwa ya dharura na kuthibitisha kifo saa 11;20 jioni hii ya
Novemba 8, 2016.” Mkuu wa kitengo cha Mahusiano cha Hospitali ya Taifa
Muhimbili, (MNH), Aminieli Aligaesha amenukuliwa akithibitisha taarifa hizo.
Joseph
Mungai, alikuwa waziri tangu serikali ya awamu ya kwanza, na zilizofuatia kabla
ya kukihama chama cha mapinduzi wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka uliopita 2015 ambapo
yeye na mkewe walijiunga na CHADEMA.
Joseph Mungai akihutubia mkutano wa hadhara wa CHADEMA, baada ya kutangaza kujiondoa CCM
0 comments:
Post a Comment