Na
Theresia Mwami TEMESA
Kivuko
cha Magogoni kinakusanya hadi jumla ya shilingi milioni 17 kwa siku za kazi
kuanzia Jumatatu mpaka Ijumaa kutokana na kutoa huduma ya kusafirisha abiria, mizigo
na magari kwa kutumia vivuko vya MV Magogoni na MV Kigamboni.
Takwimu
hizo zimetolewa na Mkuu wa Kivuko cha Magogoni Mhandisi Lukombe King’ombe alipokuwa
akitoa taarifa ya kivuko hicho kwa Mtendaji Mkuu wa TEMESA Dkt. Mussa Mgwatu
alipotembelea kivuko hicho hivi karibuni.
Mhandisi
King’ombe aliongeza kuwa kwa sasa wanakusanya mpaka milioni 17 kwa siku za Juma
na kwa siku za mwisho wa wiki yaani Jumamosi na Jumapili kiasi hupungua kidogo kutokana
na abiria wengi kutotumia kivuko hicho.
Aidha Mkuu wa Kivuko cha Magogoni Mhandisi
Kin’gombe alimueleza Dkt. Mgwatu kuwa hali ya makusanyo hivi sasa inaridhisha
kwani abiria wengi wameanza kurudi kutumia kivuko hicho baada ya kujiridhisha
kuwa MV Magogoni imerudi kutoka kwenye
ukarabati mkubwa na sasa inafanya kazi vizuri.
Kwa
upande wake Dkt. Mgwatu alimuagiza Mhandisi King’ombe kuhakikisha kuwa wanaziba
mianya yote ya upotevu wa mapato kivukoni hapo ili kuhakikisha wanafikia lengo
la kukusanya shilingi milioni 19 kwa siku ambayo ni agizo la Waziri wa Ujenzi,
Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Profesa Makame Mbarawa alipotembelea kivukoni hapo
mapema mwezi Oktoba mwaka huu.
Mtendaji
Mkuu wa Wakala wa Ufundi TEMESA alitembelea na kukagua kivuko cha Magogoni ili
kujiridhisha utendaji kazi wa kivuko hicho.
MWISHO
0 comments:
Post a Comment